Safari Ya Adam Mchomvu, Kusoma Uganda Mpaka Kufanya Kazi Clouds | SALAMA NA ADAM MCHOMVU PART 1

Поділитися
Вставка
  • Опубліковано 5 вер 2024
  • #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
    Adam Mchomvu ni jina kubwa kati ya majina makubwa ya watangazaji mahiri ambao nchi yetu imeshawahi kuona. Toka kuanzishwa kwa Radio za FM hapa nyumbani ambayo ilikua miaka ya kati kati ya 90 mpaka mwanzoni mwa miaka ya 2000, hapo pia ndo kilipoanza kuzalishwa kizazi cha watangazaji na ma DJ mahiri ambao pia kwa kiasi kikubwa waliweza kulisukuma soko la vipaji mbali mbali vya muziki na filamu kufikia hapa vilipo leo hii. Kazi nzuri iliyotukuka ambayo pia imejaa jasho machozi na damu ilipitiwa. Mpaka leo hii ukiona watu wana launch album zao au filamu zao ujue kuna kazi nzuri ya kujenga misingi ilifanywa na walioianza kazi hii miaka hiyo ya nyuma.
    Kwa uelewa wangu Adam ni Generation ya tatu ya wimbo hilo la watangazaji, ukiachana na kina Charles Hilary, Abubakar Liongo na Marehemu Misanya Bingi au Mike Mhagama, kizazi kilichofuata baada ya hapo ni hiki chetu, cha kiza Dozen na Fetty na Anna Peter na kina Adam Mchomvu. Generation sasa ya Bongo Flava na Bongo movie. Kizazi hiki ndo ambacho umahiri wa Adam ulianza kuonekana, XXL bila ya yeye kwa asilimia 100 utalisikia pengo lake, aina ya matamshi na kusema mambo kwa jinsi yalivyo ndo kumemjengea huo upekee. Ila pia ukaribu wake na wasanii wa Bongo flava pia umesaidia kumpatia story za ndani kabisa pamoja na kujua maendeleo ya kazi zao na struggle zao.
    Pengine ukaribu huo ndio ulimfanya na yeye atake kuwa mwana muziki?
    Sote tunajua kama mziki una mambo yake mengi sana, pengine wewe unaweza ukadhani unauweza na ni rahisi sana kuufanya lakini nadhani ukimuangalia Adam na kumfuatilia kwa kiasi kikubwa unaweza kujua ugumu wa zoezi zima maana kwa mtu kama Adam ambaye yuko jikoni kabisa ameshindwa kufanya muziki kama kazi yake nyengine au kama ambavyo yeye angetaka iwe muziki ndo maisha yake, si tahisi kama ambavyo unadhania. Kwa miaka ambayo nimekua nilifanya kazi kama mtangazaji wa Radio nimeona watangazaji wengi nao wakitaka kujikita kwenye muziki, ambao wamefanikiwa ni wanawake zaidi kuliko wanaume. Adam ameniambia kwenye maongezi yetu haya kwamba wakati mwengine anaona kama watu wanahisi hayuko seriou pengine, pia ameniambia kuhusu utajiri wa nyimbo alizonazo kwenye hifadhi yake. Hii pia imenionyesha jinsi tunavyokua tunafanya kazi ambayo wewe una hakika nayo ni nzuri sana ila kwa watu upokeaji wake unakua sio kama ambavyo wewe umetegemea.
    Mi naamini kuna siku tutamuelewa tu maana kwa kumskiliza tu utaelewa utashi wake na jinsi ambavyo anaangalia vitu na uelewaji wake. Kwa wengi Adam ni HODARI na ambaye ameweza kufanya kazi kwa muda mrefu na kuwa muaminifu pia kwa muajiri wake, kama unakumbuka hapo katikati kulikua na wimbi la wafanyakazi wa Radio kupata ofa kubwa za kuhamia Radio nyengine, na nna uhakika mwingi na yeye ofa hizo alizipata, tena nyingi ila aliamua kuendelea kubaki palepale alipokua. Tunaambiwa loyalty haiuzwi wala huwezi kumfundisha mtu, ni aidha unakua nayo au hauna.
    Humu mimi na yeye tulizungumzia mwanzo wake, fahamu zake za vitu na maamuzi yake ya kutaka kufanya kazi ambayo anafanya leo. Jinsi ambavyo wazazi au mzazi wake alilipikea hilo. Pia nilitaka kujua mazingira ambayo amekulia, humu amenielezea utukutu wake na jinsi ambavyo alikua na uwezo wa kumdanganya Mama yake ilimradi aishi kwenye aina ya maisha ambayo alikua ameichagua. Na jinsi pia ambavyo aliweza kujichomoa kutoka kwenye dunia hiyo ambayo ilikua imejaa kupotea kama asingekua makini.
    Yangu matumaini kuna kadhaa ya kujifunza na yatakua na faida kwako na kwa uwapedao.
    Love,
    Salama.
    Support us through anchor.fm/yahs...
    SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
    Listen our Podcast on
    Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
    ‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
    GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
    Audiomack Link bit.ly/YahSton...
    ‪UA-cam Link bit.ly/UA-camS...
    Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
    Follow:
    Twitter: / yahstonetown
    Instagram: / yahstonetown
    Facebook: / yahstonetown
    Channel Administered by Slide Digital
    Instagram: slidedigitaltz

