Dizasta Vina - Mbuzi

Поділитися
Вставка
  • Опубліковано 7 жов 2024
  • Official Lyric video of the record MBUZI as prepared and performed by Dizasta VIna. Off the studio album, A father figure
    Stream/Download
    UA-cam - • Dizasta Vina - Mbuzi
    Mdundo - mdundo.com/son...
    Boomplay - www.boomplay.c...
    Audiomack - audiomack.com/...
    Apple music - / mbuzi-single
    Other Musical contents
    Audiomack - audiomack.com/...
    Boom play - www.boomplay.c...
    UA-cam - / dizastavina
    Mdundo - mdundo.com/a/2263
    Spotify - open.spotify.c...
    Apple music - / dizasta-vina
    Deezer - www.deezer.com...
    Spotify Playlist - open.spotify.c...
    Connect with Dizasta Vina on social medias
    Instagram - / dizastavina
    Twitter - / dizastavina
    Facebook - / dizastavina07
    sw.wikipedia.o...
    Business: Pan.authentik@yahoo.com
    Website - bio.link/dizas...
    Lyrics
    Mbuzi alipata wadudu kwenye kwato
    Iliathiri furaha na nguvu alizonazo
    Mchungaji alihakikisha mbuzi ananawa
    Aliondoa wadudu wote kisha akamweka dawa
    Alikampangusa chawa akampa chakula kwa wakati
    Akamjengea chumba kwa nafasi
    Ajisikie huru, Akashika ratiba na itifaki
    Muda ukapita afya mbuzi ikatamalaki
    Mtaa ikahamaki ukasukwa uvumi
    Kuwa bwana Kheri Anatoa muda kisha sumni
    Japo hali yake ya uchumi ilikuwa ni duni
    Aliuza matunda mboga chache na kuni
    Hakuna siku mbuzi alipiga kelele kwa njaa
    Watu walimwonea gere balaa
    Alinawiri kwa kilele cha umaridadi
    Majambazi walipiga misele kadhaa
    Na usiku hauwi mwanana akisikia mbiu
    Mbuzi akilalama kwamba anahisi kiu
    Mchungaji alikuwa macho, Akatambua kuna
    Magonjwa nyemelezi akavumbua chanjo
    Mbuzi aling’ara alinona
    Manyoya yalitawala kuashilia afya kila kona
    Hakuwepo hata mwanga mmoja wa kuroga
    Hata Waliojaribu kuchanja walikoma
    Najiuliza maana ya upendo nini
    Mpaka uwe na kingi ndio ushee?
    Au pesa kipindi michango ya sherehe?
    Au mzazi anayetamani uendelee?
    Ndio maana anakulea ile umlee
    Inasadikika kuwa upendo wa kweli ni kujali
    Mama mzazi homa ikikushika tu halali
    Tabasamu analokupa unaposhika Masarali
    Ungekuwa hai ingekuwa kutoa mimba ni halali?
    Wazalendo wanahitaji hela na nyadhifa
    Wanalipwa kutetea sera za taifa
    Wadini wanakumbatia itikadi na imani yao
    Mpaka wanamwaga damu wenzao
    Au mapenzi kwenye timu inapoingia mtimani
    Unaumia inashika mkia na hauhami
    Kufichiana dhambi tabia wanayoisifia masela
    Au mjeshi anavyofia bendera
    Nani anajua siri ya kupenda penda?
    (Ni) kujitoa sadaka kwa ajili ya mwenza?
    Wapo wanaosema kuwa kupenda ni ushupavu
    Wanaumizwa wanachukia wanaandika vitabu
    Ukijua mwenza wako ana mtu anampenda
    Utampa nafasi aende upige moyo konde?
    Mama akifariki na una dawa ya kusahau maumivu
    Swali ni utakula vidonge?
    Je upendo wa kweli ni mpaka aagize mungu?
    Aliyesema ufuge paka alafu umchinje kuku
    Amemmtoa mwanaye kama mdhamini msalabani
    Awafie watu ambao dini hazifanani
    Bado Mawazo yananisumbua nasinzia
    Nawaza ingekuwaje tungechagua familia
    Je mtoto angempenda baba angekuwa lofa?
    Au Baba angemchagua mtoto angejua ni shoga?
    Wanandoa tungekuweka kwenye Time Chamber
    Muda urudi ungemchagua patner wako tena?
    Wangapi wanawish wangepita sehemu hii?
    Wangapi wangemchagua Justin Bieber na Jay Z?
    Kabla ndoa haijakufunga pini
    Jiulize kama mkeo angekuwa na wewe ka' ungekuwa chini?
    Licha ya hizi nyimbo zinazofanya watu walie sana
    Washikaji walingoja niwe msanii ndio niwe mwana
    Pengine inabadili maana ya upendo
    Na kuacha swali upendo je ni haja au matendo?
    Mchungaji alifuga mbuzi alifuga na ajenda
    Alimjali lakini si kwa sababu alimpenda
    Kwani ilipofika sikukuu alitoa vitu
    Sufuria jungu kuu akanoa visu
    Yule mbuzi mzuri aliyenona sana
    Ndiye aliyechinjwa na adhuhuri alichomwa nyama
    read more about Mbuzi genius.com/Diz...

