Salama Na SAMATTA SE6 EP49 | HEADMASTER PART 1 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460

Поділитися
Вставка
  • Опубліковано 9 лют 2025
  • #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
    Kila kijana wa ki Tanzania ambae anaupenda na kuuthamini mpira wa miguu na ambaye angependa ndo iwe kazi ya maisha yake basi Mbwana Ally Samatta ndiye role model wake, hakuna doubt kwamba watakua na mapenzi na Cristiano Ronaldo au Leo Messi au Kylian Mbappe au Marcus Rashford ila yule ambaye amewaaminisha kwamba INAWEZEKANA ukacheza POPOTE hapa duniani na hasa kwenye ligi yetu pendwa ya Uingereza ni Samatta. Rafiki tu kutoka Mbagala rangi tatu ambaye kashacheza saaana ndondo na makombe ya mbuzi wakati anakua na mwisho wa siku akaenda kucheza kwa wazungu na bado anaendelea kutafuta rizki yake huko, hata kama sio ligi ile ambayo hata yeye mwenyewe angependa awepo ila BADO ni MWAMBA wetu. Samatta huyu huyu ndo ambaye alijitwika mpira kichwani na kuitika nyavuni mbele ya beki ambae anaaminika kuwa BORA kwa misimu hii miwili mitatu ndani ya Virgil van Dijk. Hata wakati naandika hii bado mwili unanisisimka kwa wazo tu kwamba nililishuhudia lile, pata picha kwa mtoto ambaye ana ndoto hizo. Lile goli lilimfanyia NINI kwenye ndoto zake. KRC Genk walipoteza mchezo ule wa ugenini wa kombe la mabingwa wa Ulaya kwa magoli 2-1 ila kwenye mitaa yote ya mikoa ya Tanzania ile mechi ilikua ya USHINDI.
    Mbwana ametokea kwenye familia ya kawaida sana sana, wazazi wake wote kama kumbukumbu yangu itakua 100 basi walikua polisi, najua kwa hakika Baba yake alikua Polisi kwa asilimia 100. Kwa marehemu Bi Mkubwa wake ndo sina hakika sana ila kwa hakika jibu limo kwenye haya maongezi yetu. Anakumbuka jinsi ambavyo Mzee wake alikua anasisitiza kwenye suala la elimu na heshima, kama mtoto wa mwisho kwenye familia hiyo, Mbwana aliupenda sana mpira, zile za kujiiba na kwenda kucheza mechi za mbali alishafanya sana na matunda ndo haya ya leo. Nadhani ilifika kipindi Mzee mwenyewe aliona basi sawa, twende huko utakako. Familia yao yote ni wapenzi wa mpira na Kaka yake Mouhamed bado anacheza hapa hapa Tanzania. Sasa akiwa kama kioo kikubwa sana kwenye jamii hii Samatta anazungumzia presha ambayo hupewa hasa pale anapoitwa kwenye timu ya Taifa, jinsi maneno mengi ya kashfa yanaporushwa kwake kutoka kwa wananchi na anakumbuka pia wakati bado anacheza T.P Mazembe kuna kipindi kocha aliacha kumuita yeye na Rafiki yake Thomas Ulimwenguna ilisemekana kama pengine hakuna na interest na team au hakua anatoa 100. Pengine kipindi hicho aliumia zaidi maana hiyo haikua jambo zuri kwake.
    Mbwana anazungumza na mimi kuhusu urafiki wake na Ulimwengu na maisha ambayo walikua wanaishi pamoja wakati wako DRC, anakumbuka jinsi walivyokua wanapanga kufanikiwa pamoja na mipango yao endelevu kwenye career yao. Ulimwengu nae ana siku yake kwenye kiti chetu In Shaa Allah maana nae ana mengi ya kutuelezea. Majeraha ya mara kwa mara bila ya shaka yalisababisha kwa kiasi kikubwa ndoto zake za kucheza Ulaya kutochukua hatua ya juu kama ambavyo angependa, ila mimi naamini hayo yote maisha tu, kila kitu kilikua tayari kimesha andikwa.
    Samatta ni Baba ambaye watoto wake wanasoma hapa hapa nyumbani, nilimuuliza kama watoto wake wanajua yeye ni nani na akanipa story ndogo ya yeye kung’amua kama wanafahamu fika Baba yao ni nani.
    Mwenzangu humu kuna mengi sana ambayo yatakufaa na kwa nafasi ya kipekee ningependa kumshukuru Captain wa Taifa kwa kuchukua time kwenye ratiba yake ambayo ilikua imebana kweli kweli ili tu aje kutubarikia meza yetu kwa uwepo wake.
    Yangu matumaini uta enjoy sana.
    Love,
    Salama.
    Support us through anchor.fm/yahs...
    SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
    Listen our Podcast on
    Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm‬
    ‪ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru‬
    GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
    Audiomack Link bit.ly/YahSton...
    ‪UA-cam Link bit.ly/UA-camS...
    Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
    Follow:
    Twitter: / yahstonetown
    Instagram: / yahstonetown
    Facebook: / yahstonetown
    Channel Administered by Slide Digital
    Instagram: slidedigitaltz