КОМЕНТАРІ • 213

  • @innocentsimika1937
    @innocentsimika1937 Рік тому +11

    Adam is most recognised media personality in Tz.. Mshikaji anajielewa sana, Akili yake inafanya kazi effectively..
    Ona hapo alivyowatoa matongotongo wafiadini na wale wanaojifanya wakihudhuria sana huko kwenye majumba ya ibada ndio kuiona pepo.

  • @mahinga
    @mahinga Рік тому +71

    Tunataka Millard ayo munipe like kama tunakubaliana

  • @joiana4663
    @joiana4663 6 місяців тому +2

    Adam Mchomvu the krislam, imekaa vizuri

  • @emmanuelnzaligo6262
    @emmanuelnzaligo6262 Рік тому +18

    Napenda sana interview za Adam Tisha sana.

  • @hildayona852
    @hildayona852 Рік тому +2

    Dada salamà nakukubali mno kwanza tangu no kuone nampenda sana kitu unacho kisema kweli uko vinzuri naomba mungu sikumoja tuonane tuongee

  • @msafirikilongo7429
    @msafirikilongo7429 Рік тому +6

    Salama ungekuwa mwalim Basi ingekuwa unafundisha watoto na wangekuelewa sana.......humble

  • @Kobe_254
    @Kobe_254 Рік тому +10

    Vicks Kingo was our best advert when growing up in Kenya..🇰🇪🇰🇪🇰🇪 big up!! Your story inspires na sikujua eti wewe Toto la Arusha, kumbe ndio maana kijiti cha majani ni kama ibada, big up Adam Mchovu🤝👏🏿👏🏿👏🏿

  • @BONGO_FILAMU
    @BONGO_FILAMU Рік тому +3

    Huwez Amin nilipanga kusikiliza dakika tatu Ila Mwamba anastory hadi nimemaliza

  • @edgardevis8152
    @edgardevis8152 Рік тому +14

    Napenda sana Hiki kinamafunzo mengi yamaish nk
    Naomba 2wekeeni na yamchungaji Rich

  • @makantaafrika
    @makantaafrika Рік тому +5

    Mchomvu anabonga sana! Kumsikiliza hachoshi kabisa ✊🏿🙌🏿

  • @Heismasai
    @Heismasai Рік тому +4

    hii Krislam kama nipo nayo jamani!! naamini huyu Mungu wetu ni mmoja wa wote Mimi Mkristo na Waislam Pia...God bless us

  • @chesterbrand6723
    @chesterbrand6723 Рік тому +4

    His my brother from another religion the first Man kwa dunia Arifu.
    ....

  • @RazakiMmalinda-rl3ej
    @RazakiMmalinda-rl3ej Рік тому +2

    Adam mchomvu namkubali xn

  • @shabanijuma2085
    @shabanijuma2085 Рік тому +1

    Pole siku ukija kujua ushachelewa Mzee.Mungu akupe hidaya.Isha allah

  • @salumuseif3324
    @salumuseif3324 Рік тому +8

    Mtangazaji anayependwa na vijana mchomvu

  • @baswarimohamedi2766
    @baswarimohamedi2766 Рік тому +9

    Adamu nakubal sana... presenter

  • @epiphaniaallute2726
    @epiphaniaallute2726 Рік тому +5

    🤣🤣🤣🤣🤣big up @adammchomvu nimecheka sana Asante Dada Salama umenipa kicheko.

