Salama Na MASOUD KIPANYA SE6 EP60 | HERI KUFA MACHO… PART 1 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460

Поділитися
Вставка
  • Опубліковано 27 бер 2023
  • #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
    Habibi Masoud Kipanya ni Ally Masoud Nyomwa ambaye ni LEGEND. Kwa mujibu wake alizaliwa huku kakunja ngumi na dhana yake ni kwamba alizaliwa ili awe bondia! Kwa anacho kifanya na ambacho amekua akikifanya tena kwa ufasaha kwa miaka nenda miaka rudi bila ya shaka ni UBONDIA. Hakuna ambaye atabisha juu ya hilo. Amekua akipigania mambo tele na kuyasemea mengi pamoja na kuchekesha na kuelimisha kupitia kalamu yake. Kwa mujibu wake yeye ni mbobevu katika taaluma ya kupuuza na kuchukulia mambo poa kwa kipindi sasa. Lakini pia anaamini yeye ni MTATA. Tukienda mbele na kurudi nyuma, hapo kwenye UTATA hakuna ambaye anaweza kumbishia, hasa kwa wale ambao kalamu yake imewanyoosha kwa kiasi kikubwa.
    Mimi na yeye tulikutana kwa mara ya kwanza takriban miaka kumi na tisa iliyopita, wakati huo mimi mbichi hasa na yeye akiwa kashajielewa na chemchem yake ya kipato tayari ilikua inatoa neema. Mimi nilikua ndo kwanza naanza kazi ya kujishikiza pale Times FM kipindi hiko bado ilikua kule Kamata. Masoud alikua analichorea gazeti la Majira ambalo lilikua liko kwenye mwamvuli mmoja na Radio ambayo nami nilikua nimejishikiza baada tu ya kumaliza skuli. Urafiki wetu ulikuja naturally tu maana sote tunapenda kucheka. Kupitia Zuhura Yunus na Binti mwengine wa kuitwa Rahma ndo mimi naye tulifahamiana. Wakati huo yeye alikua na gari kwahiyo lifti za hapa na pale zilikua hazikauki. Pia tulikua tunaitumia gari yake kama sehemu ya ku chill na kuskiliza muziki kwenye parking za Times FM.
    Huwezi kukaa kwenye tasnia moja kwa muda mrefu kama wewe si hodari na mwenye kujielewa. Moja ya vitu ambavyo naviusudu kutoka kwake ni uelewa wake wa mambo tele wa tele, IQ yake ni ya juu sana na jinsi ambavyo ana reason ndo huwa anamaliza kabisa, kama binadamu wakati mwengine ni bora kukubaliana kuto kukubaliana na kwakwe yeye wakati mwengine jinsi anavyo wachora baadhi ya matukio na watu huwa haviishii kuzuri lakini hiyo haikuwahi kuwa sababu ya yeye kuacha kufanya ambacho anakifanya na ambacho amekua akikifanya kwa muda sasa. Uelewa wake kwenye mambo ambayo yanaendelea, uwezo wake wa kuona mbali na kuweka sanaa yake hiyo kwenye karatasi kisha kutuachia sisi tung’amue maana yake kwa kweli ni kipaji cha kipekee ya sana. Mmoja anatakiwa akae tu mbali na ku admire akifanyacho na hiko ndo ambacho mimi nimeamua kufanya.
    Nilikua nataka anielezee maana halisi ya baadhi ya michoro yake ambayo iliacha gumzo kwa muda mrefu lakini kwa sababu ambazo niliziheshimu alisema asingependa iwe hivyo, uhuru wa kuwaacha watu watafsiri wao ndo raha ya kazi yake ingawa yeye anajua hasa kwanini alichora na maana yake hasa ni nini! Kwa heshima ya sanaa ilibidi nikubali matokeo. Toka umeanza kumjua na kufuatilia kazi yake, mara ngapi ushawahi kuskia Masoud yuko matatani? Yaani kakamatwa au hajulikani alipo? Kwangu mara kadhaa lakini haikuwahi kuwa kizuizi cha yeye kuacha kufanya afanyacho, kuogopa je? Nadhani kama binadamu kuwa na uoga ni jambo la kawaida, ila unafanyaje baada ya hapo ndo tofauti yetu.
    Episode hii inajumuisha karibu yote ambayo niliwahi kutaka kumuuliza, mengine nilipata majibu nlotaka na mengine yalitolewa mbavuni, kwa ki vyovyote vile nili enjoy sana mimi na wenzangu na kutoka kwetu tunatumai nawe uta enjoy kama ambayo nasi tuli enjoy na kujifunza kutoka kwa MWAMBA huyu.
    Love,
    Salama.
    Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
    SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
    Listen our Podcast on
    Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
    ‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
    GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
    Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
    ‪UA-cam Link bit.ly/UA-camSalamaNa
    Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
    Follow:
    Twitter: / yahstonetown
    Instagram: / yahstonetown
    Facebook: / yahstonetown
    Channel Administered by Slide Digital
    Instagram: slidedigitaltz
  • Розваги

