WAKILI MADELEKA AMVAA MAKONDA HANA MAMLAKA YEYOTE KIKATIBA KUAGIZA VIONGOZI WA SERIKALI AOMBE RADHI
Вставка
- Опубліковано 1 лис 2023
- Endelea kufuatilia taarifa mbalimbali za kina na zenye ukweli na kuaminika
Tufuatilie kupitia mitandao yangu kila siku kama ifuatavyo:-
Facebook: / kusagamedia
Instagram: / kusaganews
UA-cam : www.youtube.com/@kusagatv6320...
Tiktok. www.tiktok.com/@kusaganews?la...
Uko vizuri sana wakili mspmi, elimisha waTz wamedangamywa sana mpaka wamekuwa mbumbumbu.😮
Kikubwa tunahitaji maendeleo umeme unazimazima2 porojo 2 Makonda piga kazi watie muhasho hao
Apige Kaz wapi tatizo ni huyo mskonds na chama Chao?
Mimi ningelikuwa mkuu wa mkoa wa Dodoma aliyeagizwa kukimbia, hakika palepale ningesimama jukwaani na kuagiza polisi wamkamate Makonda na kuwekwa maabusu masaa 48 kwa kuidalilisha serikali ( dolla). Ni aibu tupu.!!!!
Mnapo ongerea chama Cha mapinduzi.chama kina Ilani yake ambapo Viongozi wa chama wanatakiwa kusimamia,serikari kutekekeza Ilani hiyo.
Kuingilia kazi za wataalam
Nimekwelewa sana kaka
Hoja Haipigwi Rungu
Hoja Ijibiwe Kwa Hoja Siyo Viroja Wala Kebehi.
Bro. Madeleka Unatema Madini.
Maendeleo ni Pamoja na Wananchi Kujitambua Kwa Kutofautisha kati ya Pumba na Mchele.
Ma-chawa Wamegeuzwa Ma-zuzu hawawezi kukuelewa zaidi ya Kukubaliana na Kila Kinachosemwa hata ikiwa kinapingana na Katiba.
Wewe na Mwabukusi Mnatupatia Elimu ya Uraia Kwa Sehemu kubwa.
Hongera msomi kwakutupa elimu japo wanzania tuvichwa vigum
Profesionalism ikitawaliwa na hisia za kisiasa ndipo mtu anaweza kujenga hoja dhaifu
Waelimishe,, wewe mwanasheria msomi sana ,, huyu mwandishi Nate haelewi akasome katiba mana Naye ni miongoni ya wasiojua katiba😂
Asante Mh Wakili kwa elimu
Mbona tunasikiaga viongozi wa vyama vya upinzani vikitoa maagizo kwa serikali? Kwanini hapa Chama kishindwe kujisimamia au kujisahihisha chenyewe?
Havitowi maagizo vinatoa mapendekezo tu na ni hiari ya serikali kuyatekeleza au kuyakataa na VYAMA haviwezi kufanya lolote
Kama ni ya kweli hayo ebu kafungue kesi mahakamani
Asante kwaelimu nzuri.hata Polepole alikuwa anamuamrisha IGP Siro.
Uyu vipi chama kinanadi kuwa kama kitapata ridhaa ya kuongoza sisi kama chama tutafanya hayahaya ndo inaitwa ilani
Hata mimi nimeshangaa makonda kutoa maagizo kwa viongonzi wa serikali nilicheka sana jana duh ulimbukeni wa uongonzi bana ni mbaya mno
Nadhani anajiona ni Rais wa Nchi tayari !!
Makonda hanamamlaka yakutoamaagizo yoyote ilakwenyechama haposawa
Naliona giza katika nchi yetu ukweli utaongea daima RIP Magufuli
Ulichoharibu ni kumtaja Magufuli lkn ukweli ni kwamba kuna giza nene linaiingia Tanzania.
