Safari Ya Adam Mchomvu, Kusoma Uganda Mpaka Kufanya Kazi Clouds | SALAMA NA ADAM MCHOMVU PART 1

Поділитися
Вставка
  • Опубліковано 8 лют 2025
  • #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
    Adam Mchomvu ni jina kubwa kati ya majina makubwa ya watangazaji mahiri ambao nchi yetu imeshawahi kuona. Toka kuanzishwa kwa Radio za FM hapa nyumbani ambayo ilikua miaka ya kati kati ya 90 mpaka mwanzoni mwa miaka ya 2000, hapo pia ndo kilipoanza kuzalishwa kizazi cha watangazaji na ma DJ mahiri ambao pia kwa kiasi kikubwa waliweza kulisukuma soko la vipaji mbali mbali vya muziki na filamu kufikia hapa vilipo leo hii. Kazi nzuri iliyotukuka ambayo pia imejaa jasho machozi na damu ilipitiwa. Mpaka leo hii ukiona watu wana launch album zao au filamu zao ujue kuna kazi nzuri ya kujenga misingi ilifanywa na walioianza kazi hii miaka hiyo ya nyuma.
    Kwa uelewa wangu Adam ni Generation ya tatu ya wimbo hilo la watangazaji, ukiachana na kina Charles Hilary, Abubakar Liongo na Marehemu Misanya Bingi au Mike Mhagama, kizazi kilichofuata baada ya hapo ni hiki chetu, cha kiza Dozen na Fetty na Anna Peter na kina Adam Mchomvu. Generation sasa ya Bongo Flava na Bongo movie. Kizazi hiki ndo ambacho umahiri wa Adam ulianza kuonekana, XXL bila ya yeye kwa asilimia 100 utalisikia pengo lake, aina ya matamshi na kusema mambo kwa jinsi yalivyo ndo kumemjengea huo upekee. Ila pia ukaribu wake na wasanii wa Bongo flava pia umesaidia kumpatia story za ndani kabisa pamoja na kujua maendeleo ya kazi zao na struggle zao.
    Pengine ukaribu huo ndio ulimfanya na yeye atake kuwa mwana muziki?
    Sote tunajua kama mziki una mambo yake mengi sana, pengine wewe unaweza ukadhani unauweza na ni rahisi sana kuufanya lakini nadhani ukimuangalia Adam na kumfuatilia kwa kiasi kikubwa unaweza kujua ugumu wa zoezi zima maana kwa mtu kama Adam ambaye yuko jikoni kabisa ameshindwa kufanya muziki kama kazi yake nyengine au kama ambavyo yeye angetaka iwe muziki ndo maisha yake, si tahisi kama ambavyo unadhania. Kwa miaka ambayo nimekua nilifanya kazi kama mtangazaji wa Radio nimeona watangazaji wengi nao wakitaka kujikita kwenye muziki, ambao wamefanikiwa ni wanawake zaidi kuliko wanaume. Adam ameniambia kwenye maongezi yetu haya kwamba wakati mwengine anaona kama watu wanahisi hayuko seriou pengine, pia ameniambia kuhusu utajiri wa nyimbo alizonazo kwenye hifadhi yake. Hii pia imenionyesha jinsi tunavyokua tunafanya kazi ambayo wewe una hakika nayo ni nzuri sana ila kwa watu upokeaji wake unakua sio kama ambavyo wewe umetegemea.
    Mi naamini kuna siku tutamuelewa tu maana kwa kumskiliza tu utaelewa utashi wake na jinsi ambavyo anaangalia vitu na uelewaji wake. Kwa wengi Adam ni HODARI na ambaye ameweza kufanya kazi kwa muda mrefu na kuwa muaminifu pia kwa muajiri wake, kama unakumbuka hapo katikati kulikua na wimbi la wafanyakazi wa Radio kupata ofa kubwa za kuhamia Radio nyengine, na nna uhakika mwingi na yeye ofa hizo alizipata, tena nyingi ila aliamua kuendelea kubaki palepale alipokua. Tunaambiwa loyalty haiuzwi wala huwezi kumfundisha mtu, ni aidha unakua nayo au hauna.
    Humu mimi na yeye tulizungumzia mwanzo wake, fahamu zake za vitu na maamuzi yake ya kutaka kufanya kazi ambayo anafanya leo. Jinsi ambavyo wazazi au mzazi wake alilipikea hilo. Pia nilitaka kujua mazingira ambayo amekulia, humu amenielezea utukutu wake na jinsi ambavyo alikua na uwezo wa kumdanganya Mama yake ilimradi aishi kwenye aina ya maisha ambayo alikua ameichagua. Na jinsi pia ambavyo aliweza kujichomoa kutoka kwenye dunia hiyo ambayo ilikua imejaa kupotea kama asingekua makini.
    Yangu matumaini kuna kadhaa ya kujifunza na yatakua na faida kwako na kwa uwapedao.
    Love,
    Salama.
    Support us through anchor.fm/yahs...
    SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
    Listen our Podcast on
    Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
    ‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
    GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
    Audiomack Link bit.ly/YahSton...
    ‪UA-cam Link bit.ly/UA-camS...
    Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
    Follow:
    Twitter: / yahstonetown
    Instagram: / yahstonetown
    Facebook: / yahstonetown
    Channel Administered by Slide Digital
    Instagram: slidedigitaltz
  • Розваги