КОМЕНТАРІ • 135

  • @Jibambeshow254k
    @Jibambeshow254k Рік тому +4

    Santa very humble and peaceful guy naona ananyayo kama za Ali hana mbwembwe and that's why he's unique ❤hii sampuli ndio kio cha jamii

  • @samniza1763
    @samniza1763 2 роки тому +13

    The first ever sensible young Tanzanian born and raised in Tanzania. Proud of who you have become.

    • @JJ-sx7ne
      @JJ-sx7ne 2 роки тому

      Labda wewe kingereza hakipo kabisa! 98% kaongea kiswahili..

  • @chiconinde8135
    @chiconinde8135 2 роки тому +9

    Baada ile ya Jakaya....Hii tena umefanya kubwa Salama🙌⚽️💪

  • @rashidchimwenda
    @rashidchimwenda 2 роки тому +3

    Big up kwa Salama kuweza kutuletea Samatta. Anaongea mambo mengi mazuri ya mfano kwa vijana wetu kwa soka letu.
    Ila suala la maadili sikubaliani naye aliposema ni yeye mwenyewe. Bila shaka maadili yake mazuri yamejengwa ktk familia yao (baba na mama) na hususan kwakuwa ni familia ya kipolisi, timu alizopitia hapa bongo na tamaduni zetu za kitanzania. Sisi watanzania tupo vizuri kimaadili kuliko baadhi ya watu wa mataifa mengi.
    Kila la heri kwake na Salama.

  • @arafajabir3194
    @arafajabir3194 2 роки тому +14

    Mungu amempa uwezo ila hapendi show off anaishi kama Ali kiba good bless you

  • @stevewanga957
    @stevewanga957 2 роки тому +11

    Hes very humble like Ali Kiba...much love from🇶🇦🇶🇦

  • @sawaabyahya584
    @sawaabyahya584 2 роки тому +1

    Huyu mwanamme mbona best baba! Ni kioo cha jamii..... Vijana wajifunze kupitia tabia yake.... Ahsante Salama kumtafuta...

  • @mbwanamtessa8607
    @mbwanamtessa8607 2 роки тому +41

    Kama bado unamkubali huyu jamaa gonga like twenzetu

  • @tatutumbi4640
    @tatutumbi4640 2 роки тому +2

    Salama Hongera Sana. Nafatilia Sana Vipindi Vyako. Navipenda. 👍

  • @hanssenbensonmturi2435
    @hanssenbensonmturi2435 2 роки тому +14

    Ulivofanya interview na Idris, nilitamani ufanye na Samatta as well. Nilivyoona hii leo, ilinikosha sana kwani Samatta ni nguli na role model to a lot of us young footballers. I am currently playing my football in The Thailand 3rd division and I dream one day not only to replicate the legend’s work but also I dream of being part of this show. Thank you Salama and Samatta for this wonderful interview

    • @Chemba67
      @Chemba67 2 роки тому

      Keep it up Hanssen Benson.......your name sound Danish.......