Huyu wakili hajitambui mpinga selikari, chama kina ilani ya uchaguzi ndio mana chama lazima kisimamie Kile walicho ahidi wakati wa kampeni, je Muheshimiwa Mboe akitawala hatafuata Irani ya Chadema?
Makonda nikama mama lazima ajifanye kama rais hakuna utaratibu guy’s.
Kuna wakati sio kila jambo linapotokea unatakiwa kulitolea maelezo.unapoteza umaarufu.nifafanulie nini maana ya chama tawala.kipi kikojuu kati ya chama au serikali.
Kumbe haujui kama chama ni Cha wachache naserekal ni ya wote pole sana
Muda Mwingine Izo Shelia Zinaludisha Nyuma Maendeleo Kama Ni Ivo Mbona Wakati Tunasikia Mafisadi Amjayumia Vizuli Shelia Zenu Kuwakamata Ayo Mafisadi Shelia Za Tanzania Ukizifata Unaweza Hata Usiwape Maendeleo Wananchi Wake Makonda Yuko Kazini Kuokoa Waliozulumiwa Kama Mko Na Shelia Kwanini Msiende Jela Kuwauliza Wafungwa Kujua Makosa Yao Mzitumie Kuwatoa
Wewe Madeleka fanya kazi zako mambo ya makonda achana nayo, wanaofata katiba na sheria mbona ndio wamekuwa kipaombele kuihujumu nchi ikiwemo kuuza rasilimali za nchi, kulinda mafisadi, matamshi ya makonda hayana tatizo kwani anaowapa maelekezo ndio waliomweka pale hana chakufanya .
Serikakali inaongoza na chama,ila chama hakiongozwi na serikali twelewe,kwahiyo makonda yupo sahihi kwasababu serikali ikishindwa nichama kimeshindwa
Waxenge mnatolewa kwenye leli mpate cha kufanya mmejadili bandari mda mrefu na ilani imetimia sasa msikae kimya chuma icho kazi kwenu msojielewa mnahisi CCM ni ngoma ya kiti moto wanawamba ngozi ya Ng'ombe
Kidumu cha chamapinduzi Makonda chapa kazi tu. Mwanachama wa CCM mpe maerekezo tu
Mamlaka amepata kupitia cha cha mapinduzi au ccm Ndio anakiwakilisha na viongoz ano waamrisha ni wachama cha Mapinduzi
Hii ni sawa na mkuu wa wilaya akiwa muumini wa kanisa au dhehebu fulani au kiongozi mkubwa yoyote anapokwenda katika ibada za mila
Kwa hiyo mwanasheria achoongea ni sawa kwa mktadha wa katiba lakini katika uhalisia hicho kitu hakuna kwanini kwasababu mkuu wa wilaya na cheo chake akiwa muumin wa kanisa akiingia kanisani anafata maelekezo ya kanisa ili aweze kwendana na imani hata kazi ataifanya kulingana na maelekezo ya imani yake
Kwani mkuu wa mkoa anatokana na chama ndugu😂 au na wewe haujaelewa,
@@asiliyetuonlinetv5063 ili uteuliwe kuwa mkuu wa mkoa lazima wajilizishe kwamba uko pamoja nao vinginevyo hupati hiki cheo nduguyangu
Nimepata elimu ndugu mwanasheria kweli baadhi ya viongozi wa CCM hawajitambui
Kwani katiba huletwa na nani katika taifa.. hata asiwe na mamlaka anafanya ya muhimu
Kanisani kusipokuwa na biblia sizani kama waumini mtasali, sheria na katiba ndo zinatuweka mjini, lasivyo watu tunaweza kuuwawa kisara bila sheria
Unabugi kwa sababu viongozi waserikali wote wapo pia kwenye chama,,hao wakuu wa mikoa ni wajumbe wa ccm,,isitoshe serikali inasimamia Sera za ccm
Mbona ninyiwagumu kuelewa? CCM.ndo mama wa serkali Makonda yuko sahihi pigakazi Makonda
mwandishi wa habari uwezo wake ni mdogo sana
Kaka Madereka Umeferi maana Umeshindwa Badari Umerudi huku Makonda Umuwezi fanya kazi zako kaka. Tafuta kesi
Madelaka anafafanua aibu iliopo tanzania ujinga mwingi. Lini chama kikaingilia shughuli za selikali. Aya wazili mkuu angekuwa ni chama cha upinzani angefanyeje angetoa hayo maagizo. Tanzania kikubwa kuishi tu.
