Salama Na ALLYBEE SE6 EP72| KULE NI KULE... PART 1 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460

Поділитися
Вставка
  • Опубліковано 18 чер 2023
  • #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
    Kwenye jiji la ‘Maraha’ hapa nyumbani kwetu Tanzania ambayo kwa miaka ya hivi karibuni sehemu za starehe zimekua tele na kila mmoja ana uwezo wa kula bata zake vizuri tu kulingana na urefu wa mfuko wake basi hakuna ambaye HAJUI jina la DJ huyu mahiri ambaye kwa ubunifu wake ameweza sana kubadilisha kabisa jinsi ambavyo wenzake walomtangulia walikua wanafanya. Yaani Ally alikichukua kitabu cha jinsi ya kutoa burudani kama DJ na kukichanachana na kisha akaanza kuandika cha kwake, ambacho mpaka tunaenda mtamboni kiiila msomaji wake anapeeenda ambayo yameandikwa na ambayo anaendelea kuyaandika.
    Wakati msimu huu unaanza Ally Bee hakua moja ya majina ambayo yalikua yameandikwa kama mmoja ya watu ambao tungependa kujua story ya maisha yake, kutaka kujua nini kinampa hamasa ya kufanya ambacho anafanya na pengine mambo mengine tele ambayo atakua na uhuru wa ku share na sisi. Ila kuna siku nilikua nyumbani na Rafiki yangu ambaye pia ni mdogo wangu Ndugu Sadam Almando Sanare ambaye nilikua namuuliza maswali kuhusu Dj mwengine kabisa huku nikilalamika kuhusu huyo mtu kwamba pengine kuna jambo haliko sawa kuhusu simulizi zake za baadhi ya mambo maana amekua kama anaongelea sana skuizi, then yeye akaniambia kuhusu Ally Bee (binafsi hupenda kumuita Ally Bee kwasababu wote tunamjua nyuki, na ukali wake lakini asali yake sote ndo kama hivyo, hopefully it will make sense kwake someday 😄). So wakati ananiambia nami tayari nilikua nishamuona, basi mengine yakaendelea kwenye meza yetu adhimu.
    Story ya maisha yake Ndugu yetu huyu ni ya mateso mengi sana, ila kwa sasa na hata pengine mwanzo kwa adha zote hizo tunamshukuru Allah kwa hayo yote maana hayo ndo yameleta hasira za yeye kutaka zaidi, kuomba zaidi na kufanyia kazi zaidi yote ambayo anayo leo. Ally anakumbuka jinsi alivyofika Dar es Salaam mara ya kwanza na pia amenihadithia adha ya kutokua na sehemu ya kukaa hasa unapokua umekuja mjini mara ya kwanza. Alinifanya nijiulize maswali mengi sana mimi kama binadamu wa kawaida kabisa, au ambaye Mwenyezi kanibariki kwa mengi zaidi ya wengine, nini nafanya kuwasaidia ambao nawaona barabarani? Au ambao hawana uwezo wa kunifikia lakini wana uhitaji? Kanifundisha kuhusu kutochukulia maisha au nafasi ambazo tunazo kwenye maisha yetu kwamba ni kawaida tu. Ki ukweli kila ambacho tunacho kwenye maisha yetu TUNA KILA SABABU YA KUMSHUKURU AMBAYE AMETUPA. Ila pia inabidi mara moja moja tujipigie makofi kwa mbali ambapo tumetoka na ambapo tumefika lakini zaidi tumuombe Mwenyezi Mungu azidi kutuimarisha na kutufungulia milango ya Kheri, ZAIDI.
    Niamini mimi nikikuambia kuhusu kutoa, kwamba kutoa ni raha zaidi kuliko kupokea ingawa wengi wetu tunapenda zaidi kupokea, ukitaka kujua hilo jaribu kwa kuanza kumpa hata mtu zawadi ndogo tu, hata pipi ambayo alikua hategemei kama utampa au utakumbuka, sura yake itakueleza mengi hata kama yeye ataamua asikuambie kwasababu zake zozote tu. Ally alisaidiwa na mtu ambaye hata walikua hawafahamiani na kuamua kumpa hifadhi katika sehemu ambayo yeye alikua anakaa. Pengine yeye alipofanya wala hakujua kama Ndugu Ally atakuja kuwa mmoja wa ma DJ HODARI na Hyper Man bora ambae nchi hii imewahi kuona.
    Leo ningependa tujifunze kuhusu hilo, kuhusu kuwa kind, kuhusu kuwapa watu nafasi kwenye maisha yetu na kutosubiri malipo kutoka kwao maana pengine yanaweza yasije lakini wewe tayari unakua ushamaliza kazi yako.
    Yangu matumaini story ya DJ Ally Bee itakua na impact kwenye maisha yako kama ambavyo imekua kwenye maisha yangu.
    Enjoy and stay BLESSED.
    Love,
    Salama.
    Support us through anchor.fm/yahstonetown/support
    SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahStoneTownSubs
    Listen our Podcast on
    Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
    ‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
    GooglePodcast Link bit.ly/GooglePodcastSalamaNa
    Audiomack Link bit.ly/YahStoneTownAudioMack
    ‪UA-cam Link bit.ly/UA-camSalamaNa
    Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
    Follow:
    Twitter: / yahstonetown
    Instagram: / yahstonetown
    Facebook: / yahstonetown
    Channel Administered by Slide Digital
    Instagram: slidedigitaltz
  • Розваги