    • @allahisone6386
      @allahisone6386 2 роки тому +1

      @Hanssen God bless you ❤️🙏❤️

  • @shwaibukhatibu2838
    @shwaibukhatibu2838 2 роки тому +2

    SAMATA NA KING KIBA
    ALLAH BLESS YOU OTHER CELEBRITIES THEY HAVE TO COPE FROM YOU

  • @maishakisunzu391
    @maishakisunzu391 2 роки тому +6

    Kama umegundua lafudhi ya samatta ishabadilika automatically kuwa ya kiingereza gonga like hapa😝

    • @navigatorelias9794
      @navigatorelias9794 Рік тому

      Wewe acha zako babu, Asa si lazima hiyo hata wwe ukitoka kwenu huko dongo kusimamia ukija mjini lazima kiswahili chako kibadilike, so sielewi unataka kumaanisha nn

  • @com5766
    @com5766 2 роки тому +12

    The best interview
    Hey kenyans give likes for it

  • @RehemaChap3
    @RehemaChap3 Рік тому

    Samanta MUNGU akubariki sana una busara sana

  • @luciasteven3314
    @luciasteven3314 Рік тому

    Nimechelewa sn kumjua samatta❤

  • @mussachabonga9595
    @mussachabonga9595 2 роки тому +5

    Fantastic interview big up sister Salama 2023

  • @peterkichochi7510
    @peterkichochi7510 2 роки тому +9

    This Guy is very humble and smart, he knows how to communicate

    • @ahmedjaffari9375
      @ahmedjaffari9375 2 роки тому

      Exactly… he is truly a professional footballer, may Almighty Allah bless him abundantly 🙏🏿

  • @erickchitumbi1308
    @erickchitumbi1308 2 роки тому +1

    Mbwana unayo hekima na busara sana.safi sana.

  • @majomamajoma8776
    @majomamajoma8776 2 роки тому +5

    Nina mwanangu anakupenda na anacheza mpila hatari Huwa anajiita samata, sapoti wanetu vijijin kaka nao watimize ndoto zao Allah akufanyie wepesi uzidi kung'ara

  • @januarysungura8119
    @januarysungura8119 Рік тому

    Your the best not just of luck but you deserve it keep up samatta

  • @homan_nkwama
    @homan_nkwama 2 роки тому

    kama baadhi ya majibu yanatakiwa Sana ili kutimiza mahojiano ni sawa ila kama sivyo, naomba salama punguza kujenga MASWALI yanayo mlazimu mtu ajibu katika mtazamo fulani.....awe huru tusitarajie atajibu nini I LOVE YOU SALAMA

  • @nomamatata754
    @nomamatata754 2 роки тому +2

    I keep saying salama you got best questions for your guests.....you keep asking my questions every time i get time to see your sessions.....be blessed girl

  • @deospackle2158
    @deospackle2158 2 роки тому +5

    Samatta anasound humble sana🔥🔥🔥

  • @albogastmselejr4583
    @albogastmselejr4583 2 роки тому +5

    Aiseh! Jamaa Mbona Haongei Kingereza Kama Mimi Wakati Mimi Nimekaa Week Tu Nime Sahau Kiswahili 😁😁

    • @jackbujimu3220
      @jackbujimu3220 2 роки тому

      🤣🤣🤣🤣 mie nimesoma tu English medium primary Ila mpka Sasa ninachanganya ngeli Kama nimeish mambele