Bongo hamna Katiba na sheria za bongo siku zote zinawahusu watu hohehahe
We mwanasheria acha kupotosha watu mtandaoni Makonda yuko Sawa Serikali imeumdwa na Chama Tawala na Makonda ni kiongozi wa juu wa Chama sasa unayegemea Nini hivi uanasheria wako ulisomea wapi
Ccm ndio serekali au?
Viongozi wa Serikali waoga kwa chama. Uoga huo ndio unaodhoofisha utendaji wa serikali. Hawaconcentrate kuitendea haki katiba kwa kutimiza wajibu wao.
Hiyo tunaita ni kutaka kujikombakomba waonekane niwatiifu ili waendelee kutetea matumbo yao
Kwa hiyo Samia pia haelewi katiba? Ndiyo maana kamuweka muenezi mbumbumbu? Kwa nini hamtoi makonda anabwatuka tu mambo yasiyoeleweka.
Selina tambukwa wauguzi
Mimi sio mwanasheria na nikitumia akili tu ni kwamba, kwenye uchaguzi vinashindanishwa vyama na viingozi wa serikali wamepata nafasi zao kwa kupitia chama chao hivyo ni lazima viongozi wa chama hicho wawe na nguvu kwa wanachama wao walooko ktk serekali kuweza kuwawajibisha wanachama wao kufuata ilani ya chama chao kwa munibu wa katiba
Sahihi
Makonda atakipangachama
Achamawakili
Walalahoi hawana hoja
Mmm hata mimi naona kunakitu hakijakaa sawa kiongozi upo sawa
Wewe mwandishi wahovyo Sana, unatakiwa kuwahoji viongozi wa hovyo Kama wewe ulivyokuwa hovyo,
Great minds,
Mh.Madeleka anajizima data kujitengenezea mjadala you tube wakati anajua ukweli na anajua anacho taka yeye.Ukweli wakati wa uchaguzi kitakacho kuja kupimwa kama kinatosha kuongoza Nchi si Waziri mkuu wala Rais Bali ni Chama Hajui kitu gani huyu afutiwe cheti cha uwakili,na elimu ya katiba aanze yeye kupewa,hajaelimika anajua anacho soma tu .
Hapo siyo makonda Bali ni chama chake;:
Makonda Kwa CHEO cha uenezi taifa ana mamlaka YA kutoa maelekezo,Yaan mamlaka
Makonda aisome katiba ya jamuhuri,, na y chama Ili atofautushe chama na serikali
makonda hajui mipaka yake . ndo maana baba lao alimuondoa. analopoka tu
Makonda hakuondolewa na yeyote kazini ila aliacha yeye
Madeleka hana haki yeyote kukisemea chama cha ccm na ilani yake ! Hichi sio chama cha kikanda na sio Sacco's ya wachaga , kama chadema ,akae kushoto ! Makonda piiiiga kazi
Madeleka anafanya vizuri kama umeenda shule utae!ewa
Chini ya katiba ya ccm wakichukuwa kadi ya ccm majaliwa hana uwaziri mkuu ndio wanafata maagizo ya chama makonda ajavunja katiba angekuwa waziri ni tlp akampa maagizo hayo hapo sawa ameagiza wana ccm wenzake
Ahsante
Makonda kama anaweza kumwajibisha waziri mkuu. Tuone sasa nguvu hiyohiyo ayipereke kwa kwa vyombo vya ulinzi na usslama kuwajibisha
. Akifanya hivo mimi nitsomba uraia kenya. Makonda anafanya b hivo kwa viongozi wanawo omba kazi kujaza fomu za ccm. Wamjadiri. Apitishwe. Awe mubunge apate uwsziri lakini vyombo vya ilnzi na usalama hakuna anaye omba kazi kujaza fomu za ccm.