КОМЕНТАРІ • 216

  • @mahinga
    @mahinga 2 роки тому +73

    Tunataka Millard ayo munipe like kama tunakubaliana

  • @joiana4663
    @joiana4663 Рік тому +3

    Adam Mchomvu the krislam, imekaa vizuri

  • @RazakiMmalinda-rl3ej
    @RazakiMmalinda-rl3ej Рік тому +3

    Adam mchomvu namkubali xn

  • @innocentsimika1937
    @innocentsimika1937 2 роки тому +11

    Adam is most recognised media personality in Tz.. Mshikaji anajielewa sana, Akili yake inafanya kazi effectively..
    Ona hapo alivyowatoa matongotongo wafiadini na wale wanaojifanya wakihudhuria sana huko kwenye majumba ya ibada ndio kuiona pepo.

  • @maigajohn5828
    @maigajohn5828 Рік тому +1

    Salut kwako salama jabir

  • @emmanuelnzaligo6262
    @emmanuelnzaligo6262 2 роки тому +18

    Napenda sana interview za Adam Tisha sana.

  • @hildayona852
    @hildayona852 2 роки тому +2

    Dada salamà nakukubali mno kwanza tangu no kuone nampenda sana kitu unacho kisema kweli uko vinzuri naomba mungu sikumoja tuonane tuongee

  • @edgardevis8152
    @edgardevis8152 2 роки тому +14

    Napenda sana Hiki kinamafunzo mengi yamaish nk
    Naomba 2wekeeni na yamchungaji Rich

  • @msafirikilongo7429
    @msafirikilongo7429 2 роки тому +7

    Salama ungekuwa mwalim Basi ingekuwa unafundisha watoto na wangekuelewa sana.......humble

  • @shabanijuma2085
    @shabanijuma2085 2 роки тому +1

    Pole siku ukija kujua ushachelewa Mzee.Mungu akupe hidaya.Isha allah

  • @Heismasai
    @Heismasai 2 роки тому +4

    hii Krislam kama nipo nayo jamani!! naamini huyu Mungu wetu ni mmoja wa wote Mimi Mkristo na Waislam Pia...God bless us

  • @allywaziry6419
    @allywaziry6419 2 роки тому +1

    Bangi mbaya sana....

  • @gerry_macopper3808
    @gerry_macopper3808 2 роки тому +3

    Noma sana

  • @makantaafrika
    @makantaafrika 2 роки тому +5

    Mchomvu anabonga sana! Kumsikiliza hachoshi kabisa ✊🏿🙌🏿

  • @chesterbrand6723
    @chesterbrand6723 2 роки тому +4

    His my brother from another religion the first Man kwa dunia Arifu.
    ....