КОМЕНТАРІ • 735

  • @dizastavina
    @dizastavina  5 місяців тому +204

    Nunua nakala yako ya A FATHER FUGURE Kwa whatsApp, Email au telegram. Tuma 10,000tzs au 650ksh kwa Mpesa +255 762 158 871 au Tigopesa +255 655 696 811 (Jina Edger Vicent Mwaipeta). Kisha tuma jina au sms ya malipo kwa hizo namba.

    • @hamismbwana8592
      @hamismbwana8592 5 місяців тому +1

      Ina nyimbo ngap?

    • @thomaslima921
      @thomaslima921 5 місяців тому +3

      Poa big brain rapper,ndyo maana DUBO alisema mc mbovu utakata tamaa ukimsikiliza dizasta we ni darasa tosha

    • @Mungopark187
      @Mungopark187 5 місяців тому +3

      Jamn mkuje sasa mnunue albamu yenye magoma makali.. Verse kali, beats kali.. Yani kilakitu kikali.

    • @terminal_tz
      @terminal_tz 5 місяців тому +6

      Despite being an MC, I bought this Albam na sijajutia ...nafikiri vijana wengi wangefata failsafA za dizasta maana nawaona Akina Karl max Napoleon hill na wengine wengi Sana ktk history...walioongelea kuhusu ukombozi wa kifikra...dizasta katuletea mawazo Yao in a simple form Kwa Lugha adhimu Sana ya Kiswahili akiilenga jamii yetu....AFF ni album yangu pendwa na nasikiliza Kila siku ubongo unapata Chakula...Dizasta is the master Art, and the only orchestrated symphony...

    • @brunoh_bx
      @brunoh_bx 5 місяців тому +1

      Pamoja san kaka👏👏🔥🔥🔥

  • @magotimtani2180
    @magotimtani2180 5 місяців тому +26

    Sehemu ya kwanza ya wimbo inaonekana kuashiria uhusiano kati ya mchungaji na mbuzi kama mfano wa uhusiano kati ya watawala na wananchi, au hata kati ya watu katika jamii. Mchungaji anawakilisha nguvu au serikali, wakati mbuzi anaweza kuwakilisha raia au watu wa kawaida. Mchungaji anajitolea kumtunza mbuzi, ikionyesha wajibu wa serikali kwa wananchi wake, lakini kuna maudhui ya utata kuhusu nia ya mchungaji - je, anamtunza mbuzi kwa upendo wa kweli au kwa sababu ya faida zake binafsi?
    Sehemu inayozungumzia bwana Kheri inaonesha changamoto za kiuchumi na jitihada za kujikimu katika jamii. Ingawa bwana Kheri anajitahidi na hali yake ya uchumi ni duni, anaonyesha uvumilivu na ujasiri katika kukabiliana na changamoto za maisha.
    Katika sehemu inayohusu upendo, wimbo unachunguza maana ya upendo na kujitolea kwa wengine. Inaleta mifano mbalimbali kuhusu jinsi upendo unavyoweza kueleweka na kutekelezwa katika maisha ya kila siku, iwe ni katika uhusiano wa kimapenzi, uhusiano wa kifamilia, au hata katika uhusiano kati ya watu na imani zao au utamaduni wao.
    Mwisho wa wimbo unatoa picha ya kusikitisha ambapo mbuzi, licha ya kutunzwa na kustawi chini ya uangalizi wa mchungaji, anakatwa na kuliwa. Hii inaweza kuashiria udanganyifu wa watawala au nguvu kuu katika kutumia na kudhulumu watu wa kawaida kwa manufaa yao binafsi, huku wakionekana kama wachoyo au wasiojali.
    Na hii verse ya mwisho ndio inasahihisha nia ya utata inayotajwa katika verse ya kwanza.
    Verse ya kati, ni kama anaonesha tu upendo wa kweli ni nini, ili aje afanye hitimisho vema kwenye verse au eneo la mwisho

