Salama Na Fid Q Ep 7 | NGOSHA WA MBASA Part 2
Вставка
- Опубліковано 14 бер 2020
- #YAHStoneTown #SalamaNa #PodCast
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcasts Link apple.co/2Ou1bru
UA-cam Link bit.ly/UA-camSalamaNa
NGOSHA WA MBASA
Nakumbuka kipindi ambacho Fidi alikua anaamini kabisa kama kuweka ‘uso wa mbuzi’ ndo kulikua kunakufanya uwe ‘hard core’, sina uhakika lini aliachana na dhana hiyo ila kwa kipindi cha miaka miwili au zaidi tabasamu na bashasha vimekua havibanduki kwenye uso wake, jambo ambalo mimi kama rafiki nalifurahia sana. Nakumbuka baadhi ya marafiki zangu wa kike ambao ni wapenzi haswa wa mziki wake walikua wakiniambia eh, sema rafiki yako mgumu jamani, Kha! Mi hucheka tu na baadae wakishazoeana basi sidhani kama kuna hata mmoja anaweza kusema kitu kibaya kuhusu yeye. Nilikua nacheka kwasababu mimi naamini namfahamu rafiki yangu huyu, yeye hupenda sana matani, na kucheka na marafiki wa karibu wanaweza wakathibitisha hilo maana katika watu ambao unaweza ukawatania weeee mpaka asubuhi, na utani mpaka wa vitu vyengine ambavyo wewe wa karibu unaweza kusema ey, hiyo sasa imepitiliza, yeye waala... Atacheka tu!
Mwenye kipaji chake cha kujifunza mwenyewe, nasema hivyo kwasababu nadhani kufahamiana kwetu na kuelewana kwetu pia kunatokana na kuwa na vitu vinavyofanana ndani yetu. Kajifunza jinsi ya kupenda kusoma vitabu mwenyewe, kujifunza jinsi ya kuandika na kurap mwenyewe, kajiendeleza mwenyewe (bila ya shaka kuna watu walomsaidia kwa tafu za hapa na pale ila walitokea baada ya kuona jitihada zake). Alihakikisha anasafiri kwenda nje ya nchi na Africa kwa jitihada zake mwenyewe na mpaka leo, kukiitwa watu ambao wamesaidia kwa kiasi kikubwa kufikisha Hip Hop ya nyumbani hapa ilipo basi jina lake litakua ni miungoni ya yale yatakayopata heshima ya juu kabisa. Pia anachekesha sana. Uelewa wake wa baadhi ya vitu unaweza ukakuacha mdomo wazi wakati mwengine. Kwenye uwepo wake? Vicheko lazima vitawale.
Hii siku nilitia nae story haikua kama kazi, bali kama mtu na rafikiye tu wakitia story juu ya njia za maisha ambazo tumepitia mpaka sasa. Fidi amekuzwa na Mama yake ambae alikua ni mfanyakazi wa serikalini (ameshastaafu), alikulia mkoani kama wengi wetu, alifika Dar akakaa kwa ndugu kama wengi wetu, alianzia sehemu na kutoka hapo mdogomdogo akajijenga kufikia hapa alipo. Humu tumeongelea hayo, watoto, muziki, ndoa, maisha ya wasanii na maendeleo kwa ujumla. Yangu matumaini uta enjoy na kuelewa baadhi ya vitu zaidi na zaidi.
Here’s to Ngosha wa Mbasa.
Love,
Salama.
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown - Розваги
Mafanikio ni nini? Jitengenezee tafsiri yako kisha ishi nayo🙌🏽🙌🏽🙌🏽 Ahsante fid
Hii ni zaidi ya shule asente salama kwa kutuletea mtu kama hyu anaetujenga kwa maongezi herimu nzuri sana hii...
Ngosha, we jamaa nakukubali always. Umenifanya niipe kazi akili yangu kuchanganua maana ya maneno kwenye mistari ya nyimbo zako. Binafsi sijutii kufahamu pamoja na kusikiliza chochote kinachotoka kinywani mwako coz naamini utakuwa hujakitoa kwa bahati mbaya.
Best interview ever
Tofauti kabisa na mkasi
Yani kama ndo mara ya kwanza fid kuhojiwa na Salama
Fid ashawahi kuhojiwa wewe na salama ingia mkasi
Broo jiongeze ...soma upya hiyo comment....#usikurupuke
Yan muuliza maswal ametulia kwenye kuuliza na anaejibu maswal ametulia kwenye kujibu..