  • @mohammedrashid2906
    @mohammedrashid2906 2 роки тому +1

    Ipo. Sawa

  • @judithsalvatory2892
    @judithsalvatory2892 2 роки тому +2

    Woooow nimewapenda

  • @josephngowoambroce418
    @josephngowoambroce418 2 роки тому +2

    Namjua Issack Momenaaa

  • @baswarimohamedi2766
    @baswarimohamedi2766 2 роки тому +10

    Adamu nakubal sana... presenter

  • @BONGO_FILAMU
    @BONGO_FILAMU 2 роки тому +3

    Huwez Amin nilipanga kusikiliza dakika tatu Ila Mwamba anastory hadi nimemaliza

  • @waziriseif5384
    @waziriseif5384 2 роки тому +1

    Best interview.... nzur san... haichoshi kbs

  • @johariramadhan5236
    @johariramadhan5236 2 роки тому +1

    Namkubali adamu sana

  • @saunyimaaru3133
    @saunyimaaru3133 2 роки тому +1

    Kaza safi

  • @Kibaadvocate
    @Kibaadvocate 2 роки тому +4

    Kubwa sana hiiiii hongera sana mchomvu

  • @mtemi
    @mtemi 2 роки тому +2

    I have to comment on this. Eyooo Mchomvu! Wape Mashavu Wanaaa...!

  • @MzeeKobe_254
    @MzeeKobe_254 2 роки тому +10

    Vicks Kingo was our best advert when growing up in Kenya..🇰🇪🇰🇪🇰🇪 big up!! Your story inspires na sikujua eti wewe Toto la Arusha, kumbe ndio maana kijiti cha majani ni kama ibada, big up Adam Mchovu🤝👏🏿👏🏿👏🏿

  • @YohanaPetro-xv9tp
    @YohanaPetro-xv9tp Місяць тому

    Mchomvu A.k.a Rugha Nyingi namkubali Sana Sana

  • @adolphmwangoje2887
    @adolphmwangoje2887 2 роки тому +2

    Adam bna comed nyingi sana

  • @uzungupoint
    @uzungupoint 2 роки тому +9

    Namkubali sana AD+ daaaah basi tu 🔥🔥🔥🔥🔥🔥

  • @michaelmpagwa2553
    @michaelmpagwa2553 2 роки тому +6

    Mwanangu mwenyewe AD+ namkubali sana

  • @joppagraphix2868
    @joppagraphix2868 Рік тому +1

    Salama na gwajima waiting for it

  • @mmn7480
    @mmn7480 2 роки тому +7

    Napenda salama anavocheka

  • @salumuseif3324
    @salumuseif3324 2 роки тому +8

    Mtangazaji anayependwa na vijana mchomvu

  • @epiphaniaallute2726
    @epiphaniaallute2726 2 роки тому +5

    🤣🤣🤣🤣🤣big up @adammchomvu nimecheka sana Asante Dada Salama umenipa kicheko.

  • @KhamisHaroub-uj5ci
    @KhamisHaroub-uj5ci 8 місяців тому

    Hakuna Krislam hommy # Allah akuongoze ln Shaa Allah uelekee kwenye Haki nothing but sharing good vibes

  • @alexkalonga5323
    @alexkalonga5323 2 роки тому +1

    Uyu mshkaji Mchomvu ni muhuni anaongea kihuni mpka anaharibu interview usela mwingi sana Brother mpka unaharibu

  • @gazzahboy9271
    @gazzahboy9271 2 роки тому +3

    Legend 🚬🚬🚬❤❤❤

  • @thomasboniphace7254
    @thomasboniphace7254 2 роки тому +1

    AD+ umetisha sana

  • @bashiruhassani1017
    @bashiruhassani1017 5 місяців тому

    Adam we 🔥🔥🔥

  • @abdulyamiri3546
    @abdulyamiri3546 2 роки тому +2

    broo umetisha

  • @sakinagumadi225
    @sakinagumadi225 2 роки тому +3

    Yes mchomvu mzee wa johnii johnii yes papaa

  • @all-victorious2156
    @all-victorious2156 2 роки тому +2

    Salama anakuwaga msengemsenge sana wao na T.I.D
    Big up Mchomvu !

  • @emmamatemu8225
    @emmamatemu8225 2 роки тому +2

    Oyaa leo sawaa mtu sahihi

  • @akidajulius8397
    @akidajulius8397 2 роки тому +7

    Da kweli maisha yanaenda Kasi, Salama Amekuwa mmama Sasa jaman da

  • @franksteven
    @franksteven 2 роки тому +6

    I had to pause and comment. What a match of energy this is 🙌🏿🙌🏿
    So much entertainment and education all in one bundle 🎉