КОМЕНТАРІ • 93

  • @RoolkayDrakedrizy-fg9sc
    @RoolkayDrakedrizy-fg9sc Рік тому +12

    Hii interview ina kupa moyo kwenye kupambana na kuamini unacho kiamini 👊✊

  • @salmanyangasa1171
    @salmanyangasa1171 Рік тому +10

    Dah!! Huyu jamaa anaongea ya maana Sana na anaonekana ni mwenye heshma na utu tofauti na umuoneakano wake katika kazi yake! MUNGU AKUBARIKI SANA bro

  • @lastsimbatv1497
    @lastsimbatv1497 Рік тому +8

    Natamanii ujihoji ww salama tujue lifestyle yakoo

  • @rhodajackson2213
    @rhodajackson2213 Рік тому +6

    Sahihi kabisa , naweza toa ushuhuda Kaka ! Wazazi ni kila kitu, R.I.P Mama

  • @g2c477
    @g2c477 Рік тому +21

    A very big fan of Salama na... From Nairobi.
    Had waited for this interview, finally I get a chance to watch this East African Star.
    I watch this show with my Tanzanian wife as well huku Pia nikijifunza Kiswahili sanifu kwenye hii show sanaaaaaa tena mno.
    Salama you're a legendary interviewer, a big fan!🔥!

    • @alijafar9098
      @alijafar9098 Рік тому +1

      Me too...Salama is just awesome! Mob love from 🇰🇪

  • @kisianganijob1068
    @kisianganijob1068 11 місяців тому +4

    Very inspiring indeed. As a human being we ain't limited at all.

  • @esterdoriye8377
    @esterdoriye8377 Рік тому +3

    Ana lafudhi na swaga za chuga/moshi

  • @aldegondejanuary5228
    @aldegondejanuary5228 Рік тому +4

    🔥🔥🔥namkubalii huyu kaka history yake huwa inanipaa nguvu

  • @zumbeshauri8114
    @zumbeshauri8114 Рік тому +5

    Allyb afadhari wewe ni lafiki alikukataa mimi ndugu yangu kabisa ndio alinitolea mbavuni

  • @saumusalimuhassan2499
    @saumusalimuhassan2499 Рік тому +3

    Mashallah, umeongea point brother.

  • @ukhutfatumah1154
    @ukhutfatumah1154 10 місяців тому +1

    Mama mzaramo baba mpare umenisha sna mwanang

  • @user-fh8fv9dz2b
    @user-fh8fv9dz2b Рік тому +5

    Daah!! Ur very humble bro ally

  • @mickthomas-lh1fs
    @mickthomas-lh1fs Рік тому +1

    Athumani tajiri umetisha sana bonge moja la yastone town.

  • @lastsimbatv1497
    @lastsimbatv1497 Рік тому +3

    Salam umeua san namkubar san huyu jamaa kwer hvi vinatokea ila binfsi siwez kuleta dem ghet nkiwa na mshikajii siweziii kbsaa

  • @moseshebrews9089
    @moseshebrews9089 Рік тому +3

    YahstoneTown is a true classroom

  • @rahmaawadh1695
    @rahmaawadh1695 Рік тому +5

    Umeongea point nimeipenda kua kuna fadhira kubwa pindi sana kwa wazazi pindi unawafanyia mema