  • @franksteven
    @franksteven Рік тому +6

    I had to pause and comment. What a match of energy this is 🙌🏿🙌🏿
    So much entertainment and education all in one bundle 🎉

  • @uzungupoint
    @uzungupoint Рік тому +9

    Namkubali sana AD+ daaaah basi tu 🔥🔥🔥🔥🔥🔥

  • @judithsalvatory2892
    @judithsalvatory2892 Рік тому +2

    Woooow nimewapenda

  • @gerry_macopper3808
    @gerry_macopper3808 Рік тому +3

    Noma sana

  • @akidajulius8397
    @akidajulius8397 Рік тому +6

    Da kweli maisha yanaenda Kasi, Salama Amekuwa mmama Sasa jaman da

  • @allywaziry6419
    @allywaziry6419 Рік тому +1

    Bangi mbaya sana....

  • @maigajohn5828
    @maigajohn5828 Рік тому +1

    Salut kwako salama jabir

  • @mbwanamtessa8607
    @mbwanamtessa8607 Рік тому +9

    Interview imempata mwenyewe Sasa hapo. Yani hapo mnainterviweana

  • @waziriseif5384
    @waziriseif5384 Рік тому +1

    Best interview.... nzur san... haichoshi kbs

  • @Kibaadvocate
    @Kibaadvocate Рік тому +4

    Kubwa sana hiiiii hongera sana mchomvu

  • @gazzahboy9271
    @gazzahboy9271 Рік тому +3

    Legend 🚬🚬🚬❤❤❤

  • @mmn7480
    @mmn7480 Рік тому +7

    Napenda salama anavocheka

  • @joppagraphix2868
    @joppagraphix2868 Рік тому +1

    Salama na gwajima waiting for it

  • @michaelmpagwa2553
    @michaelmpagwa2553 Рік тому +6

    Mwanangu mwenyewe AD+ namkubali sana

  • @josephngowoambroce418
    @josephngowoambroce418 Рік тому +2

    Namjua Issack Momenaaa

  • @adolphmwangoje2887
    @adolphmwangoje2887 Рік тому +2

    Adam bna comed nyingi sana

  • @godfreybeatusmahavile2250
    @godfreybeatusmahavile2250 Рік тому +9

    Interview kal sana 🔥🔥🔥🔥🔥🔥📌

  • @mtemi
    @mtemi Рік тому +2

    I have to comment on this. Eyooo Mchomvu! Wape Mashavu Wanaaa...!

  • @gloryleon4187
    @gloryleon4187 Рік тому +5

    Kiruuu, salama muhoji kistaarabu, achelewi huyo ku🤸

  • @mohammedrashid2906
    @mohammedrashid2906 Рік тому +1

    Ipo. Sawa

  • @johariramadhan5236
    @johariramadhan5236 Рік тому +1

    Namkubali adamu sana

  • @andrewndotela7407
    @andrewndotela7407 Рік тому +6

    sasa leo umecheza mtu wangu... naacha kazi nicheck hii interview

    • @Kobe_254
      @Kobe_254 Рік тому +1

      Mimi naicheki na niko job shift vinomanoma hadi na replay 😅😅

    • @andrewndotela7407
      @andrewndotela7407 Рік тому

      @@Kobe_254 Hahahah

  • @simaosamrosa6689
    @simaosamrosa6689 Рік тому +4

    Interview ni mbaya kwa kwel I can't lie . Anahisi kama ana present bado

  • @KhamisHaroub-uj5ci
    @KhamisHaroub-uj5ci 3 місяці тому

    Hakuna Krislam hommy # Allah akuongoze ln Shaa Allah uelekee kwenye Haki nothing but sharing good vibes

  • @ufugajiwetu7782
    @ufugajiwetu7782 Рік тому +7

    My favorite interview

  • @alexkalonga5323
    @alexkalonga5323 Рік тому +1

    Uyu mshkaji Mchomvu ni muhuni anaongea kihuni mpka anaharibu interview usela mwingi sana Brother mpka unaharibu

  • @GemmaSalim
    @GemmaSalim Місяць тому

    Ndo ela yako ya mwisho uko vizur kaka

  • @sakinagumadi225
    @sakinagumadi225 Рік тому +3

    Yes mchomvu mzee wa johnii johnii yes papaa

  • @selemanbuluba6146
    @selemanbuluba6146 Рік тому +2

    Kislam tukutane hapa

  • @saunyimaaru3133
    @saunyimaaru3133 Рік тому +1

    Kaza safi

  • @stevewanga957
    @stevewanga957 Рік тому +10

    Huaga namuelewa sana Salama ...much love from 🇶🇦🇶🇦

  • @edwardmachaku1661
    @edwardmachaku1661 Рік тому +4

    Appreciated

  • @robinsonjames9711
    @robinsonjames9711 Рік тому +5

    The Classic presenter AD+

  • @Igauf3
    @Igauf3 Рік тому +23

    Adam is a great storyteller ! 😂

  • @abrahammollel7141
    @abrahammollel7141 Рік тому +1

    dingi wa hm katisha, salama mwambie Adamu anifundishe namna ya kufunga mastyle hiyo kitu hapo shingoni nazikubali kinoma bas arif