  • @mweusiasili8345
    @mweusiasili8345 2 роки тому +2

    Capten Diego

  • @RajabuKibik
    @RajabuKibik Рік тому

    Uyu yomuli Dar Es Salaam Tz 🇹🇿🇹🇿🇹🇿🇹🇿

  • @mofungoya9729
    @mofungoya9729 2 роки тому +2

    Best player ever ♥️🇹🇿

  • @bish_daddiyao
    @bish_daddiyao 2 роки тому +2

    Mimi mkenya Ila Huyu Jamaa namkubali🙌🏾⚽♥️⚽

  • @dullayomwinyi3359
    @dullayomwinyi3359 Рік тому

    Mwamba huyu ni hatari sana

  • @marwajuma7493
    @marwajuma7493 2 роки тому

    Nilisubili Sanaa asante sanaa

  • @mountaincoffee7
    @mountaincoffee7 2 роки тому +1

    Noma sana

  • @dseven7094
    @dseven7094 2 роки тому +2

    mbagala boy

  • @Revo_silayo
    @Revo_silayo 2 роки тому

    Hyo ni nature ya intruvant peoples Huwa wanakuwa na rafiki wachche lkn wanapendwa na wengi na Huwa wanajifanyia maamuzi wenyewe na pia wapo focused na hutoboaa sanaaa.

  • @safiyatheonlything7848
    @safiyatheonlything7848 2 роки тому +2

    leo salama na samata

  • @aaronswai3092
    @aaronswai3092 2 місяці тому

    Kauli nyepesi ni kwamba Mungu alimpa neema ya unyenyelevu huyu dogo

  • @mwasagamwambuli3513
    @mwasagamwambuli3513 2 роки тому +1

    Mbwana you are what your father and mother groomed you to be what you are. Be appreciative of your parents

  • @hansigajijime4108
    @hansigajijime4108 2 роки тому +1

    Mwamba kabsa

  • @jojigeorige1056
    @jojigeorige1056 2 роки тому +1

    He's well programmed aisee

  • @flavianchuwa4370
    @flavianchuwa4370 2 роки тому +3

    Waaaaoooh Asante kwa hii Salama

  • @moganfred6473
    @moganfred6473 2 роки тому +1

    Nakkubali sana

  • @daggerslick
    @daggerslick 2 роки тому +1

    Woyoooo mbwana samatta😜😜😜

  • @xnobmedia1
    @xnobmedia1 2 роки тому

    Dah Salama kwa kumleta salama umenitouch saaaana yan. Hebu pokea 10k la soda hapooo.

  • @rosemofuga8101
    @rosemofuga8101 2 роки тому

    Waoooooo fantastic mr Samatta

  • @mr.graphics3213
    @mr.graphics3213 2 роки тому +1

    Tz oneeee🔥🔥🔥🔥

  • @aishaomarry6996
    @aishaomarry6996 2 роки тому +2

    Huyu ni mimi kabisa hua naamua mwenyewe mambo yangu.

    • @tztanzania2262
      @tztanzania2262 2 роки тому

      Usifanye hivyo mara zote jtahd baadhi ya mambo kuomba ushaur

  • @brunofernandez6608
    @brunofernandez6608 2 роки тому +2

    Samagoal Mbagala Boy

  • @SaidiHassan-pq3zf
    @SaidiHassan-pq3zf 10 місяців тому

    Bless captain Diego

  • @ayubuakko9495
    @ayubuakko9495 2 роки тому

    Salama jabir Ur on 🔥🔥

  • @MariamHamad-lr3xc
    @MariamHamad-lr3xc Рік тому

    Kipendacho moyo dawa

  • @thefeyotz
    @thefeyotz 2 роки тому +1

    Aliifunga Liverpool 😁😁

  • @mrlabay9871
    @mrlabay9871 2 роки тому +4

    🔥🔥🔥🔥

  • @andrewjulius2306
    @andrewjulius2306 2 роки тому

    Sam ✊🔨 keep it up bro unjua

  • @nadildylan6124
    @nadildylan6124 2 роки тому

    Huna Baya bro

  • @robinhomesuza8906
    @robinhomesuza8906 2 роки тому +1

    Naskia sauti ya ommy dimpoz zinafanana

  • @FireHouse123
    @FireHouse123 2 роки тому +2

    Samatta mkali sana namkubali

  • @furahambwembwe6935
    @furahambwembwe6935 2 роки тому

    Humble man...