  • @bakarilimachinga6193
    @bakarilimachinga6193 Рік тому +5

    Daah yaan hii interview imenifundisha nijuwe kuwa bongo usione watu wametoboa kuna miziki nyuma watu wanapitia hatarii 😅😂😂😂😂

  • @parfaitkalemela8733
    @parfaitkalemela8733 Рік тому +6

    Salam when u will invite Harmonize I will appreciate

  • @ibrahimurichard377
    @ibrahimurichard377 Рік тому +3

    Very inspiring
    Salama tunaomba part 2 isikawie

  • @tiffanymo9453
    @tiffanymo9453 Рік тому +4

    Big up to you salama,and Am so proud of you Ally B keep it up bro.😍

  • @hudehude7501
    @hudehude7501 Рік тому +2

    Kichaa ndani ya nyumba

  • @GivenTobago
    @GivenTobago Рік тому +3

    Ali B ni mjasiri

  • @360newssource3
    @360newssource3 Рік тому +8

    Show love to Salama from +254🇰🇪

  • @podahsalim2296
    @podahsalim2296 Рік тому +3

    Nasemajee!! Nasemajeee😂😂

  • @rashidaliy5635
    @rashidaliy5635 Рік тому +2

    Nasemajeee kula nyama nyamaza ww✌️

  • @MkenyaN
    @MkenyaN Рік тому +1

    17:25 hapo kweli kabisa. Story of my life

  • @user-jc7mi4nf4i
    @user-jc7mi4nf4i Рік тому +2

    salama Queen interviewer

  • @OMANOman-qc1lm
    @OMANOman-qc1lm Рік тому +2

    siku zote tharau mbaya ukisha pata shida ndo binadam unarud chini na kujifunza umejifunza kuheshim watu sasa hivi sasa umekua na heshima vizur nitham ndo kila kitu ukiwa maskini au tajir heshima ndo kila kitu

  • @bainolatino3412
    @bainolatino3412 11 місяців тому +1

    Pesa nyingi
    Kelele kidogo

  • @Views-mf8ir
    @Views-mf8ir Рік тому +1

    Wakazie ivo ivo mtu wangu ..

  • @user-zt7de9hv5k
    @user-zt7de9hv5k Рік тому +2

    Kaka 😂😂 appendix umetisha unatengenza box za nyaja

  • @rajabyahya8942
    @rajabyahya8942 Рік тому +2

    First to comment

  • @shaffycjg536
    @shaffycjg536 Рік тому +2

    Nimesubir sana atimae asuman

  • @johnriwa2854
    @johnriwa2854 11 місяців тому

    Asumanii, Salama pure talents

  • @Yanga_tv
    @Yanga_tv Рік тому +1

    Msasani home 🏠 welcome again brother

  • @Goshithedon95
    @Goshithedon95 Рік тому +4

    This is the reality show i loved the most apart from lil ommy podcast
    #big up da salama

  • @mosesmaryz3535
    @mosesmaryz3535 Рік тому +2

    Second to comment

  • @godfreymiho4927
    @godfreymiho4927 Рік тому +1

    🔥🔥✨🎵🎶

  • @rashdiyange7758
    @rashdiyange7758 Рік тому +3

    Mie nacho mpendea uyu jamaa nimsafi mpaka laha bigup baba sumaniiiiiiiii🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣👊👊👊👊👊👊

  • @faudhiasalum7279
    @faudhiasalum7279 Рік тому +1

    Asuman💃👌🏽

  • @user-zt7de9hv5k
    @user-zt7de9hv5k Рік тому +1

    Nyanya

  • @muzafarsharif9465
    @muzafarsharif9465 Рік тому +1

    salama I luv u ❤

  • @suleshbinmkoba1194
    @suleshbinmkoba1194 Рік тому +1

    Big up broo😍

  • @cooler3263
    @cooler3263 Рік тому

    Nakubali sana

  • @whizzycindy1476
    @whizzycindy1476 Рік тому +1

    Tunaomba next awe wema sepetu jmn

  • @mbwanadavid4371
    @mbwanadavid4371 Рік тому +2

    Mimi Ni shabiki mkubwa wa Salama tangu enzi za mkasi mpaka Sasa Salama na... Kama unasoma comments za sisi mashabiki zako mbona hatuoni feedback coz nilieomba tangu kipindi kilipokua pale EATV. Naomba umlete ALI CHOKI mzee wa Farasi pliz🙏🙏🙏