  • @emmamatemu8225
    @emmamatemu8225 Рік тому +2

    Oyaa leo sawaa mtu sahihi

  • @all-victorious2156
    @all-victorious2156 Рік тому +2

    Salama anakuwaga msengemsenge sana wao na T.I.D
    Big up Mchomvu !

  • @kingmaina1151
    @kingmaina1151 Рік тому +3

    Aaaaah hii kali sana nataman muda ungeongezwa 😂😂😂😂😂

  • @rosegideon336
    @rosegideon336 Рік тому +2

    Salama wish u all the best.

  • @thomasboniphace7254
    @thomasboniphace7254 Рік тому +1

    AD+ umetisha sana

  • @bobsalim4285
    @bobsalim4285 Рік тому +1

    Kama huamini Mungu sema tu huna dini.
    Usiseme una dini zote mbuli na hujui la kujibu.
    Kama waamini Mungu,iliweka swala ziwe swhemu husika.
    Kuna swala na kuomba mahitaji yako.
    Mahitaji waweza omba popote.
    @salama for all interviews ume do,huyu ameharibu.

  • @ramazanzibar8264
    @ramazanzibar8264 Рік тому +3

    Bangi mamae sio poa

  • @antybabybintrashid2333
    @antybabybintrashid2333 Рік тому +2

    Salama chavu vipo dada

  • @UgandanAllstarTales
    @UgandanAllstarTales Рік тому +1

    MY DAWG ADAM

  • @Boaz22
    @Boaz22 Рік тому +5

    Bangi mbaya nyie,mnamsikia vizuri Adam lakini😂😂😂

  • @utamutv_
    @utamutv_ Рік тому +1

    Adamu namkubalisana anajua mpaka anaboa

  • @aristidrichardmrema536
    @aristidrichardmrema536 Рік тому +2

    Adam adam mwanetu sana

  • @husnaharuna5480
    @husnaharuna5480 Рік тому +1

    Huyu jamaa namkubali kinoma

  • @babag7138
    @babag7138 Рік тому +2

    Baba john hatari sanaa💥💥💥

  • @ufugajiwetu7782
    @ufugajiwetu7782 Рік тому +1

    Bonge la story tamu

  • @johmafareal6730
    @johmafareal6730 Рік тому +1

    Adamu ni mtu mwenye heshima saaana kwenye game ya bongoflava .........jamaaa uzuri anafanya kitu anachokipenda

  • @mynambwambo2072
    @mynambwambo2072 Рік тому

    Yani huchoki kumsikiliza ...This interview is 💥💥💥💥

  • @hitmanhunter9557
    @hitmanhunter9557 Рік тому +1

    Viti vimechoka sister mkibadilisha itakua pouwa

  • @robbywilson224
    @robbywilson224 Рік тому

    kinachonishangaza bongo watu]hawa wapi'Heshima Wanayostahili Hawa watangazaji wa3 -Fety Mchomvu Na B12…wameipigania sana bongo flavor watu kuielewa km ni kazi sio Uhuni…Ndiomana kila mtangazaji wa kipindi km Chao ataiga swaga zao…

  • @abdulyamiri3546
    @abdulyamiri3546 Рік тому +2

    broo umetisha

  • @winifridambilinyi8043
    @winifridambilinyi8043 Рік тому +4

    Ila adam🙌🏽😂

  • @jacklineswallo3643
    @jacklineswallo3643 Рік тому +1

    🔥🔥🔥🔥

  • @abdallahmabondo8566
    @abdallahmabondo8566 Рік тому +3

    Adam The First Man On The Earth

  • @kafumash9816
    @kafumash9816 Рік тому

    Me ukufwatilia sana kutoka Nairobi Kenya

  • @michaelkipara8205
    @michaelkipara8205 Рік тому +2

    jamani salama na zuchu tunaisubiri,I love zuchu much

  • @adolfmathew9698
    @adolfmathew9698 Рік тому

    Wape mashavu Wana @adam mchomvu. #chuga #republic

  • @HemedKibao-tt7gc
    @HemedKibao-tt7gc Рік тому

    Kutikuamini tu siku ya mwisho hio inakutoa kwenye uislam kwahiyo wewe tayari ni mkristo usichanganye watu