Hakumteua waziri Mkuu
Makonda anaweza kumuondoa mtu kupitia kwa raisi wanchi, kwasababu katumwa na yeye hivyo usipo mtuu makonda utakuwa hujamtii raisi, nguvu anaitoa kwa raisi, au mwenyekiti wa chama, ambae pia niraisi wanchi
Huo ni uongo wa mchana acheni Makonda apige kaz
Boundaries has to be established
Makonda wakimbize wakimbize maana hawajitambui
Acheni roho za fihi watanzania,yy sio mwehu kufanya ivo wao walishakaa nakumpa maelekezo ya utekelezaji wa ilani ya chama bila kuchagua ni kiongozi yupi na ndo kazi yake mwenezi.hujiulizi kwann wanakubali nahawakaidi maelekezo???
MH MAKONDA PONGEZI NYINGI KWAKO TUPO NA WEWE DAIMA KAZI IENDELEE DAIMA MBELE KWA MBELE MPAKA KIELEWEKE.
Kasome na we kuliko kuwakashifu wanasheria HIV unaluma gang au umehitim kwakupewa kad ya CCM?
Niseme tu kua makonda awe amekosea ama hajakosea aendelee tu nchi imepooza sana hakuna maajabu katka hili achawakimbizwe mchaka mchaka wamelala sana
Maua yako mwanasheria. Tumeanza kujifunza katiba yetu
Serikali tuishauli katiba iwe inafundishWa shule kama masomo mengine
Nchi hii inaongozwa na mbumbumbu wa KATIBA, hii ni shida kubwa sana!!! Wanaotutaka tupewe elimu ya KATIBA KUMBE WAO ndiyo wanatakiwa wapewe elimu HIYO!!! NI AIBU KWELI KWELI!!!
Serikali inasimamiwa na chama ili kukamilisha ilani ya chama,
Asnte kutunyamazisha wastaafu mungu mkubwa
Makonda kwakua anahaki ya kuomba kura au ridhaa yakumuombea au kukiombea chamachake nafasi ya uongozi wa dola. Yaani udiwan,ubunge na urais.basi kwakua chama chake kilipewa ridhaa yakuongoza nchi.basi chama kitaunda serikali itaokua chini ya chama.hapo ilichama kitimize yale kilicho ahidi lazima kilesahani moja na serikali.kwakua serikali siolazima mlengo wa chamachako.
Madereka huwezi kuwa na wasaidizi wako afu usiluhusiwe kusimamia mali anazosimamia msaidzi wako.
Huo Ni mtazamo wako binafsi lkn sio kisheria, kisheria makonda hana nguvu hiyo
Haya mambo muwe mnasoma usifafanue kwa hisia. Kwenye nchi ya Kidikteta serikali ni chama na chama ni serikali.
Haya mpaka hapo tuu wewe niambie Makonda yuko sahihi au hayuko sahihi kikatiba. Makonda hana uhalali wa kuielekeza serikali.
Inamaana hiyo nafasi imeanzishwa leo niambie Katibu gani wa Uenezi ulishaona anafanya kama Makonda.