  • @mnyamwezijuma1140
    @mnyamwezijuma1140 Рік тому +3

    Asumoney. 😅 asumaniiii 😅😂

  • @ukhutfatumah1154
    @ukhutfatumah1154 10 місяців тому

    Auna baya DJ ALLYB PAMBANA BABA UMEASO SNA MUDA WAKO HUUU TUMIA BABA

  • @lucasezekiel9782
    @lucasezekiel9782 Рік тому

    💛💛💛

  • @vonniemarry2680
    @vonniemarry2680 Рік тому +1

    The guy is being really

  • @rasjamal9854
    @rasjamal9854 Рік тому +1

    ❤👊👊

  • @abuuarushadawg7158
    @abuuarushadawg7158 8 місяців тому

    He used to be big in Arusha back in th days

  • @ezekielhamis887
    @ezekielhamis887 Рік тому +2

    Wanangu wa tpc

  • @daggerslick
    @daggerslick Рік тому +22

    Wakwanza likes zanguu😊😢

  • @TheUraniumz
    @TheUraniumz Рік тому

    Ally B 🙏

  • @goodlucktemu3149
    @goodlucktemu3149 4 місяці тому

    uyu ameiedit ii story nsikilize mimi, Aliyefanikiwa awezi kukupa full story yake.

  • @najmaahmed3840
    @najmaahmed3840 Рік тому +1

    Allyy b

  • @abbashussein-hz4dr
    @abbashussein-hz4dr Рік тому +2

    Jamaa tumesoma shule moja mawenzi primary school pale stand ya bus tunatazamana darsa moja alikua anatuita fidodido tuko mapacha hasan na husen mafidodido ndo majina yetu dah mwamba km unanikumbuka big up sana unamkumbuka mwalimu nkya 😂😂😂😂

  • @vonniemarry2680
    @vonniemarry2680 Рік тому +2

    🙌🙌🙌🙌🙌🙌🙌

  • @MultiKelvin1994
    @MultiKelvin1994 Рік тому +1

    14:49😅

  • @MusaMargwe-ol9iu
    @MusaMargwe-ol9iu 11 місяців тому

    Umegundua nn hapo huyo msela ni Mchugastan

  • @sofiaissamkandama2742
    @sofiaissamkandama2742 Рік тому +4

    Kula nyama nyamaza kuna kitu anatuficha kuhusu mafanikio yake

  • @ashurashabani7249
    @ashurashabani7249 Рік тому +1

    Athumaniiiii😊😅🤗

  • @user-ou4nx5om2o
    @user-ou4nx5om2o 11 місяців тому

    We ni ally Kurwa Kama sikosei

  • @winfridangoloke1916
    @winfridangoloke1916 11 місяців тому

    Bwana said kokote uliko nakuaalimu😂😂😂😂😂😂😂

  • @asyafatma532
    @asyafatma532 Рік тому +1

    😂😂😂😂😂😂😂

  • @Boaz22
    @Boaz22 Рік тому +1

    Kuji adjusti adjusti ndo nini, watangazaji kuchanganya kiingereza na kiswahili inakera hamjui tuu..mara inspiration yako,mxiewwwww

    • @joycemfuru4752
      @joycemfuru4752 Рік тому +1

      Wivu tu na shida zinakusumbua kalale hukoo

  • @zagadat1129
    @zagadat1129 Рік тому +2

    Ivi 2010 boda boda zilikuwepo??

    • @sophishebby6274
      @sophishebby6274 Рік тому

      Yah boda zilianza 2007

    • @masalakulwa7601
      @masalakulwa7601 Рік тому

      Yap

    • @rizikiabdalla2501
      @rizikiabdalla2501 Рік тому

      Zilikuwepo my mm mwenye nilikuwa na boda boda wangu nikiumwa ananipeleka hospital nikiwa dodoma ila ndioo nilikuwa zinaaazaaaa

  • @fahadfahmy
    @fahadfahmy 11 місяців тому

    Inasikitisha Mzee wako ni Imamu na wewe umeangukia kua Dj

  • @abedomar5183
    @abedomar5183 Рік тому +1

    Huyu Dj nae mbembwe nyingi Hana lolote anaongea sana

  • @user-zt7de9hv5k
    @user-zt7de9hv5k Рік тому +1

    Nyanya

  • @ecostats51
    @ecostats51 Рік тому +1

    Nasemaje, kula nyama nyamaza. 😂😂😂👏👏

  • @user-zt7de9hv5k
    @user-zt7de9hv5k Рік тому +1

    Nyanya