  • @selemanbuluba6146
    @selemanbuluba6146 2 роки тому +2

    Kislam tukutane hapa

  • @robinsonjames9711
    @robinsonjames9711 2 роки тому +5

    The Classic presenter AD+

  • @edwardmachaku1661
    @edwardmachaku1661 2 роки тому +4

    Appreciated

  • @godfreybeatusmahavile2250
    @godfreybeatusmahavile2250 2 роки тому +9

    Interview kal sana 🔥🔥🔥🔥🔥🔥📌

  • @simaosamrosa6689
    @simaosamrosa6689 2 роки тому +4

    Interview ni mbaya kwa kwel I can't lie . Anahisi kama ana present bado

  • @ufugajiwetu7782
    @ufugajiwetu7782 2 роки тому +1

    Bonge la story tamu

  • @GemmaSalim
    @GemmaSalim 6 місяців тому

    Ndo ela yako ya mwisho uko vizur kaka

  • @stevewanga957
    @stevewanga957 2 роки тому +10

    Huaga namuelewa sana Salama ...much love from 🇶🇦🇶🇦

  • @andrewndotela7407
    @andrewndotela7407 2 роки тому +6

    sasa leo umecheza mtu wangu... naacha kazi nicheck hii interview

    • @MzeeKobe_254
      @MzeeKobe_254 2 роки тому +1

      Mimi naicheki na niko job shift vinomanoma hadi na replay 😅😅

    • @andrewndotela7407
      @andrewndotela7407 2 роки тому

      @@MzeeKobe_254 Hahahah

  • @kingmaina1151
    @kingmaina1151 2 роки тому +3

    Aaaaah hii kali sana nataman muda ungeongezwa 😂😂😂😂😂

  • @mbwanamtessa8607
    @mbwanamtessa8607 2 роки тому +9

    Interview imempata mwenyewe Sasa hapo. Yani hapo mnainterviweana

  • @husnaharuna5480
    @husnaharuna5480 2 роки тому +1

    Huyu jamaa namkubali kinoma

  • @bobsalim4285
    @bobsalim4285 2 роки тому +1

    Kama huamini Mungu sema tu huna dini.
    Usiseme una dini zote mbuli na hujui la kujibu.
    Kama waamini Mungu,iliweka swala ziwe swhemu husika.
    Kuna swala na kuomba mahitaji yako.
    Mahitaji waweza omba popote.
    @salama for all interviews ume do,huyu ameharibu.

  • @casablancastudioarusha775
    @casablancastudioarusha775 2 роки тому

    Acha nitie neno hapa
    #Bonge la show 🔥

  • @rosegideon336
    @rosegideon336 2 роки тому +2

    Salama wish u all the best.

  • @aristidrichardmrema536
    @aristidrichardmrema536 2 роки тому +2

    Adam adam mwanetu sana

  • @gloryleon4187
    @gloryleon4187 2 роки тому +5

    Kiruuu, salama muhoji kistaarabu, achelewi huyo ku🤸

  • @imanichando2534
    @imanichando2534 2 роки тому +2

    Nimependa sana hii show madam salama

  • @youngblack6917
    @youngblack6917 2 роки тому +4

    I'm the first one today...
    I love you salama all the way from Zambia

  • @UgandanAllstar
    @UgandanAllstar 2 роки тому +1

    MY DAWG ADAM

  • @ufugajiwetu7782
    @ufugajiwetu7782 2 роки тому +7

    My favorite interview

  • @utamutv_
    @utamutv_ 2 роки тому +1

    Adamu namkubalisana anajua mpaka anaboa

  • @babag7138
    @babag7138 2 роки тому +2

    Baba john hatari sanaa💥💥💥

  • @kafumash9816
    @kafumash9816 2 роки тому

    Me ukufwatilia sana kutoka Nairobi Kenya

  • @abrahammollel7141
    @abrahammollel7141 2 роки тому +1

    dingi wa hm katisha, salama mwambie Adamu anifundishe namna ya kufunga mastyle hiyo kitu hapo shingoni nazikubali kinoma bas arif

  • @Igauf3
    @Igauf3 2 роки тому +23

    Adam is a great storyteller ! 😂

  • @andrewmgaya310
    @andrewmgaya310 2 роки тому +4

    Chrislam 🤣🤣 I like that na ni sana bcoz it comes from brother from another mother 🙌🏾