Makonda hayuko sahihi Katiba haimruhusu hiyo iko wazi
@@shafee9128Uko sahihi 100%
Watanzania jamani jamani tusomekatiba alafu tuwe tunaangalia mtu anapo toa hoja kamazakweli alichokiongea madeleka nikweli kabisa ccm wezi wa katiba wanaiihujumu 2025.waondoke
Mheshimiwa Peter Madeleka sisi kama wanainchi tunakuona kama unapotosha Uma kwa sababu hata Raisi wetu amewaagiza Viongozi wa CCM kuisimamia serekari jee wewe unaanzaje kusema kua Viongozi wetu wa Chama wasiwe na nafasi ya kuielekeza serekali na wakati serekali imetokana na chama hicho isitoshe Raisi wetu ambae ndiye Mwenyekiti wa Chama pia ameelekeza hivyo na Mimi ninaamini kua kauli ya Raisi ni sheria kwa maana hiyo unawashauri mawaziri na viongozi wa serekali yetu wamdharau Raisi wetu ninakushauri unapotakakuongea jambo fikiri kwanza Faida yake na madhara yake hivi wewe ndugu yetu ukoje na akili yako iko wapi pamoja na elimu yako yote kwanini umshutumu Makonda kauli yake njema ya kuwaonya viongozi wa serekali yetu maana ninaamini kua mtu anaelipenda Taifa Lake na viongozi wake na watu wake atawaonya ili msiharibikiwe adui hawezi kukuonya kwa sababu anatamaani kuona mnaharibikiwa ndiyo maana hata ukichunguza utaona kua Upendo wa Mungu kwa wanadamu ndiyo uliomfanya Mungu wetu kuwaleta mitume na manabii ili wawaonye watu wake nduguyangu huo ni upofu una macho lakini hayaioni nia njema ya Mheshimiwa Raisi namwenyekiti wa CCM kuwaelekeza viongozi wa CCM kuisimamia nakuielekeza na kuikumbusha kutekeleza ilani ya CCM na pia huuoni upendo wa Mkonda aliyonao kwa Taifa letu ninamalizia kukwambia maneno yafuatayo ukiona uko na mtu ambae hakuonyi wala kukuelekeza na kukushauri huyo ni adui wako mkuu mwenye mapenzi mema na wewe atakuonya atakushauri na kukuelekeza na kukukemea pale anapoona unapotoka hivyo muondowe Makonda mudomoni mwako kwa sababu maneno yake yanadhihirisha anavyolipenda taifa Lake na jinsi anavyomtii Kiongozi wake aliemteua ninawaomba Waheshimiwa Mawaziri na viongozi wote wa serekali yetu watambue kua Makonda ni anawapenda ndiyo maana anawaonya na kuwaelekeza na ikibidi kuwakemea kwa sababu hapendi kuona mnaharibikiwa na huo ndiyo upendo wa kweli hivyo naomba nanyi mpendeni na mpeni ushirikiano ili tupate kupona ninaomba usome Biblia kitabu cha: 2Samweli 19:1-10. na ikiwezekana soma hiyo sura yote utaona jinsi rafiki mwema alivyomuonya na kumshauri na kumkemea Mfalme Daudi utaona kwa hakika kua mtu kama huyu alikua na mapenzi mema kwa mfalme Daudi ndiyo maana aliona vyema kumuonya.NB. mtu asiekupenda hawezi kukuonya kwa sababu hapendi kuona unafanikiwa bali yeye anapenda uharibikiwe pia ninaomba uelewe kua ninakupenda ndiyo maana nimekuonya uachane na jambo hilo kwa sababu halina afia kwa Taifa letu na ujumbe huu pia ni kwa wote wanaomshutumu Makonda katika jambo hili mtieni moyo ili afanye kaziyake na siyo kumvunja moyo kwa kumshutumu shut Uma hizo hazina afia kwa Taifa letu na kwa maslahi ya watanzania wote Ninaomba Mungu awasaidie mpapate kuona kwa macho ya ndani. Asante na Mungu awabariki. Amina.
WEWE PIGA KELELE WEEEE....
SISI TUNAJENGA NCHI KISHA TUTAKUHOJI TENA WAKILI UCHWARA
Serikari inasimamiwa na CCM hivyo HAKUNA ubaya CCM ikitoa maagizo kwa Watendaji wa Serikari.