КОМЕНТАРІ • 95

  • @GivenTobago
    @GivenTobago Рік тому +3

    Masoud aliwahi kunifundisha kuchora cartoon ilikua ni semina ya wikimbili kwa watoto wa shule ya msingi wenye vipaji vya uchoraji yalikua ni maswala ya usalama barabarani shule ya msingi Naura Arusha Central namshukuru sana nilipata basics nzuri juu ya comic na sasa nafanya Graphics web development na 3d graphics making big up to him.

  • @frankissaya2578
    @frankissaya2578 Рік тому +31

    I wonder why hizi doctorate za heshima hapewi Dr Kipanya

  • @leylamohamed9939
    @leylamohamed9939 Рік тому +6

    Masoud ni Kijana wa Sasa anayeishi mifumo ya Zamani, Birthday, Anniversary SIO ISHUUU... Safi sana 👊🏽👊🏽👊🏽

  • @echolude
    @echolude Рік тому +12

    From a Kenyan based in the states: Masoud has that rare quality of exuding wisdom without much affectation, a wisdom that is edifying & actually locally derived. Apwe Heshima Yake! The same can be states of Salama: a wise woman indeed without being off putting & hyperbolic.

  • @abdallahmdangadachi7030
    @abdallahmdangadachi7030 Рік тому +2

    Sichoki kumuangalia Kipanya toka mkasi hadi Yah Stonetown bonge moja la kolabo Masoud na Salama

  • @onlyacappellaallowed1743
    @onlyacappellaallowed1743 Рік тому +3

    Salama unajua ya jufanya mahojiano mazito yawe kama 'kupiga stori'
    Big up sana

  • @aminanamoyo83
    @aminanamoyo83 Рік тому +5

    We ❤ you masoud kwaajili ya Allah Asante Salama kwa kumleta kipenzi chetu ❤🙏🇹🇿🇨🇭

  • @ramadhanimtetu3656
    @ramadhanimtetu3656 20 годин тому

    Kipanya Kama kipanya

  • @agostineminde6025
    @agostineminde6025 Рік тому +3

    Huyu jamaa anahitaji heshima yake 👍

  • @saumusalimuhassan2499
    @saumusalimuhassan2499 Рік тому +9

    Nakukubali sana Masoud, sijawahi kukereka kwenye interview yako yoyote ile, bro Nakupenda sana 😘 *Masoud Kipanya*

  • @joycembuya8480
    @joycembuya8480 Рік тому +1

    Salama uu mwanamke jasiri na mwerevu sana
    Big up

  • @stanleymanimo769
    @stanleymanimo769 Рік тому +1

    Wewe ni mtu poa sana masudi

  • @claratemba44
    @claratemba44 Рік тому +2

    Ushauri mzuri sana

  • @mohdapper
    @mohdapper Рік тому +1

    Pride of Africa Masoud kipanya

  • @abuujuhayfa4321
    @abuujuhayfa4321 Рік тому +2

    Mzee wa vipanya 🎉

  • @Calky__-un5qd
    @Calky__-un5qd Рік тому

    Nimependa sana brother Masoud,nimepata kitu❤️🔥

  • @franciskassanga7999
    @franciskassanga7999 Рік тому

    nimeipenda hii, #siyo issue

  • @Marjeby
    @Marjeby Рік тому

    Masoud Kipanya ni akili kubwa sana wallah

  • @Stevematongo
    @Stevematongo Рік тому

    Incredible interview.

  • @tanzaniamycountry9308
    @tanzaniamycountry9308 Рік тому

    Ahaaaa😀😀😀😀😀 salama bhana

  • @queenmaa30
    @queenmaa30 Рік тому

    Kiukweli nimejifunza ktu...elimu nzuri sana

  • @fatmaahamadabass8080
    @fatmaahamadabass8080 Рік тому

    Duh Allah amsameh huyo mtu unafurahiya maradhi ya mwenzio kweli

  • @nurdinkarata7985
    @nurdinkarata7985 Рік тому +1

    🔥🔥🔥

  • @sossyforreal814
    @sossyforreal814 Рік тому

    Masoud is a very smart man aisee.
    Salama sasa tuletee Podcast.

  • @VictorChrispinSamson
    @VictorChrispinSamson Рік тому

    Superb interview, never thought KP atakuwa down to earth like this.

