Utacheka Utani Wa AY Kwa Fid Q "Fid q Ni Shabiki Yangu, Siku Hizi Ana-smile" | Salama Na AY PART 2
Вставка
- Опубліковано 7 жов 2024
- #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
THE ARCHITECT
Sasa ule usemi wa ukitaka kujua tabia za mtu waangalie Rafiki zake pengine unaweza kuanzia hapa kwa mtu ambaye atakua anataka kunifahamu mimi vizuri, maana hakuna mtu ambaye hajui ukaribu uliopo kati yangu na Ambwene Yessayah, kabla hatujakua na vitambi na kutambulika kwa majina yetu mawili sisi tayari ni marafiki, na pengine sasa tumeshakua ndugu.
Yeye kazaliwa Mtwara huko nami nimezaliwa Unguja, wazazi wake ni kama wazazi walonilea mimi, mara nyingi kulikua na transfer za kazi kwao kwahiyo kuhama kutoka mkoa mmoja na kwenda mwengine kila baada ya miaka kadhaa ilikua jambo la kawaida tu, ingawa lilikua linakera haswa kwa kina Kaka na Dada zetu ambao tayari wao walishakua wakubwa kiasi na washajichagulia marafiki zao, ilikua tafrani tena kuanza kutafuta marafiki wapya na kuhamia shule mpya na mazingira mapya kabisa. Ila hili ndo pengine limemfanya Rafiki yangu Ambwene Allen Yessayah awe mbunifu na muerevu katika maisha yake na kazi zake ambazo amekua akizofanya kwa umahiri kwa zaidi ya miaka 18 sasa.
Miaka ya karibuni AY atatimiza miaka 40 toka amekuja hapa duniani na kwa bahati mbaya wazazi ambao wamemleta duniani walishatangulia mbele ya Haki na Mwenyezi Mungu Awarehemu, ila AY anakumbuka mahusiano yake na Mzee wake, wakati anakua, ukaribu wao, kazi ambazo alikua anazifanya na pia alikua Baba wa aina gani. Mahusiano yake na Kaka yake na Dada zake wawili (Dada mmoja mkubwa na mwengine mdogo wake wa mwisho) ni ya karibu sana. Yeye alichukua jukumu la kuwa ‘Baba’ mara baada ya kuanza kutengeneza pesa kwenye fani yake na mpaka Marehemu Mama yake anatangulia mbele ya haki alikua anakaa kwenye nyumba ambayo Ambwene alikua anaiangalia.
So nini kilimfanya achague muziki? Mama yake alikua radhi na hili? Kuhusu shule je ambayo alikua yuko vizuri nayo tu? Aliachana nayo vipi? Mahusiano yake na East Coast Team? Mwana FA? Muziki na pesa? Yeye kuwa wa kwanza kurekodi na kufanya shows nje ya Tanzania? Vipi kuhusu industry hii na maendeleo yake? Je tuko sehemu salama? Sehemu nzuri? Future yeye hasa anaionaje?
Kuna mengi yalifaa kuongelewa humu ila kuna na mengine ambayo wakati wake wa kuyazungumza haukua muafaka, lakini suala la yeye kuwa Baba kwa mara ya kwanza hatukuweza kuliacha liende bila ya sisi kutoa hongera zetu. Aviel ndo jina la kijana wake wa kwanza, experience ya kupata mtoto kwa mara ya kwanza nayo hatukuiacha kuizungumzia.
Yangu matumaini kama ilivyo ada, utayaelewa maongezi yetu haya na kutakua na mawili matatu ya kujifunza ndani yake.
Nakutakia uangaliaji/usikilizaje mwema.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahs...
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
Audiomack Link bit.ly/YahSton...
UA-cam Link bit.ly/UA-camS...
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz - Розваги
😍 the guy is funny!!♥️❣️ na they got chemistry✌️🥰
Can't wait salama na mbwana samata
AY is a humble guy,nampenda kwa kweli
I love this gent😍 he is soo genius
lit sana 🔥 ilifikia sehemu AY akawa ana muinterview Salama 🙌
appreciate u salama n AY!!!
Kazi nzur sana nasubili ya Mchonvu na P. Hilary
Hii interview naona imekatwa sana nahisi humo ndani kulikuwa utani mwingi 😂🫡
Yah!
chemistry between this guys is AMAZING
Ila aka kanyimbo ka Salama na kanainspire sana...🥳🥳💚
#SalamaNaAY I'ts a Big Big "CONVERSATION" S/O Kwao ni "MADINI" TU.📌💯🎥🎞️🎬📽️🔥🔥🔥🔥🔥
Nilitamani kipindi kisiishe, good job salama.
One of the best chemistry. Asante sana
sound haija kaa sawa, sound engineer fanyia kazi next time.
Kumbe tulifika kuwa sehemu moja na watu wakubwa sana
Salama your one the brilliant lady in Tanzania...I really love this show ...God bless you guys
Nampenda sana AY Sana nikimaanisha kbs
Forever young East Africa's Jay-z
Salama nakuomba umtafute diamond umuhoji tunamambo mengi ya kujua kutoka kwake
#SALAMANA_NIKIWAPILI 🙏
Kitu nilikuwa sifahamu ni kuwa Ay alizaliwa Hospitali ya Ligula Mtwara na kwa bahati nzuri ndo Hospitali niliyokuwa nafanyia Mazoezi Kipindi niko chuo na Hongereni kwa Mahojiano mazuri
salama why unamis basic questions ect vipi wale members wako wapi,like ay aliweza vipi kuconnet dots na wakenya n ug,how comes now amefanikiwa kizaidi kuliko other artists tulitegemea kukuta haya majib
Interview kali salama, mi ni shabiki yako na binafsi nimekua nikijifunza mengi kutoka kwenye hiki kipindi, Naoomba upate muda umtafute mbunge mheshimiwa KIBAJAJI watu wata enjoy na kujifunza pia.
Mmmmmmhhhh binafsi sitakuwa na cha kujifunza kutoka kwa Kibajaji
jamaa ana inspirational story alianzia kua house boy mpaka hapo unavyomuona leo. kujifunza kuko kwa angle nyingi kaka, kama akiletwa ukipata nafasu jaribu tu kusikiliza.
Hii video imekatwa sana, unajua kwanini? Washkaji wanahojiana😂😂
sister salam naomba mulete Mr blue
Sema mmepiga story sana
Nakukubali sana mkaka
hapa kwenye wazungu wanaojua kiswahili, aisee umenichekesha sana ni kweli hawa jamaaa wanaboa mnooo.
kila kitu wanazinguaga tu sijaonaga afadhali.
Zeee
Salama yuko na boss wake
Salaam na novatus
Hipapu iko up bro nai peda
Zeeee
inaeza ikawa hii ndio last ep2 mana nakumbuka ya mkasi ile ep ya mwisho ilikuwa na AY
Duh! Hapana kwa kweli...😥
Kwan salama mbn kacheka sana kuskia fid Q katoa wimbo wa tarabu na Isha mashauzi mana nimehamasika kucheka sana bila ya kujua nacheka nn. Maana narudishia kila saa nicheke tena na tena
AY kaanza kumuhoji Salama... 🤣🤣🤣
Jamaa amemuua fid q 🤣🤣
Hii ni miongoni mwa interview mbaya zaid yenye mafunzo machache mno aliyowahi kufanya salama.
Salama tuletee watu wa kutufunza na kutukuza kiakili kama ulivofanya kwa idriss na Majei
Acha roho mbaya wewe
EFFORTLESS
promosm