  • @samsonwilliams2505
    @samsonwilliams2505 Рік тому +1

    🔥🔥🔥🔥 bonge la interview

  • @Antonycharles2697
    @Antonycharles2697 Рік тому +2

    Ki ukwel kabisa kutoka moyoni hata mimi napenda sana kazi ya presenter ila mm ni fundi umeme

  • @Hashdough
    @Hashdough Рік тому +1

    BEST SALAMA NA ENTERVIEW FOR 2022????

    • @shussein847
      @shussein847 Рік тому

      😊😊😊😊😊😊😊😊😊😊😊😊pppppp

  • @andrewmgaya310
    @andrewmgaya310 Рік тому +4

    Chrislam 🤣🤣 I like that na ni sana bcoz it comes from brother from another mother 🙌🏾

  • @casablancastudioarusha775
    @casablancastudioarusha775 Рік тому

    Acha nitie neno hapa
    #Bonge la show 🔥

  • @imanichando2534
    @imanichando2534 Рік тому +2

    Nimependa sana hii show madam salama

  • @youngblack6917
    @youngblack6917 Рік тому +4

    I'm the first one today...
    I love you salama all the way from Zambia

  • @NickTrickaddictedboy18
    @NickTrickaddictedboy18 Рік тому +2

    Sauti haijatokea vizuri. Nahisi kuna kitu hakikukaa sawa kwenye editing za sauti.
    All in all hongereni kwa kipindi. Nick Trick hapa niko Maputo Mozambique

  • @Abu-Hamza254
    @Abu-Hamza254 Рік тому +1

    Yani kupata mimba nje ya ndoa ni kitu cha kawaida huku Tanzania?

  • @D-Man.B-Free
    @D-Man.B-Free Рік тому +8

    Amevuta bangi,peponi ni hapa hapa motoni ni hapa hapa 🙃🙃🙃🤼‍♀️ pombe sio chai 🤔🤔🤔🥵

  • @usangu_welding_fabric
    @usangu_welding_fabric 9 місяців тому

    Hata atokee Faisal wa aina gani

  • @maryshirima1234
    @maryshirima1234 Рік тому

    Alivyoanza tu kujibu swali la kwanza mie hoi...😂🙌😂

  • @williamkavindi8520
    @williamkavindi8520 Рік тому +1

    Uwe unabadilisha hilo tisheti Salama!!!

  • @simaosamrosa6689
    @simaosamrosa6689 Рік тому +5

    Alipoongea utumbo kuhusu dini basi sikua nasikia chengine chochote after that. Laana

    • @uzungupoint
      @uzungupoint Рік тому +4

      Huenda wewe ndiyo tatizo, jitafakari tena.

    • @henrylyamuya1048
      @henrylyamuya1048 Рік тому +1

      chifuu kabonga kitu true

    • @brokenigga2842
      @brokenigga2842 Рік тому

      Huna akili

    • @Thadeus97
      @Thadeus97 Рік тому

      Stop hating,mind your own shit!

    • @salehsimba5306
      @salehsimba5306 Рік тому

      Na siku ikili yako ukitoka kwenye fikra za kitumwa utajua kama dini ni tamaduni za watu tumeletewa. Utaamka kutoka Gizani utafuata tamaduni zako za Kiafrika. Dini sio Mungu. Ni taratibu za watu. So alichoongea Adam ni Sawa tu. Amka kutoka utumwani

  • @goodlucksway1456
    @goodlucksway1456 Рік тому +2

    🤣🤣🤣🤣🤣aisee nimecheka sana

  • @saumusalimuhassan2499
    @saumusalimuhassan2499 Рік тому

    Salama Mbona Millard Ayo umleti?

  • @rogersodero3897
    @rogersodero3897 Рік тому +2

    Salama tunasubiria Esha buheti

  • @edwinmbugua7738
    @edwinmbugua7738 9 місяців тому

    amejifunika kama hii mic

  • @abdullyndwatta9427
    @abdullyndwatta9427 Рік тому

    Tunamtaka ney wa mitego

  • @ismailmshana2828
    @ismailmshana2828 Рік тому

    Adam Ni mtt wa kihuni

  • @boniimsokwa8627
    @boniimsokwa8627 Рік тому

    tall wa ajabu way back since 89.5 Mbeya fM