  • @nadildylan6124
    @nadildylan6124 2 роки тому +2

    Salama tunaomba ufanye interview na nadir haruob canavaro

  • @googleus4903
    @googleus4903 2 роки тому +3

    MWAKINYO ANGEPATA NIDHAMU NA HESHIMA KAMA YA NDUGU NYETU SAMATTA ANGEFIKA ZAIDI YA ALIPO LEO.

    • @tztanzania2262
      @tztanzania2262 2 роки тому

      Mbona na mwakinyo yupo fresh tu!

    • @barbarasara4033
      @barbarasara4033 2 роки тому

      @@tztanzania2262 dharau nyingi

    • @mickidadybakari9974
      @mickidadybakari9974 2 роки тому

      Mwakinyo mtu poa saaana kama utam chukulia poa ila kama ukiwa mduanzi utam hulia mbona ila ni mshikaji saaana tena zaid ya saaana

  • @nadildylan6124
    @nadildylan6124 2 роки тому

    Legend Bro

  • @edwardfaraji1133
    @edwardfaraji1133 2 роки тому

    Sama goal Sama Sama goal....

  • @dmikepresenter
    @dmikepresenter 2 роки тому +2

    Samatta Goal 🇹🇿🇹🇿🇹🇿

  • @dreamfootballclip1096
    @dreamfootballclip1096 2 роки тому +1

    Home boi

  • @kabirigisaidi8253
    @kabirigisaidi8253 2 роки тому +1

    Sama goal Sama goal. You de best bro

  • @hassanikipusa8328
    @hassanikipusa8328 2 роки тому

    Champion Boy 🇹🇿

  • @ibraimoissiaca6058
    @ibraimoissiaca6058 2 роки тому +3

    Popa

  • @abuujuhayfa4321
    @abuujuhayfa4321 2 роки тому +11

    SAMATTA 🔥🔥🔥 gonga like kwa mwamba

  • @jamaalsaleem2926
    @jamaalsaleem2926 2 роки тому +3

    WA kwanza leoooooo

  • @kulwamwakagali24
    @kulwamwakagali24 2 роки тому

    Champs Boy

  • @MariamHamad-lr3xc
    @MariamHamad-lr3xc Рік тому

    Wanasema pesa ni sabuni ya roho

  • @samludo5435
    @samludo5435 2 роки тому +1

    Mlete mandonga salama

    • @henrymassawe699
      @henrymassawe699 Рік тому

      😁🤣🤣🤣🤣😁😁😁😁 hatavuruga interview aiseee!!!🤣🤣

  • @donnietommie8444
    @donnietommie8444 2 роки тому +2

    #SalamaNaDrLeaky

  • @saumusalimuhassan2499
    @saumusalimuhassan2499 2 роки тому

    Laana ya wazazi ndio hiyo mitihani.

  • @pheninhojr5875
    @pheninhojr5875 2 роки тому

    Samagoal #hainakufel

  • @anumario7footballlife936
    @anumario7footballlife936 2 роки тому +2

    Kaka yangu

  • @rehemambilinyi9452
    @rehemambilinyi9452 2 роки тому +1

    Tuletee na pastor Tony kapola,

  • @kanyika14kanyika16
    @kanyika14kanyika16 2 роки тому +3

    SAMATTA anatabia kama zangu😁😁

  • @mdalamgir-gu9hu
    @mdalamgir-gu9hu 2 роки тому

    Yan pia salama leo ujui umulize nn..