  • @epiphaniaallute2726
    @epiphaniaallute2726 Рік тому

    Asante Kaka Mosoud kuna jambo nimejifunza kupitia maelezo ya Malcom. Barikiwa sana kwa hili.

  • @emilyrenatus9374
    @emilyrenatus9374 Рік тому +1

    Kp 🗽

  • @abdulhamis9825
    @abdulhamis9825 Рік тому +4

    Mwamba Kabsa, Mtu Makin Jamaa Ambaye Sijawah kuchoka Kumsikiliza Na Kujifunza Kutoka Kwake KP

  • @florageofrey9486
    @florageofrey9486 Рік тому

    Nimecheka sana kwakweli

  • @nurdinkarata7985
    @nurdinkarata7985 Рік тому +1

    Logic sister salama 👊🏻

  • @bumbuli4170
    @bumbuli4170 Рік тому +1

    Genius

  • @mwajabujumanne9025
    @mwajabujumanne9025 Рік тому

    Yaan story ya malcom hua lazima nlie pole sana masud😢😢😢

  • @faudhiasalum7279
    @faudhiasalum7279 Рік тому

    ✌️✌️

  • @enockcharles6750
    @enockcharles6750 Рік тому

    nimesubir sana hii yani

  • @nepiasmwasanga1309
    @nepiasmwasanga1309 Рік тому +2

    Kumbe wengine hawapeleki michango SHUBAMIT..😀😀

  • @jacklineabella7634
    @jacklineabella7634 Рік тому +11

    I was waiting for this interview so badly.

  • @philemonpeter8973
    @philemonpeter8973 Рік тому +2

    salama nimependa sana,maswali yako,na jinsi masoud kipanya anavyo jibu,maswali yako,natamani sana kujua jinsi ya kununua hisa

    • @joviangeofrey7212
      @joviangeofrey7212 Рік тому

      Nafikir ni vyema utafute taarifa za makampuni mbalimbali. Kuna muda wanatangaza hiza

  • @abdulhakimmwango9370
    @abdulhakimmwango9370 Рік тому

    Leo ndo umeamua kuiachia si ndio😅😅😅 haya bwana master mind salama

  • @amytullah2175
    @amytullah2175 Рік тому +1

    Hio ya makochi jamani hata mie nilishachanaa😅😅😅😅 daah!! Nilichezea zakufa mtu😅😅😅

  • @albogastmselejr4583
    @albogastmselejr4583 Рік тому +1

    Nilikuwa Naisubiliaa Kwa Muda Hii Interview 🏃🏃

  • @salviusbasil5334
    @salviusbasil5334 Рік тому

    Masoud arudishe ile #MaishaPlus

  • @msafirimiracle6613
    @msafirimiracle6613 Рік тому

    Haya bhana kwa hiyo mmeamua kurudi nyuma miaka,2022 😁

  • @barakawiseman5073
    @barakawiseman5073 Рік тому +4

    Masudi anamuonekano wa umwakyembe flani ivi

  • @NGUFUSALOMI
    @NGUFUSALOMI Рік тому

    Hilo cheko la Salama

  • @SeekerMaulid
    @SeekerMaulid Рік тому +1

    Sister Salama Leo umecheka sana Jamani :), Huu sio 2022 ni 2023.

    • @godblessmwacha5201
      @godblessmwacha5201 Рік тому

      ni ya muda kweli.. usidhani ni wamekosea. ivi vipindi vingi vya salama ni vya muda.

  • @mohamednaaman188
    @mohamednaaman188 Рік тому +1

    2022 😀

  • @JanethKomba-tv7jy
    @JanethKomba-tv7jy Рік тому

    Jamani tujifunze kupitia interview za ece jay not always tunataka kuona makosa t,ila we need to be strong bhna as broo kp did to handle Malcolm's issues

  • @sangomamourice3539
    @sangomamourice3539 Рік тому

    Akili mingi mno mwamba hasa

  • @hustlaztv2352
    @hustlaztv2352 Рік тому

    Nlijua dr harison 😅

  • @issakitundu617
    @issakitundu617 Рік тому +1

    et huu mwaka gani salama

  • @Jaycollection
    @Jaycollection Рік тому

    Tuna hitaji elimu kwenye hisa

  • @leilaassey1726
    @leilaassey1726 Рік тому

    Kumbe ya kitambo salama 22 tena

  • @richardcastromzena5136
    @richardcastromzena5136 Рік тому

    13:30 😂
    16:10 😂
    19:52
    22:40 kaka imara sana

  • @joviangeofrey7212
    @joviangeofrey7212 Рік тому

    Jaman kuna benk flan ilitaka kuanzishwa nikanunua hisa. Huu mwaka wa kumi sijapewa gawio. Inauma jmn

  • @nicodemusmajani9698
    @nicodemusmajani9698 Рік тому

    huyu #Mzee Hanaga shidah.

