Dizasta Vina - Wachezaji wa timu
Вставка
- Опубліковано 5 вер 2024
- Official lyric video of Wachezaji wa timu. Marks a 2nd release off the album A FATHER FIGURE
Stream/download wachezaji wa timu
Boom play - www.boomplay.c...
Spotify - open.spotify.c...
Apple Music - music.apple.co...
Mdundo - mdundo.com/son...
Audiomack - audiomack.com/...
Dizasta Vina
Instagram - / dizastavina
Twitter - / dizastavina
Facebook - / dizastavina07
Lyrics
Wanasema duniani kuzimu
Kwanini ukeshe kushika protocol wakati
Ulaji muhimu
Watu wanachohifadhi ni mbinu
Kucheza kulia kushoto ila wote ila wote
Ni wachezaji wa timu
Chumba kilijaa njemba za kisasi
Walipanga vifaa ka' wanakwenda kwenye kazi
Palikuwa jitu juu meza yenye glass
Limeshika tissue kusafisha chemba ya risasi
Walijaa na maninja na ma bouncer
Wamevimba wenye sura za kutisha
Wamekausha,
Wamegadhibika mpaka amani ilijificha
Nilihisi mkojo unatiririka kwenye trouser
Sura za kutisha nafuu devils
Crate zimemwaguka utadhani sikukuu kesho
Kulikuwa kumejaa camera full angles
Huku warembo waki-twerk twerk juu ya pool table
Huku watemi wa ngenga wameketi
Mwonekano wa Rostam Bakhresa na Mengi
Palikuwa na mabegi ya cheda na chenchi
Yalikuwa mengi hata wachache kubeba hawawezi
Walikuwepo mabinti wamefanya line up
Mfano wa dinner set Sura ziko innocent
Zikionyesha zina majuto ya kusign up
Na baadhi yao walikuwa wadogo yaani minors
Babake Jesca alisimama kwenye chanja
Ametingwa kuchanganya plama kwenye ganja
Nikamsalimia hakuijibu salamu yangu
Akavuta beri kisha akapiga chafya mara saba
Kabla muda wake wa kumaliza
Akanyonga jani akapaka mate kwenye Lizzla
Akasnap vidole kuonyesha alikuwa Taita
Kumwita Mrembo na mrembo akaja Na lighter
Mrembo akamwashia kipuri wakapiga Puff mbili
Wakatoa moshi wakaanza kukiss pasi siri
Ka’ wacheza ngono mbele ya Binti yake Jesca na mbele yangu kiasi nafsi ikakosa tafsiri
Baba'ake aka-struggle kukumbuka jina langu
nikamwambia jina langu naitwa Toni Glove
Akauliza umemjua vipi binti yangu
Nikamwambia mi na jesca tumekutana kwenye coffee shop
Akaisogelea glass, akanywa kilichomo kisha
Aka-scan majibu
Ili kuhakikisha ninachokiongea fact, akasema sikujui unatokea wapi
Nikamwambia nimezaliwa hapa Nonde Sua
Nyumba no 77 kwa mzee Kilua.Akasema ninapiga simu mbili tatu kama hawakujui
Nitakushauri tu uombe dua
Akaja mtu akani-snap kwenye IPhone
Design kama anafanya michongo ya passport
Akainua uso nikaona umeweka ndita
Akatikisa kichwa kisha akaendelea ku-type more
Mkono wa jesca begani ukinipeti peti
Huku moyo wangu ukienda lesi lesi
Board guard wake wakinichekicheki
Mara wani-search mifuko mara wani-search begi
Nikaletewa maji ili nipoze kiu
Design hamu ilinikata mzee
Wasaidizi wakingiza jina langu kwenye simu ya kimtandao
Kunifanyia background check
Babake Jesca
Akanipa face look kisha
Akaomba simu sikubisha
Akaanza kukagua photo Akalog in kwenye social kunikagua Facebook Twitter
Ghafla ukimya ukaitawala nyumba
Wakati akili ikiwaza kufa
Nikitushwa Na yale mandhari yanayofanana na nyumba ya mafia mkubwa
Kutoka Kuala Lumpur
Akauliza je nipige down town
Maana najua kila mtu kule ukinidanganya bure
Nitakukausha kama kau kau mpaka uta shout shout
Jesca akasema Daddy calm down
Mi na Tony tayari tumependana
Amekuja kutoa mahari ili tuishi ka' mke na bwana
Anaomba kibali anataka kunioa
Na kama utakubali basi soon tutafunga ndoa
Baba Jesca akaegemea kwenye kiti mwisho
Akashusha pumzi kwa masikitiko
Kwanini unadate na mtu hatumjui
Na unajua style ya kuleta hawa wakati ringi
mwiko
Jesca unajua hadhi ya hii business
Equation ya ndoa haifiti into this case
Kwanini usitafute a guy from inside
Ipo time utaleta ma-spy au ma-witness
Jesca akajibu daddy Tony Doctor
PhD holder chuo kikuu cha oxford
Anamiliki migahawa kadhaa hapa town
Analipwa vizuri na kipato kinamtosha
Namfahamu Tony sio mnoko