Best interview
Nampenda Bure salama namna alivyopoz sio wanahabr wengine huwez jua nan ana muitaview muingine coz wote unakuta waongeaz mpka c poah but hapa salama karelax fid Q anaflow vzr sana. Love you all .
Naenjoy na kujifunza kwenye kila interview ninayo kusikiliz na uwa siachi interview yoyote inipite ambayo umeojiwa. WE NI DARASA LINALOTEMBEA, MZIKI WAKO NI SHULE TOSHA
Jamaa nilikuwa simfuatilii ila ep ya kwanza na hii haijaisha nataman kutafuta intview nyingine zaidi umeongea point pia hilo n darasa kabsa
Hiki kichwa hiki ,kweli maisha NI elimu na SI ya darasani NI vitabu tu,Kisha uhalisia !!,
Yaani Fid Q is so deep, appreciate you sharing your story and experiences especially around single parenthood and blended family life. You are doing a great job and an exemplary role model for others in similar circumstances. Asante bro, continue living your truth 🙏🏽
Fid Q ni chanzo cha busara yangu
Unaeza mckiliza fid badae ukahisi ulisoma ktabu Cha professor flan.......MAY GOD BLESS U MUCH BRO
Exactly, Mafanikio ni kujitengenezea tafsiri yako na kuiishi kila siku..
Ila Salama umenichekesha, ukaamua kumalizia na ya Fid eti..
kama kuna kitu mmegundua kweny hii interview...sio intervention ya mwaka huu niya mwaka jana....kwhyo ilkuw imefanywa tayar...🔥🔥🔥
Ni pale aliposema mwaka huu godzilla amepotea, Kumbe ilikuwa ni mwaka jana yan 2019
Ndio kifo cha zilla
Sawa kabisa,
Lkn pia kuna madini ambayo si ya Mwaka huu ni ya miaka 100 ijayo.
Makini sana
Salama big up,can you bring his friend Nikki wa Pili
Interview iko vzr san jinsi unauliza maswali na anavyojibu iko poa sana nadhan ndio salama na best mpaka sasa lakini jaribu kumpa airtime Niki mbishi amwage madini yake
Haswaaa
The best hip hop artist ever in tanzania
sema salama ni kizuri kinyama big up sn kwahuyo muhuni anae ishi na huyu manzi
Nimetaman sana hii interview isiishe madini ya ghali sana yapo humu
Mrete na joseph kusaga
Fid Q ni mwalimu.
Fid nakuelewa sana... nakumbuka KAN Festival nlivamia jukwaa ulivyopanda tu... duh nakukubali sana bro
Dah nimepata faida kubwa sana kuingalia hii interview kwani nimejifunza kitu kikubwa sana kutoka kwa fid q
safi!
Muda Kama ni Mdogo sana kuna madini mengi sana yamebaki kwenye hicho kichwa
Therealjoh fact
Iv ndo inaishia hapa!!??
lov this women no reason
Nimependa show ilivyoisha 👏👏
Salama na #Djfetty itakua poa sana
Madini tosh namkubali ngosha
mmmetisha sana wakongwe
Sio mnaojiwa na wasafi basi kelele nyingi sana
Salam kipind Chako kizur ila Jitahdn Saut Maik Unaziweka Mbalii Sanaa hautisikii Vzr
Daah natama niwe naangalia anavyo hojiwa fid q everyday
Napenda interview za hv sio zile za no comment
Changa moto IPO kwenye saut hatuwasikii vzr lifanyieni kaz tu enjoy kpind
Nimempenda sana mama faridi ni mama bora. Huwezi kuweka chuki kwa mtoto kwa matatizo yenu ambayo yy hayamuhusu baba atabaki kua baba na mama atabaki kua mama haiwez kubadirika
Thanks fid Q God bless you
Salama tuletee mnyamwezi P funk majani militisha sana kwenye Mkasi.