  • @gasorekassim5499
    @gasorekassim5499 2 роки тому

    Kizaz san

  • @nahyialetomia9284
    @nahyialetomia9284 2 роки тому

    Nafurahia wewe kujenga msikiti

  • @abdallahmanula1627
    @abdallahmanula1627 2 роки тому +1

    Apo salama umenichanganya kabla amjaaanza nyuma muanze mbele mimi cjakuelewa kabisa

  • @cvanoedward3093
    @cvanoedward3093 2 роки тому

    Salama mbona watukatisha?

  • @albertbayona8441
    @albertbayona8441 2 роки тому +1

    Kwan jaman ilo neno shock mbona watu ulitumia vibaya

    • @Oldskulgemini9991
      @Oldskulgemini9991 2 роки тому +1

      SEMA hata wazungu hutumia Hilo neno mara nyingi Sana so Wala sio ajabu SEMA labda kwakuwa umeona wabongo pekee😅

    • @ahz6907
      @ahz6907 2 роки тому

      Linatakiwa litumikaje?

    • @kamanziian1073
      @kamanziian1073 2 роки тому

      Wewe ndo hulielewi

  • @adamsengo1869
    @adamsengo1869 2 роки тому +5

    Wape points zao wazazi maana wao ndio source ya tabia yako

    • @mashamassingisa8738
      @mashamassingisa8738 2 роки тому +1

      Masikito kua cjasikia hili kutoka kwake

    • @adamsengo1869
      @adamsengo1869 2 роки тому +1

      @@mashamassingisa8738 eti ni yeye tu amejikuta yupo ivo yani kama vile alijikuza mwenyewe, naona kama vile kwa mbali ana katabia cha kujimwambafai flani hivi

    • @mashamassingisa8738
      @mashamassingisa8738 2 роки тому

      Masikitiko makubwa kk

    • @izzi198
      @izzi198 2 роки тому

      angevuta bangi na kuwa teja mngewapa point wazaz wake? Acheni kushinikiza ujinga

    • @mashamassingisa8738
      @mashamassingisa8738 2 роки тому

      @izzi haya kk uko vyema sana

  • @Bam268
    @Bam268 2 роки тому +2

    Apo mnatuchanganya Birmingham ipi sasa ya gwajima au?

  • @kostasagelidis5326
    @kostasagelidis5326 11 місяців тому

    ωχχ ο σαματαςς χαχα

  • @msuyatztv5201
    @msuyatztv5201 2 роки тому

    ua-cam.com/video/bOC1NRBzhQA/v-deo.html
    Ujumbe wa wafanyakazi Kwa Mama samia

  • @nadildylan6124
    @nadildylan6124 2 роки тому

    Bro umetupa funzo kubwa cc vijana, wewe nd mchezaji usie kuwa na wajivuno na nadir haruob Kwa maono yangu

  • @ibrahimshilinde6129
    @ibrahimshilinde6129 2 роки тому

    Kwani wewe Salam,Nani huaga anakushauri kuwakandia vijana wenye talent za mziki?

  • @tutumarzouk9803
    @tutumarzouk9803 2 роки тому +5

    mbona sama goal anajifanya kama hajui kiswahil vzr, yan kama ameish eurupe since he was childhood

    • @mdalamgir-gu9hu
      @mdalamgir-gu9hu 2 роки тому

      Kizungu gan kazumgumza apo izo actualy nyingi..

    • @bryanlimbi326
      @bryanlimbi326 2 роки тому +2

      Sasa he was childhood ndo nini ..!? , Jifunze grammar mbwa wewe

    • @Nimebarikiwa
      @Nimebarikiwa 2 роки тому

      @@bryanlimbi326 ilikua na ulazima wa kumtukana????

    • @noelsanga6853
      @noelsanga6853 2 роки тому +1

      @@Nimebarikiwa wivuuu tu unawasumbua

    • @anoldjefsta177
      @anoldjefsta177 2 роки тому

      @@bryanlimbi326 na aanze kubweka saivi

  • @jilalajr_official
    @jilalajr_official Рік тому +2

    @samagoal77 #diego

  • @baritone_online_tv2565
    @baritone_online_tv2565 2 роки тому

    Noma sana