Na kwao wana uwezo sana baba yake don sio kitoto
Tumejuana miaka kadhaa ameshanikaa
Maana penzi nililolihifadhi moyoni sio kidogo
Babake Jesca akanicheki amenuna
Nikawa nimevex nimechuna
Moyo unaenda resi kama duma
Mabaunsa yapo next yametuna
Yakisubiri mechi hii kubuma
Nikamwona mshikaji ameshika panga bisu
Alikuwa busy anapanga vitu
Sura yake ilikuwa tayari kuanza bifu
Jesca akaniambia yule kaka'angu na ana anger issues
Akaja ameshika vipisi vya kete
Kisha akanidadisi si kibwege
akashout naskia harufu ya polisi kwa huyu bwege
Jesca akamuwahi akasema we' chizi acha usenge
Akatoa syringe kwenye small bag
Akauliza unapendaga cocaine
Nikamwambia huwa situmii hizo zaga
Kaka'angu alitumia akabwaga akajibu okay
Nilihisi harufu ya casket
Kaka'ake Jesca alihisi mi' shushushu akani-suspect
Nikahisi napokwenda sio
Moyo wangu ukienda mbio
Babake Jesca nae anahamaki
Baada ya kugundua nina camera kwenye kifungo cha shati
Akatoa bunduki nikahisi uhai wangu unaishia
Ndipo polisi wenzangu wakavamia
Dizasta is very intellectual, mindful, script writer, lyricist, musician and natural gifted man you can say he has philosophical, transgressive mindset, with unconventional perspective along with marvelous way of narration from his writing which imply the poetic mentality from very different level. To understand what he intent or the way he conveys the message in his songs you need brain man!
For real he is Genius!
As ultimatum, has very high consciousness beyond ordinary, he tries to do music in a unique story-telling style way, I have listened 90% of his songs, he did amazing work. I think his work has been very inspirational to young generation musician who fit to this type of music especially in HipHop.
When different people try to listen to his songs everyone feels they have been touched in very different way.
🎉🎉🎉🎉🎉
noma sana
Yah sometimes you need to be intelligent too and very reasonable to understand him
Simply, genius.
Definetly
Nasikia harufu ya polisi kwa huyu bwege,
Jesca akamuwai we chizi acha useng×.
🔥🔥🔥🔥🔥🔥
For those who will be here in 3010 years to come in our absences remember thiz man was our teacher shule nzima kwake❤❤❤❤❤❤❤
Arusha town wamethibitisha hili ni bonge la ngoma,likes ziko wapi
My children will have all the freedom to listen to dizasta vina's music or else leave my house
you think just like me brother
What a courage 😅
Itabidi umfundishe kufikili kwanza😂
100
Yaan mm manzi yang mara ya kwanza alikuwa ananiambia nyimbo gani hzo lkn baada ya kuanza kumckilzisha MWANAJUA, SHAHIDI, NDOA, MONEY sasahv yy ndio ananipa update kuwa RAFIKI YAKO DIZASTA KATOA WIMBO MWINGINE HUKO anazipenda hasa zile NOBODY IS SAFE tena hasa Namba 4
Alishasema yupo kwenye top two and he is not the second am here to prove ✔✔
Vina is the best
Nimechelewa kidogo nimekuwa 20😢 lakin kama unaamin dizastavina is number one rapper in Tz like here from BBC London 🏴🔥💥👊🇹🇿✈️
Enyi watu mtakaoishi mpaka mwaka 2080 na mtakaozaliwa mimi Babu yenu niliishi kwenye hii generation ya the best hiphop artist,nimeshuhudia hizi harakati, sijajua kama kizazi chenu kitapata bahati ya Kuwa na Rapper mwenye akili kiasi hiki lakini nawaaambia tu mtu uyu walikua wanam-Underate imagine..Basi mumpe heshima yake Babu yenu huyu.
🎉
Umetisha broo
Leo wa kwanza nipen like zangu from songea RUVUMA DIZASTA💥💥💥
Unstoppable master vina from BBC London 🏴🔥💥👊
Wa namba flan from Ruhuwiko
Dizasta Vina
Hahahahaa! M nilikuwa nimelala tu ila ningekuwahi kaka, sema hamna mbaya kikubwa uzima👊
Homeboii💪💯
Waungwana tusiishie kumsifia tu mwamba anauzaga album zake on line tununue kwa wingi ili jamaa aendelee kutushushi midizasta yenye VINA yake
Hatua ya kwanza naanza kuisikiliza nilikuwa nimetengeneza mawazo yangu kichwani, hatua ya pili nikabadili welekeo. Ebwana! Hatua ya tatu nikasikigina fegi na kisigino cha kiatu. Nairudia tena hii timu.