igot u broo
Kinachoniumizaga ni watangazaji waloshindwaga kuuliza maswali kuhusu maisha ya fid na rado hadi kufikia kuwa na beef
Rado alikuwa mshikaji wake ijapo sio kivile Ila alitaka kutoka kwa kupitia fid q
#madsoft
vibe up salama kipindi leo kizur ila vibe up maan
Nomaa sanaa hii show ya ngosha
one of the lately best interview, big up both of y'áll
Mkal wa rap tz
Eb mm namkubali sana huyu mzee. Lkn sijui kwanini waafrika walio wengi wakishakua maarufu wanatafuta wanawake au kama ni wanawake wanatafuta wanaume weupe. Japo huyu mzee ameeleza sababu zake. Ila wenzetu weupe inakua ktk 10 basi mmoja ndio atakua kimapenzi na mtu mweusi tena labda awe star🤷🏿♂️
Farid kibandan (ELIMU PURE YA KUWA MZAZI BORA)
Salama umeolewa coz l Love U
Best interview salama big up Faridi kubanda
Good
Makin
Fid katisha sana 😂😂😂👌👌👌👌👍👍👍👍👍👍👍👍👍👍👍👍👍
Master mind
Perfect Conclusion
moja safi sana
Heshima kwako Dada Salama Jabir & Fid Q Ngoshaaa mwanzo mwixho nimeipenda Sana hii interview kinomanoma big up kinomanoma tangu Vina Mwanzo Kati na Mwisho mpaka KitaaOlojia heshima kama zoteeee
I love salama jabir💕
Salama na Mwana FA... Naisubir hii
Heee kanywa zoteee??
nice
Fid q mwn hisabati
Fid q anajib vizur sana
Entertaining plus Educating
Its The best 🔥🔥🔥
Sasa tuletee na mwana fa yaaani daah mtatisha sana
Yahstone nmependa
Namwelewa sana sana FIDQ
One love
Madam unajua sana Mungu akujalie tu
Hip hop has spoken
Duh nashkuru sana fid q mafanikio sio magorofa na magari
Bless up Sana salama
Majani aise niwe aingie
Mashaallah utulivu na interview nzurii Sana salama jabir wwe mkongwe na hii kazi big up
Two geniuses 👌🏿👌🏿
You guys are amazing
Mbn hii interview fupi asee
😂😂😂kujifunza na kuburudika Mungu azid kuwasimamia
Mambo zuchu
WoooW Hii ni Moja Kati ya "INTERVIEW" Kaliii Kabisa Kuwai Kuiona 🧠💯. #SalamaNaFidQ
📌 Maswali Magumu na Mzuri & Majibu Mepesi na Mazuri + MADINI, nime'ENJOY Sana Kuiangalia Hii "CONVO"👑✨ #SalamaNa MOJA KATI YA KIPINDI KIKUBWA KABISA KUWAI KUTOKEA TZ 📌 🎥🎞️🎬📽️🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥
📽️🎬🎞️🎥🔥🔥🔥🔥🔥
Kama nakuona Sine Club miaka ya 2004 vile. Uligayanda ga nguzu nkoi.
dah kipindi kizuri
Fareed nakuelewa sana.
Shukran my dear brother, kila la khery ndugu zetu 🙏
Super interview
Wadau, labda mimi nafikir tofauti , ivi hichi kipindi ni chakutoa siri zako au? Nauliza tu maana mtu anajieleza yote nazani hiii si pow
True like me napenda sana creole na french zouk halafu sielewi
*FARID UMETISHA* Good job Salama respect 😘
ongeza bando inaendelea😂😂
Nimemuelewa sana huyu jamaa
😂😂😂😂😂😂 Leo mmekutana wana appetite
13:24
😍😍😍😍😘😘😘 Salama sikuwezi, huwa nakupenda sana. Your interview are awesome
Sauti iko chini sana, ... NO comments
Sorry madame Salama nakutafuta nikupe madini usikilize unipe madini niyafanyie kazi excuse madame
"Kama kilichokutambulisha kwenye jamii ni kiki, endelea kutengeneza kiki nying...." mwisho wa kunukuu
Bando lipo lakutosha haina haja ya kuongeza
" Bill Naz or Zizi?Zizi anytime " a good one
Salama tupe utaratibu tuna msika vp kaka mkubwa!!
Musukuma utampindisha hivi na vile ila hawezi kusahau chakula
Just tease on you ngosha
Salama Fanya kumdondosha mwana falsafa apo yahstone twn
mbn hazifungk
Kubanda