  • @insectondama798
    @insectondama798 5 місяців тому +9

    Mchungaji alifuga mbuzi
    Alifuga na agenda
    Alimjali, lkn si kwa sababu alimpenda
    Kwani.....
    Ilipofika sikukuu ..alitoa vitu
    Sufuria jungu kuu.. akanoa kisu
    YULE MBUZI MZURI ALIENONA SANA , NDIE... ALIECHINJWA NA ADHUHURI ALICHOMWA NYAMA

  • @lukasbuyamba4135
    @lukasbuyamba4135 5 місяців тому +8

    Hem ngojeni kwanza. Mna hakika huyu jamaa ni mwanadamu wa kawaida.. aseeee big up brother Ediga

  • @gotintito4455
    @gotintito4455 5 місяців тому +14

    Rafiki zangu wengi wamekuwa wafuasi wa dizastavina baada ya kuwasikilizisha ngoma kazaa...Jana Tu Kuna mwana mmoja kaisifia sana hii ngoma alafu Leo umekuwa released aisee...tunaomba uandae show moja Yako mwenyew tutaingia kwa gharama yoyote.

  • @SAMAMBIRE
    @SAMAMBIRE 5 місяців тому +9

    Mnasifia sana tungo za vina ila mnajifanya kama hamuoni namba za kutuma iyo miamala mazee afu kesho na kesho kutwa vina aka pause music mtasema vina kapotea

  • @jovinkivelege7604
    @jovinkivelege7604 5 місяців тому +6

    SIO POA WE JAMAA UNAJUA

  • @QoberConstant
    @QoberConstant 5 місяців тому +5

    Aseee nmeelewa kuwa ukiskiza nyimbo za vina ni sawa na siskilizi nyimbo za wanadamu wenzetu..bado natafuta jina la kiumbe wa kumuita tofaut na binadam wa kawaida ila sijafankiwa kupata asee👊🏼🙌

  • @allychilinga1958
    @allychilinga1958 5 місяців тому +11

    Ina pigwa violin inapigwa guitar Tunasikia neno baada ya neno..mpangilio mzuri wa Mashahiri hakuna yo-yo..

  • @msimika_III
    @msimika_III 5 місяців тому +4

    Nadhani ni muda wa kukubali sasa kuwa Dizasta vina ndie msanii mwenye maarifa mengi zaidi na ana namna nzuri zaidi ya kufikisha kuliko msanii yeyote wa hip hop kwa sasa
    Asilimia 90 ya nyimbo za hip hop bongo humalizi hata verse moja unaona unazichosha tu ngoma za masikio yako, lakini ukimsikiliza muwa wa Dizasta vina unatamani hata uwe na verse kumi
    Dizasta vina ndie msanii pekee ambaye huwa nakuwa na shauku sana ya kusikia his next project, bro is pure genius, too good for this industry
    Sijui hii nyumba ya hip hop imebaki na mihimili mingapi mpaka ianguke ila Dizasta vina ni miongoni mwa mihimili inayofanya ili jumba la hip hop lisianguke
    All the best Dizasta vina natumai utakuwa na Madusko yanayoendana na kipawa chako na juhudi ulizowekeza kwenye sanaa yako

  • @YunusYahya-gr6ks
    @YunusYahya-gr6ks 5 місяців тому +8

    Waliorudiaa hio nyimbo Zaid ya.mara 10 piga like hapa Jamaa anauwasha Hakuna kama hii kichwaa

  • @JosephRobert-uf5dr
    @JosephRobert-uf5dr 5 місяців тому +3

    Dizasta aseee sema media za bongo chai sana hawasikiagi hivi vyuma kutoka kwa mwana kuvichaka...