Serikali inasimamiwa na bunge sio ccm
Anachokifanya makonda kwa sasa ni zao la vitu vitatu,navyo ni; 1.Bangi. 2.Madaraka. 3.Kipato. Sasa kwa makonda huenda vyote vinamsumbua.Ukivuta bangi itakutuma useme au utende lolote bila aibu.madaraka na pesa navyo hivyo hiyo.
Na 4. Ulimbukeni
Huyu wakili hajitambui! Hivi Muheshimiwa Tundulisu akitawala nchi Chadema hawatashauri selikari yao?
Yan ww ndio hujielewi
Wanasheria acheni kushangaa ,badala yake, mpelekeni Makonda mahakamani, ashike adabu
Hao mawazori wanachaguliwa na chama . Munahaza kumuchonganisha . Makonda anafanya vya chama chake na sio vya katika. Wabunge wote ni wachama . Makonda hajawajibisha mtu bali anawahambia mawaziri wa chama chao. Chukibinasfi.
Unawapotosha watanzania so tunataka maendeleo katiba ya chama inaeleza hivyo ccm Oyeee
Sasa kaka wakili unawezaje kutimiza ulichoahid kwa wananchi bila kusimamia. Makonda yupo sahihi ila ww ndo bdo hujaelewa.
Sasa rais na waziri mkuu ana kazi gani?
Tunataka katiba mpya sasa
Kila chama kinakatiba yake je unalijua hilo?
Ukiwasikiliza wasomi unapotea wanatumiwa nawazungu kutukologa
Acha kupotosha watu sisi wa Tz sio wajinga. Wabunge na wawakilishi ndio huchaguliwa na Raisi kuwa mawaziri iweje m'bunge wa chama asiwajibishwe na kiongizi wa chama wakati bila ya chama asigekuwa waziri?...
Asante kaka nilikua sielewi
Hii hipo kwenye katiba ya chama
Ndugu mwandishi kichwa chako kizito mnoo
Mimi ninaomba ututajie kipengele kinachomkataza kufanya hivyo pia utufafanulie kusudi na kazi ya ilani ya Chama katika kuomba uongozi.
Wabunge wote ni CCM
Peter Madeleka nakukubali sana. Ila kwa hili niko against na wewe. Viongozi na watendaji wa serikali kwa asilimia kubwa wanatokana na CCM na wanatekeleza ilani ya CCM. Hivyo mwenezi Makonda ana nafasi kubwa kuitisha uwajibikaji wao ili chama kizidi kukubalika kwa wananchi ndipo na wao watabaki kwenye hizo nafasi maana kama chama hakipo na aliyewateua hayupo.
Vinginevyo hoja ya katiba mpya yaweza kuifanya hoja yako wakili Madeleka iwe na maana. Kwa sasa tumwache jemedari Makonda na sekretarieti wapambanie chama.
Ni maoni yangu tafadhali.
Sio kutoa maelekezo kama anayoyatoa wenezi wengi wamepita walifanya kazi yao
brother hebu usituchanganye,makonda yupo sawa tu kwan kuwakumbusha viongozi kutimiza kaz zao ni vby
Nyiye tulishawazoweya tunataka kazi sisikatiba yanini makoda chapakazi
Kwa katiba ipi?
Usiku umeendelea Sana asubuhi imekaribia sana
Makonda ni mvunjaji wa Amani ya Nchi yetu
Nikweli hayo tutete mtu ambae amsha asha mandeleo,na kuwatetea masikini ambao Awana pakisikilizwa
Huyu mwandishi naye ni chenga
Nahisi kuna la siri juu ya waziri mkuu.Mara naibu wazir mkuu,mara magizo ya Makonda kwa waziri mkuu.Hadhi ya waziri mkuu imeshukaa bora na ambapo alikuwa afisa elimu.
Sikia muuliza Maswali hata wafuasi wa ccm kuvaa sare za chama kwenye ziara za rais za kiserikali mnajua kwamba sio sawa ila watu hawajui hilo wanavhukulia poa tuu.