Sina nyongeza brother.
Tuzo ya utungaji Bora inamuhusu🎉🎉🎉🌍🙏
My best writer of all time😊,wanaomkubali Vina tugonge like hapa tuendelee kufurahia mziki mzuri
Best writter,best story teller with incomparable intelligence of the century 🔥🔥viva DIZASTA viva you are a mental therapist
WATOA WAPI VITU HIVI KAKA JAMBAZ,,,,,,AU DUNIA TUNAYOISHI CC SIO DUNIA UNAYOISHI WWE,,,,,,UNA MOYO MKUBWA SANA DIZASTA VINA,,,,,,HOPE KALII✊
Akili kubwa sana unajua sana kuandika imenibili kusikiliza zaid ya mara tano ili kuelewa.
Dizasta the next earth 🔥🔥wachezaji cheza kwa step mi beki 5😂 respect bob
Watu wanachohifadhi ni mbinu!!!
Man of the world 🌍 mzee wa vinaa , nipe like
We jamaa unajua sana aisee sio poa
We Mzee nyoko Sana Yani, umeshindikana, upo nje ya hii sayari, bado sijaona wakufika ulipo kaa wewe🙌🙌🙌bonge la kazi Yani ni 🔥🔥🔥🔥🔥the high voltage ⚡ Mae! Bonge la story Mzee wangu big up Sana 👊👊👊
Achia jala💥🙌🙌🙏
Naaaaam tuko pamoja na dizasta
Narudia tena na tena na tena huyo ndio rapper wangu bora wa muda wote achana na wao wapiga kelele more than story taller 🔥 🔥 🔥
wachache sana tunamuelewa msela wetu dizasta vina🔥🔥🔥🔥
Big up nilikuwa nawaza kweli tusipate hata song ya kuvuka mwaka
Bongo movie's mnafeli wapi njooni kwa mwamba awape vitu maana movie zenu hazina content za maana
Mazee hii sio ngoma ni bonge la movie
We jamaaa unajua mpka unajua Tena
HISIA ZINAZOTEMBEA.✅
Bs ndo ivo bhn nusu tumkose dizasta vina 😊😊
The story teller 🎉
We chizi acha usenge 😁🔥🔥
Dizasta vina,thanks for Good music and story teller to us like na watch movie flan mmh Rapper wangu Bora wamda woteeee ✍️🎶🎵🙏♥️🇹🇿
Hv Basata na Bakita haimuonag huyu mjamaa wamjengee sanam au kumuandalia kitab cha mhan bora wa muda wote wa mashairi na tenz.
👏👏👏👏👏 kabisaaaa Amin bob
vina apa ndo nimekuelewa uliposema upo underground umeshikilia nguzo. apa tanzania hakuna roma mwenye stamina ya kurap na wew coz wee ni god wa rapppp khaleluyaa
Dizasta hajawahi toa boko
Ngoma Kali Hadi unatamani kuskikiliza muda wote
Storytelling ✍️100%
Strong verses ✍️💯
Style rap 💪💯
Hii niyamoto aise 🎶💪👏👏👏👏
Wewe jamaa ni Canibus wa Bongo namaanisha kwa kuchora
Dizasta akitoa ngoma naona kama nimepata mshahara
Umeufunga mwaka kaka .... HAIPINGWI STORY TELLER 🔥🔥🔥🔥🔥🔥
Shule Ulikuwa King kwenye Dorm fight Ila ukapigwa na jamaa Prom Night. Hujawahi kuniangusha Prof Tungo.
The verteller @black Maradona 🔥🔥🔥
Nadhani hii ngoma inahitaji video, itabamba sanaaa 🔥🔥
Huyu mwamba inatakiwa awepo kwenye kitabu cha kiswahili (fasii) na asomwe kuanzia la kwanza mpaka chuo. Kaka dizasta unatisha
Huyu Ndio Dizasta vinna niliekuwa namsubiri kwa Muda Kidogo!✌️
Hakuna rapper kama dizasta huyu jamaa ni fundi sanaa❤❤
My no 1 rapper in tz🔥🔥🔥
Leta rapcha 200 sawa na d vina 1
Daah. Mwanangu unatisha kinoma. Mimi kuanzia leo shabiki yako
Mwalimu wangu D zasta nakukubali sana
DIZASTA VINA IS GINIUS🔥🔥🔥
Stanza kama zote 🎵🔥🔥🔥🔥🗣️ sauti ya Tanzania. ......✍️from Nairobi Kenya..