    • @terminal_tz
      @terminal_tz 5 місяців тому

      Sisi hatutaki media za Bongo....tununue Albam Kwa Dizasta ...Vina

  • @susumantalanta8505
    @susumantalanta8505 5 місяців тому +6

    Siku zinakuja hili Taifa litabadilika, vijana hawata kuwa inspired na machawa bali ngoma kama hizi....thamani yako itakuwa ya juu sana....Big Up Rasta

  • @CertifiedStoic
    @CertifiedStoic 5 місяців тому +8

    Tulionunua Album day one tu ilivyotoka tunakosa cha ku-comment maana tulishachambua wimbo mpaka tukauchambua tena. Big Up Vina 🙌

  • @robygeniuz
    @robygeniuz 5 місяців тому +5

    Nadiliki kusema tangu niwe mshabiki wa HIPHOP uyu mwamba ndio msanii wangu bora tangu niijue hiphop nikiipokea mikononi mwa prof J oyaaaaa 👊

  • @ibni_H2TL6r
    @ibni_H2TL6r 5 місяців тому +6

    Coment Yangu Ni Ya 99 Dizasta Vineration 17 April 2024 when you read My Comment In 2099 Generation this Dude Was The Best & Genius

  • @JREMPIRE-jd1ms
    @JREMPIRE-jd1ms 5 місяців тому +7

    mifumo ya taifa letu d..vina umeuwa...🙄🙄 yule mbuzi mzuri aliyenona sana ndiye aliyechinjwa na adhuhuri alichomwa nyama......

  • @Antary9
    @Antary9 5 місяців тому +6

    BLACK MARADONA. SALUTE KWA MADINI BRO.

  • @lampadshigonko3006
    @lampadshigonko3006 5 місяців тому +5

    Nimeelewa kipande cha mbuzi kinanikumbusha tukio la ngwajima kula muhumini wake.

  • @ismailmtengwa8370
    @ismailmtengwa8370 5 місяців тому +8

    Jamaa kipindi unajiita dizasta vina ulikuwa unajua kuwa jina lako litakuwa linaendana na vina vyako mwanangu unajua sana sioni wakukufananisha nae

  • @ayubukaduma1017
    @ayubukaduma1017 5 місяців тому +4

    vina tungo imesimama mzee , n wateule wachache sanaaa tunaelewa izi chuma unatuachia keep moving broo tunakufuata

  • @Yeah-k3h
    @Yeah-k3h 5 місяців тому +4

    Marafiki zangu wamebadilika na wamekuwa wakielimisha wengine kupitia mistari ya huyu mwamba wengine walipata wapenzi kweli huyu ni Mungu wa Rap 100%

  • @dankirunda3368
    @dankirunda3368 5 місяців тому +6

    Daaah peni imezingatiwa sana humu 🔥

  • @user-badboyrozay
    @user-badboyrozay 5 місяців тому +8

    Vina juu ya vina humu ndani Kuna bonge la disaster kiufupi hamna usalama🔥🔥❤

  • @soudyruge-fi9xv
    @soudyruge-fi9xv 5 місяців тому +4

    Huyu mwamba nilichelewa kumjua ila nilivomjua nikamfanya Best RAPPER wa muda wote haiwezi kupita siku bila kusikiliza ngoma zake kama 5, nikianza na TRIBULATION, ACHIA JALA, WACHEZAJI WA TIMU, NO ONE IS SAFE, (zote) na HATIA (Zote)

  • @omarabdulaziz3786
    @omarabdulaziz3786 5 місяців тому +4

    Level 5 sorcerer kutoka far future!!

  • @stapinuswilliam860
    @stapinuswilliam860 5 місяців тому +4

    Japo hali yake ya uchumi ilikuwa duni liuza matunda mboga chache na kuni

  • @rockonsonmlandi2818
    @rockonsonmlandi2818 5 місяців тому +7

    Mimi naomba bifu ya vina na Rapcha tena 🤤...