Serikali ni Taasisi sio kitengo cha Chama cha Siasa 😂😂😂. Akiwa pale rais ni mwajiliwa wa Nchi sio chama na ndio maana halipwi na chama ila analipwa na Taasisi inayoitwa serikali. Shida hii Nchi ni welevu wanatake advantage ya wajinga kuwaburuza
Ila raisi samia alisema kuwa katiba ni makaratasi hivyo hawaeshimu katiba
Madeleka wakati mwingine tukifanya makosa lazima tutumie vizuri uwezo wetu wa kufikiri. Chama hakiwezi kutenganishwa na Serikali kwa mfumo tulionao ambao hauna mgombea huru. Huyu anayetoa maagizo hajakosea, Chama ndiyo mwajiri wa Viongozi wote wa kuteuliwa kwenye nafasi zote za kisiasa. Eleza ukweli, common sense uitumie na angalia miundo
uongo dhambi madeleka uwa unajua mambo mengi na unajua kutoa elimu juu ya Sheria sema basi tu uwezi pata nafas
WANATOKANA NA CHAMA NA HIVYO WWANAWAKILISHA CHAMA CHAO...
KUME UNAJUA CHAMA KINANGUVU SASA UNASEMAJE KUHUSU ILANI YA CHAMA?
ACHA MASIFA HAUJU CHOHOTE MADELEKA
Huyu Mwanasheria yuko sahihi 100% Makonda hayuko sahihi kabisa Kwenye serikali ya chama Kimoja au Nchi inayoendeshwa Kidikteta ndio Makonda angekuwa sahihi ila kwa Tz mimi mwenyewe nilikuwa nashangaa sana Makonda anapiga biti mkuu wa mkoa waziri mkuu dooh 😂😂😂😂
Dah,,Atamimi nilishangaa sana Mkuu wamkoa anakimbizwa na kiongozi wachama AIBU yaani Haijui ata nafasiyake
Mkuu wa mkoa anaganga njaa zake asifukuzwe kazi
Watu ambao bado wanaishi kwa yale yalioandikwa siwatofautishi na mwanafunzi ambae bado yupo shule akitafuta elimu na bado hajaelimika. Kwa wanasheria kama hawa sioni kama baadhi ya wasomi wanaweza kuisaidia Nchi kuleta maendeleo katika Taifa.
Mimi nimegundua kumbe makonda anaishi miaka ya 1977- 1992,
Ningekua uyu mwanasheria ningempiga uyu mwandishi Kofi la kichwani Kwa mujibu wa sheria ya ibara ya 16a
Piga Kofi jamani.
Katiba mpya ni sasa
Sana!
I wonder where is Bashiru....
Welldone Wakili Madeleka.👏👏
Viongozi wa selekari wanapo fanya vibaya chama ndo kinalaumiwa kua kinatuwekea viongozi waxembe inakuwrje Leo useme chama hakidtaili kuwasimamia viongozi wa serekari?
Ndugu kuwa na uelewa kikatiba hiyo sio sawa kama Kuna shida wao wanatakiwa Waitane waambizane wenyewe Sasa ikiwa ivo basi tusifate katiba ambayo ndo sheria mama yaan tujifanyie tu mambo nje ya katiba mfano wananchi wasilipe kodi wasifanye yote yaliyopo kwenye katiba uone kitakachotokea na kwa nn waliweka katiba? Hakukuwa na maana kama ndo ivo
Makonda anawadaa wanananchi kuwa ccm ina nguvu hii ni geresha toto ya ya serkali na ccm yao iliyopoteza mwelekeo ccm haifai kuendelea kuiongoza nchi imeharibu kila kitu
Ckiliza Milad Ayo Waziri Mkuu kajibu nn???? Wacheni kupotosha watu bhana nyie
Je,makonda ni mteule wa Rais?
Sasa na hiyo Ilani ya chama unapimaje we wakili bhana....😂😂