  • @samsonwilliams2505
    @samsonwilliams2505 2 роки тому +1

    🔥🔥🔥🔥 bonge la interview

  • @adolfmathew9698
    @adolfmathew9698 2 роки тому

    Wape mashavu Wana @adam mchomvu. #chuga #republic

  • @hitmanhunter9557
    @hitmanhunter9557 2 роки тому +1

    Viti vimechoka sister mkibadilisha itakua pouwa

  • @lawrencemwakyonde8655
    @lawrencemwakyonde8655 2 роки тому

    Kipindi safi sana

  • @johmafareal6730
    @johmafareal6730 2 роки тому +1

    Adamu ni mtu mwenye heshima saaana kwenye game ya bongoflava .........jamaaa uzuri anafanya kitu anachokipenda

  • @jacklineswallo3643
    @jacklineswallo3643 2 роки тому +1

    🔥🔥🔥🔥

  • @mynambwambo2072
    @mynambwambo2072 2 роки тому

    Yani huchoki kumsikiliza ...This interview is 💥💥💥💥

    • @pascarmwatosya6815
      @pascarmwatosya6815 2 роки тому

      Daa nimecheka Sana Sana Mambo lokapu Tena toli wa ajabu

  • @jandaboytzz2755
    @jandaboytzz2755 2 роки тому +1

    Adamu Mtu Peac Sana🖐️

  • @winifridambilinyi8043
    @winifridambilinyi8043 2 роки тому +4

    Ila adam🙌🏽😂

  • @NickTrickaddictedboy18
    @NickTrickaddictedboy18 2 роки тому +2

    Sauti haijatokea vizuri. Nahisi kuna kitu hakikukaa sawa kwenye editing za sauti.
    All in all hongereni kwa kipindi. Nick Trick hapa niko Maputo Mozambique

  • @abdallahmabondo8566
    @abdallahmabondo8566 2 роки тому +3

    Adam The First Man On The Earth

  • @maryshirima1234
    @maryshirima1234 2 роки тому

    Alivyoanza tu kujibu swali la kwanza mie hoi...😂🙌😂

  • @ismailmshana2828
    @ismailmshana2828 2 роки тому

    Adam Ni mtt wa kihuni

  • @salumjumah5648
    @salumjumah5648 2 роки тому

    Baba joniiiii

  • @r14kgroup68
    @r14kgroup68 2 роки тому

    Hili jembe nalakubali kinom

  • @michaelkipara8205
    @michaelkipara8205 2 роки тому +2

    jamani salama na zuchu tunaisubiri,I love zuchu much

  • @abdullyndwatta9427
    @abdullyndwatta9427 2 роки тому

    Tunamtaka ney wa mitego

  • @robbywilson224
    @robbywilson224 2 роки тому

    kinachonishangaza bongo watu]hawa wapi'Heshima Wanayostahili Hawa watangazaji wa3 -Fety Mchomvu Na B12…wameipigania sana bongo flavor watu kuielewa km ni kazi sio Uhuni…Ndiomana kila mtangazaji wa kipindi km Chao ataiga swaga zao…

  • @williamkavindi8520
    @williamkavindi8520 2 роки тому +1

    Uwe unabadilisha hilo tisheti Salama!!!

  • @goodlucksway1456
    @goodlucksway1456 2 роки тому +2

    🤣🤣🤣🤣🤣aisee nimecheka sana

  • @Boaz22
    @Boaz22 2 роки тому +5

    Bangi mbaya nyie,mnamsikia vizuri Adam lakini😂😂😂

  • @jorickmaanga3131
    @jorickmaanga3131 2 роки тому

    AD+ 🙌

  • @rogersodero3897
    @rogersodero3897 2 роки тому +2

    Salama tunasubiria Esha buheti

  • @ramazanzibar8264
    @ramazanzibar8264 2 роки тому +3

    Bangi mamae sio poa

  • @BBrown_vevo
    @BBrown_vevo 2 роки тому +2

    Mchomvuuu

  • @boniimsokwa8627
    @boniimsokwa8627 2 роки тому

    tall wa ajabu way back since 89.5 Mbeya fM

  • @HemedKibao-tt7gc
    @HemedKibao-tt7gc Рік тому

    Kutikuamini tu siku ya mwisho hio inakutoa kwenye uislam kwahiyo wewe tayari ni mkristo usichanganye watu

  • @maigajohn5828
    @maigajohn5828 Рік тому

    Adam Mchomvu wape mashavu jombaaa