  • @godblessluvanda9808
    @godblessluvanda9808 5 місяців тому +8

    Kweriii huyuu jamaa NI NYOKOMBILI 🙌🙌🙌🙌🙌🎧🎧🎧🎤🎤

  • @mchattachattanoga7795
    @mchattachattanoga7795 5 місяців тому +3

    Kweli dizasta akiwaka anaweza kumgeuza fid akawa sajna

  • @mulanmike1997
    @mulanmike1997 5 місяців тому +3

    wa kwanza kucomment
    mbuziiiiiiiiiii

  • @Yegon254
    @Yegon254 5 місяців тому +4

    Hii ni aina ya mziki ninaoupenda haswa wakati nimetulia

  • @shenamtukufu1224
    @shenamtukufu1224 5 місяців тому +4

    Asante sana homie hujawai tufelisha wana.

  • @antonyngao131
    @antonyngao131 5 місяців тому +3

    Vina! Vina! Vina,nimekuita ngapi? Noma sanaa

  • @user-badboyrozay
    @user-badboyrozay 5 місяців тому +6

    Vina juu ya vina humu ndani Kuna bonge la disaster kiufupi hamna usalama🔥🔥

  • @rigajunior8487
    @rigajunior8487 5 місяців тому +4

    Mwanangu...! Sema tu kiki ndo hunaga but katika watu ambao ni blessed na branded upo kaka yan ni wewe na darassa yani ni brand za kitofauti mno na ladha kali❤❤. Mbeyahood.

  • @AhmedYasseen-eg2kz
    @AhmedYasseen-eg2kz 5 місяців тому +1

    Black maradonaa.....
    Vinaaaa🙌🏾🙌🏾🙌🏾

  • @AhmadMuya
    @AhmadMuya 5 місяців тому +4

    Jaman na mm Leo naombeni like zenu håtä 10

  • @shaddyqualityfurniture3595
    @shaddyqualityfurniture3595 5 місяців тому +4

    Goat 🐐

  • @langemwepesi
    @langemwepesi 5 місяців тому +6

    Kama vile nazama namuona mwamba kadondosha sijui niseme nizare la professa😂❤

  • @khatibkapire877
    @khatibkapire877 5 місяців тому +3

    Dizasta nataka nimguse huenda sio binadam

  • @YunusYahya-gr6ks
    @YunusYahya-gr6ks 5 місяців тому +5

    Yanii huyui mwambaa anapigaa mamboo ambayoo hata fid q anakubalii mwambaa anajua kufichaa maana huyu ni kama langaa wa pilii ila mwambaa sijuii wakumgananisha naee dizastaa ni zaidiii yaoooo aiseeee

  • @bashirusalehenandoro3128
    @bashirusalehenandoro3128 5 місяців тому +5

    Upendo nipamoja na kumtendea mwenzako mema,dhana ya upendo ni pana sana ila kwenye upendo jambo kubwa linalotafsir upendo ni uvumilivu, sabab binadamu ni lazima akosee tu so upendo ndio utafanya chuki isiwagawe anapokosea unaempenda au anaekupenda

  • @DullahXella-xb4cz
    @DullahXella-xb4cz 5 місяців тому +4

    DVN is G.O.T

  • @LudeofficialXworldwide
    @LudeofficialXworldwide 5 місяців тому +2

    Hii Hot Kabsa🔥

  • @VictorKotein
    @VictorKotein 5 місяців тому +2

    Wewe mwamba unajua sana unafanya ubongo wangu utafakari sana

  • @insectondama798
    @insectondama798 5 місяців тому +3

    This ma'faka is an alien💥💥

  • @ahutamorris
    @ahutamorris 5 місяців тому +3

    Utaratibu au mpangilio wa kutuma pesa kutoka Kenya hadi Tanzania ni upi kakangu @Dizasta Vina

  • @dmgaya8856
    @dmgaya8856 5 місяців тому +4

    @Mbuzi 💥💥💥

  • @patrickmgaza9927
    @patrickmgaza9927 4 місяці тому +7

    hapa ndipo tunapopimwa IQ zetu huyu jamaa kama umezoea kuskiliza singeli huwezi muelewa bonge moja la ngoma

  • @allyhabibu1117
    @allyhabibu1117 5 місяців тому +2

    Acha wajisifie nimarapa bora ila wewe ndo mwalim wao✊✊✊

  • @AmanHaonga-c7u
    @AmanHaonga-c7u Місяць тому +4

    Oooh no Dizasta... Mbeya we feel high..reee to have you wish u well 🔥 fire man straight from the cold hooray green town.