  • @barakakusa7606
    @barakakusa7606 Рік тому +3

    Masoud ni mwamba hasa ila nashangaa kwanini kwenye teuzi zinazofanywa wanamsahau, Ana kitu huyu 😂😂😂😂

  • @dansondannytv8111
    @dansondannytv8111 11 місяців тому

    Salama ivi nikifikia level gani ya kimaisha naweza fanyiwa Interview na wewe

  • @allybobsaith
    @allybobsaith Рік тому

    Hakuna mzee asiyejua siku za kuzaliwa watoto wake huyo mzee mjanja sana namkubali sana big up masoud. Huyu jamaa ni mind reader 😂😂😂😂😂

    • @nsanyarasheeed8693
      @nsanyarasheeed8693 Рік тому

      Kubali ukakae watoto 8 utakumbuka siku zao za kuzaliwa kuna sis unakumbuka siku ya kuzaliwa imepita

  • @hamyrhai9957
    @hamyrhai9957 Рік тому

    Kipanya

  • @mr.theoswahiliteacher.
    @mr.theoswahiliteacher. Рік тому

    Watu wawili wenye IQ kubwa wamekutana.

  • @godblessmwacha5201
    @godblessmwacha5201 Рік тому +1

    kumbe ni ya mwaka 2022? Dah

  • @mactongathe179
    @mactongathe179 Рік тому

    Apo kweny family dah nmechKaaa saNaa Brooo kipaNya! Birthday na hio namba yao Dah! But ....

  • @godfreymiho4927
    @godfreymiho4927 Рік тому

    Making sana,jamaa alinifany nipend kuchor

  • @romes-tz7323
    @romes-tz7323 Рік тому +2

    Mwamba wamda marefu like kwake👊

  • @Yusufu940
    @Yusufu940 Рік тому

    Salma ume una ma swali 😮

  • @abdulnaseermrisho4342
    @abdulnaseermrisho4342 Рік тому +3

    😂😂😂😂 Masoudy kama Masoudy

  • @dengahmediatz1230
    @dengahmediatz1230 Рік тому

    Tunatak interview yak salama

    • @famymbirore2756
      @famymbirore2756 Рік тому

      Yan apatikane mtu wa kumuhoji vizuri kama yeye anavyowahoji wengine

  • @peterkichochi7510
    @peterkichochi7510 Рік тому

    Miaka imeridi nyuma mwaka 2022😂😂😂😂

    • @nzumbimasanja
      @nzumbimasanja Рік тому

      Wanarekodi kisha wanapandisha muda wowote. Hii ni ya zamani

  • @Hashdough
    @Hashdough Рік тому

    OPENING YA KIBABE KABISA

  • @joesimba
    @joesimba Рік тому +1

    17:00 hizi interview nyingine zilifanyika mwaka jana nini.

    • @brightvatta284
      @brightvatta284 Рік тому

      Yawezekana naona pia mtangazaji kasema 2022

  • @philomenamushi5606
    @philomenamushi5606 Рік тому +7

    🤔😂salama hii ni 2022😓🤔realy😳👀😳hii ni 2023 tafadhali✋🏿

    • @highmanjerry9640
      @highmanjerry9640 Рік тому +5

      Kipindi kilisha recodiwa mzee kama ww ni mfatiliaji kwa tv ungesha jua,humu kwa youtube huwa wanaweka baada ya kuonekana kwa tv kwhyo walio kosa show kwa tv basi utakutana nayo huku

    • @charlesolomi9514
      @charlesolomi9514 Рік тому +1

      Interview yooteee umeona hilo kosa tu

  • @godsonmunisi7229
    @godsonmunisi7229 Рік тому

    Interview was badly .salama anakuuliza swali .but swali halijibu anatoa maelezo mengi sana nje ya swali.

  • @godsonmunisi7229
    @godsonmunisi7229 Рік тому

    I know you was want to act like genius. But wasn't what happens like you was wish .try to listen question carefully before answering questions

    • @frankkajoba8372
      @frankkajoba8372 7 днів тому

      Tatizo kujifanya "much know" kiingereza gani hicho sasa wewe chizi? Hujui chochote kipindi kama hiki hakikufai kasikilize singeli ndio saizi yako.

  • @blandinamyinga9489
    @blandinamyinga9489 Рік тому

    ""anivesari""???🤣🤣🤣🤣🤣@masoudkipanya🙌🙌🙌🙌