Vipi mazee, nasoma comments zetu kwa sauti ya Dizasta, nikifatiza hiyo beat, jaribu tu utapenda 😂😂😂
Daaaaaah aiseee we ni Mungu wa rap🔥🙌🙌🙌 hallelujah napenda nijifunze uwandishi wako hakuna rapper wala mc anaekufikia
Heshima Dizasta kila ngoma inatibu.
The Black Maradona 🔥🔥🔥
Dizasta Vinna wewe ni toleo la mwisho la viumbe wa aina yako, upo kwenye dunia yako mwemyewe. Huwa nasikitika sana ninaposikia wanavyokulinganisha na wasanii ambao hawafikii hata robo ya uwezo wako
Mr.Dizasta....UNANIDAI, amini!!
Mmmmhhh weweeew moto sana
Mwambaa unajuwaa tenaa sanaa 🔥🔥🔥🔥
Uandishi...💥💥💥💥💥
Namba inazidi kupanda kushuka ni mwiko 💯🔥💫
dah ila dizasta me natamani kila siku uwe unatoa ngoma sitachoka kusikilza wew ni number moja yang🎉🎉🎉🎉🎉🎉🎉
1. DIZASTA 2. DIZASTA 3. DIZASTA 🙌🙌🙌🙌🫶💯✔️
Nilipata notification yahuu wimbo juzi lkn mazingira niliyopo nikashindwa hata kushika cm......... Hili nidarasa tena.....We jamaa watu wanakuelewa sana
Dizasta your the Best All the time 🎉🎉🎉🎉🎉
We mzee akili ni nyingi sana 🙌
Lyrical atheist n nobody can go against ma perspective coz its pure fact "YES"
Professor tungo🔥🔥🔥🔥
Black maradona another one🙌🏻🙌🏻🙌🏻🙌🏻🔥🔥🔥
Anajua had anazidi sanaa sasa🔥
Jamani weekend ilikuwa mbya brother the top of the top best lyrical rapper never seen kabadilisha weekend ninaenjoy popot niendapao na MCHEZAJI WA TIMU💥💥
Hii ni zaidi ya nyimbi big brother dizasta vina..asiye kukubali ni mchawi..1000000000🇰🇪🇰🇪🇰🇪
Ngoja nikomenti ili mwaka 2070 mtu akilike inirudishe kwenye hii masterpiece... hii biti sasa acha tu
Sikutaka kukurupuka kuisikiliza nilitaka nitulie kama hivi leo ndio niingie darasani. Shule ya bure ada bando lako tu✊
Great stroyline great punchlines lyrical genius
Hanaga ngoma mbovu💪
I use to like before watching.... Dizasta is 1000000000000 miles far away from these mumble rappers.....
Familia Dizasta brother unaweza man calm down utawauwa ao vijana
😂😂jesca akamuwahi we chizi Acha Usenge😂😂 unyama sana
Nimecheka kisenge
Dizasta mashabiki tulimix nyimbo za move❤
Dah!!! Kumbe raundi hii Maradona alikua usalama/mpelelezi bana😂 sema story tunaiombea part 2 coz hatujui kua mpenzi wke Dizasta alikua anaelewa kua bwana wake n usalama kwaiyo alitaka aende akamuuze faza wake au na yy pia hakua akijua😂
Sijawahi Jutia sikiliza Nyimbo za Huyu Mwamba💥💥💥💥💥💥💥💥💥
Najifunza vitu vingi sana kutoka kwa Black maradona kweli huo umeme ni wa Cable nying
Dah speechless, nawaambia kila siku kitaa kuhusu huyu mwana. Umenifanya nifute nyimbo zote, nibaki na zako tu
Mpaka unatamani kama Kuna next episode... Mf you rock🔥
Dizasta wewe basi tena leo ndo nimethibitisha Upo kwenye Sayari Ya Peke Yako Hakuna Mtu Anaefikiria Kuandika More than U 🔥🔥🔥
Best lyrical rapper ever top 1 or pin to top1 unatsha sana D_vina🔥🔥🌋
My Teacher vina 🔥🔥
Vina!!! Kichupa kimenyooka we ni nyoko√√√
nimemsikia kaa humo ndan . hop kuna goma lingine atahusika mna chemistry nzuri saaana. goma limeenda bro
Dizasta Vina Ni kina Jo 70🙌
Dah..!😢😢😢 Teacher unajua
😂😂😂 baba jesca general kabsa.. ninja ninja hunter
daaah me cna neno mkuu umetisha humu✌️✌️✌️✌️✌️
Kutoka moyoni Nakuelewa sana Mr Tungo love ftom🇧🇮
Oaaa d vina ili tambo limesimaaa mnooo 100%
Heavy weight❤❤vina the role modal
Yo vina Team Nairobi tunakutambua Sana Hip hop ya bongo iko mikono salama❤❤
ANAE ITAKA PARTY 2 KAMA MIMI AGONGE LIKE 👍