  • @Almarsprince254
    @Almarsprince254 5 місяців тому +3

    Nmedakia juu kwa juu,,,❤❤

  • @wizzyjabary7777
    @wizzyjabary7777 5 місяців тому +2

    DIZASTA UMETISHAA SANA UJUMBE MZURIII NGOMA KALIII SANA🎉🎉🎉🎉🎉

  • @wilbardlameck8025
    @wilbardlameck8025 5 місяців тому +4

    Aliyeelewa hii ngoma anieleweshe tafadhari

  • @pcthemaster9096
    @pcthemaster9096 5 місяців тому +3

    Ujawai kosea mzee. Nice

  • @talebanistudio4513
    @talebanistudio4513 5 місяців тому +1

    Oya wanangu wa mziki mzuri kama huu tusiishie ku like na kusifia tununuue ngoma na tisapoti mziki mzuri ili mwana aendelee kutudondoshe ngoma Kali kama hizi Kuna vitu vingi vya kuimba ila wasanii wa bongo banaa mapezi mapenzi wana boa sana dizasta tuna kuaminia wapige msasa wasani wa mapenzi kila siku❤

  • @ramadhanishabani7095
    @ramadhanishabani7095 5 місяців тому +2

    Nakupenda Sana HIP HOP

  • @Goalscorer12
    @Goalscorer12 5 місяців тому +5

    Dizasta vina ni Extraordinary 😂💥💥

  • @tariqkhassim4059
    @tariqkhassim4059 5 місяців тому +6

    BILA MEDULA HUWEZ KUENJOY MZIKI MTAMU HUU

  • @DennisUnju
    @DennisUnju 5 місяців тому +5

    Kudadekiiii unajua we Fara

  • @runtown____3587
    @runtown____3587 5 місяців тому +3

    Bro this guy deserves more support nunueni album much love dizasta.

  • @NachiLapa-zo9ld
    @NachiLapa-zo9ld 5 місяців тому +8

    Magoma ndo kama hayo kutoka kwenye album ya dizasta vina inaitwa a father figure
    😅😅 Sasa kuelewa kilichoimbwa kwenye hizo ngoma inategrmea na matokeo yako ya form four ulipata ngapi!😂😂😂

    • @Voxmediatz
      @Voxmediatz 5 місяців тому

      😂😂😂😂 FOUR KARIBU NA ZERO

    • @musafadhili7950
      @musafadhili7950 5 місяців тому +1

      Na sisi tulio kimbia hata form 4 hatujafika inakuaje hapa😂😂😂

    • @cdeegwau551
      @cdeegwau551 5 місяців тому

      😅😅😁

  • @elizajafaphary6559
    @elizajafaphary6559 5 місяців тому +3

    Umetisha mkali wa vina 🔥🔥🔥

  • @innowatamaduni9248
    @innowatamaduni9248 5 місяців тому +2

    Sawaaaaa mzee

  • @Jida-tz
    @Jida-tz 5 місяців тому +4

    Kama masikio na akili zako vilishazoea kusikia "WEE ZOMBII,,HAUJUIII" hapa hutoelewa kitu😂😂😂

  • @mbegumohammed7398
    @mbegumohammed7398 5 місяців тому +3

    Yani huyu mwamba kashashindikana kabisaaa🙌🙌

  • @JosephRobert-uf5dr
    @JosephRobert-uf5dr 5 місяців тому +1

    This man is not a human asee dizasta ni monster

  • @essauleesomogo2468
    @essauleesomogo2468 5 місяців тому +4

    Je upendo wa kweli aliagiza mungu aliesema tumfuge paka tumchinje kuku?? 😂🙌🙌🙌😊

  • @AdveraPhilipo
    @AdveraPhilipo 5 місяців тому +2

    nikiwa mkubwa niwe kama wewe, sijui unamaanisha Nini huu wimbooo😢😢😢😢😢😢😢

  • @bahopamontana6381
    @bahopamontana6381 5 місяців тому +2

    Kama kweli unampenda Dizasta em tukanunue Iyo nakala ya A FATHER FUGURE mapema saaaaaana... 2:36

  • @KijukuuMtemi
    @KijukuuMtemi 5 місяців тому +4

    Makonda hii nyimbo isikulize kuna vitu utajifunza ukiisikiliza kwa makini @

    • @KijukuuMtemi
      @KijukuuMtemi 5 місяців тому

      Hii nyimbo imfikie makonda

  • @tariqkhassim4059
    @tariqkhassim4059 5 місяців тому +4

    SOON HUU MZIKI UNAANZA KUA NO 1 ON TRENDING INSHAALAH

  • @jrluhombo
    @jrluhombo 5 місяців тому +3

    Mwisho wa siku mbuzi akaliwa nyama😂

  • @NestymwampambaMwampamba
    @NestymwampambaMwampamba 5 місяців тому +3

    Mbuzi🔥🔥 ❤❤❤

  • @emmanueljames9215
    @emmanueljames9215 5 місяців тому +5

    👊 vina kisha somo, umesomeka vina uwezo wako hauwezi kupimwa kwa tuzo za pombe

  • @cdeegwau551
    @cdeegwau551 5 місяців тому +2

    😅😅😅 🙌 flow tamu, beat imetulia., japokua sijaelewa amemaanisha nin, DVN ni Allien 🙌

  • @abelmsaki
    @abelmsaki 5 місяців тому +2

    Kazi nzuri sana mwana fanya kazi moja na bele 9 am sure it will be a banger

  • @Mwalimu_seleman
    @Mwalimu_seleman 5 місяців тому +8

    Dah. Nilivoona title nikajua distrack kwa Lunya. Nikafungua kusikiliza. Ila huyu mwamba bwana Anatumia akiri nyingi kwenye kitu kidogo sijui atafanyaje vitu vikubwa.😂😂😂 kwani ungeiita UPENDO ungepungukiwa nini hahaha😂. Heshima kwako vina.

    • @mckoba2428
      @mckoba2428 5 місяців тому

      Mwalimu nimekupata vizur maana ya hii ngoma ila ata sikuelewa

  • @hasanibakari6924
    @hasanibakari6924 5 місяців тому +4

    Serikali hainitambui na ushairi Wangu shule 😂👏👏👏🙌

  • @sharifukitori239
    @sharifukitori239 5 місяців тому +3

    Huu wimbo umeacha athari chanya katika mtazamo wangu kuhusu maana ya upendo..nina maswali kadhaa ambayo nimekosa majibu hadi sasa lakini kukosa majibu huko kunanifanya nitabasamu kila mara ninapojiuliza maswali hayo hayo.
    GOOSEBUMPS
    1:16
    1:48
    2:00
    2:12
    Nahitimisha..Ringle ni mmoja wa Goated producers wa hapa bongo.
    Vinanda ya humu ni vyamoto mno kuvigusa🔥

    • @dizastavinafanaccount
      @dizastavinafanaccount 5 місяців тому +3

      Mwisho hapo wameandika Music by Dizasta kaproduce Dizasta hii. Beats za Ringle zina sign tag ya jina lake

  • @boygavana4674
    @boygavana4674 5 місяців тому +3

    VINAAAAAA

  • @nicksonchisunga3062
    @nicksonchisunga3062 5 місяців тому +4

    GOAT DIZASTA VINA

  • @josephmasenga7718
    @josephmasenga7718 5 місяців тому +2

    Nipo kwenye top 2 and iam not second ile ngoma uliua sana

  • @hashimswalehe1550
    @hashimswalehe1550 5 місяців тому +2

    ukijuwa mwenza wako ana anampenda
    utampa nafasi aende upige moyo konde🔞🧠🎤🎤

  • @newzhots4431
    @newzhots4431 5 місяців тому +3

    Fireee💥💥

  • @dismasmushi9328
    @dismasmushi9328 5 місяців тому +6

    Kila siku unaniachia lines kwa kichwa leo nmeshika hii,,, je mtoto angempenda baba angekuwa lofa au baba angemchagua mtoto angejua nishogaa

    • @vancykhan234
      @vancykhan234 5 місяців тому +1

      na wangap wangechangua huu wangap wangemchangua justin bibier na jay z

  • @fredjachi7008
    @fredjachi7008 5 місяців тому +2

    Conscious 🧠

  • @Simulizitube
    @Simulizitube 5 місяців тому +3

    Ukweli ni kwamba hakuna mapenzi ni maslahi yetu tu ila binaadamu tunadanganya mpaka nafsi zetu Maana hata mungu angekuwepo kweli na anavyodai anatupenda Kisha atutese ndio atupe pepo ni ujinga na uvundo tuliokaririshwa

  • @kabatelletv4157
    @kabatelletv4157 5 місяців тому +2

    Kendrick lamar wa bongo..

  • @gaddibullahtzg5635
    @gaddibullahtzg5635 5 місяців тому +2

    Dizasta vinaaaaa umetisha sana nasubiri uchambuzi but you deserve great Honor in Hip-hop Industry

  • @nickbway2052
    @nickbway2052 5 місяців тому +2

    Mbn kama bado haija isha mkuuu🎉

  • @husseinshabani429
    @husseinshabani429 5 місяців тому +4

    🐐

  • @BonyTz
    @BonyTz 5 місяців тому +84

    ivi uyu mwamba ni mtanzania kweli 😅😅

    • @leonardmhagama5828
      @leonardmhagama5828 5 місяців тому +10

      😅😅😅Aseee mwenyewe simuelew huyu mwamba sasa tukubaliane tu kuwa yeye ni toleo la mwisho la chapa yake.

    • @invocavitmbise5296
      @invocavitmbise5296 5 місяців тому +8

      Hahahahaha wee unawaza kama ni Mtanzania badala ya kuwaza kama yupo duniani??😂😂

    • @allyseba172
      @allyseba172 5 місяців тому

      ​@@invocavitmbise5296mm nime skilza lakin daaah sjaelewa bado

    • @denzetz3391
      @denzetz3391 5 місяців тому +3

      Ni m-argentina husikii MARADONA

    • @hinikasteve176
      @hinikasteve176 5 місяців тому +3

      Ni mtanzania ila.sio binadam mwenye akili ya kawaida

  • @mozu2450
    @mozu2450 5 місяців тому +4

    Lazima uwe msomi na mwenye falsafa ya hiphop ndo uweze kumuelewa DIZASTA🔥

    • @makero04
      @makero04 5 місяців тому +2

      Oya hii ngumu mno

    • @ibrahimmrutu
      @ibrahimmrutu 5 місяців тому

      ​@@makero04🤣🤣🤣

  • @MalickMazikublood-gq2fs
    @MalickMazikublood-gq2fs 5 місяців тому +3

    Hivi dizasta unavyo andika wimbo kichwa kinakua kinauma au kuna machine unatumiga kutungia nyimbo zako, mm nahis sio kichwa cham2 kinacho andikaga

  • @Dyram_dee
    @Dyram_dee 5 місяців тому +4

    Tulio na vichwa vibovu tusiumize sana kichwa. Maana ya hii ngoma ni kutaka kuhoji au kuuliza "NI NINI MAANA YA UPENDO..??"
    Mbuzi ni ametumika tu kama icon ya kujua kutofautisha kati ya jinsi watu wanavyoelezea kuhusu upendo, na upendo wenywewe jinsi ulivyo. 🤔
    Kwa upande mwengine nyimbo unawe uhusisha upendo kati ya watawala wetu na raia wa kawaida. Viongozi huwa wanacare sana time ambayo wanahisi kwao ni timing nzuri ili akuandae kisaikolojia but mwisho wa siku inakuwa ni tofauti na unavozani, kwa maana lengo lake likitimia hutokuwa na faida tena bali ni kubuluzwa tu. 🤒
    N.B Huyu jamaa ni mwandishi na nusu. 🔥🔥🙌🙌
    Unaeza itafsiri nyimbo kwa angle nyingi sana. 🙌🙌🔥🔥

  • @ChuxDaniel
    @ChuxDaniel 5 місяців тому +3

    the verteller ❤❤❤🔥🔥🔥🔥🔥

  • @SeifMgulumbi
    @SeifMgulumbi 5 місяців тому +2

    Mbuzi kama mbuzi

  • @ammyskills5588
    @ammyskills5588 5 місяців тому +3

    Huyu jamaa ni noma 🔥