Safari Sio Kifo Mbaraka Mwinshehe & Orchestre Super Volcano

Поділитися
Вставка
  • Опубліковано 6 вер 2024
  • Old is Gold!

КОМЕНТАРІ • 92

  • @renatuskillo5304
    @renatuskillo5304 5 років тому +15

    Kwangu mimi, Mbaraka Mwinshehe Mwaruka, ndiye Mwanamziki wangu bora kabisa wa muda wote katika maisha yangu. Pumzika kwa Amani mwanamziki wangu. Hakuna atakae ziba pengo lako katika muziki wa Tanzania.

  • @salehborry4547
    @salehborry4547 6 років тому +6

    mungu ampumzishe mahali pema peponi , nguli mbaraka mwishehe , nyimbo zako bado zinaishi japo haupo

  • @maregesifidel3810
    @maregesifidel3810 2 роки тому +3

    Huyu mbaraka ndiye mwanamuziki wangu.nyimbo take zilienda na wakati zijaa mafundisho ,maonyo mafunzo na alijua kwa ustadi kulitumia jukwaaa.Hajapatikana wa kilinganisha.

  • @rudaerisa3721
    @rudaerisa3721 Місяць тому +1

    RIP Mbaraka , the Swahili ambassador

  • @mariamfritsi9761
    @mariamfritsi9761 6 років тому +10

    namkumbuka sana mbaraka alikuwa rafiki wa mume wangu, mwaka 1975 nakumbuka alikuja nyumbani kwetu kututembelea huko korogwe Tanga, ilikuwa usiku akapige mziki korogwe kwenye hall, sasa sauti ilikuwa haitoki alikuwa anaumwa na kifua, basi nikampa asali nakumbuka, baada ya muda akapata nafuu na sauti ilitoka tena.R.I.P.shemeji.14.05.18.

    • @kakimuniafu450
      @kakimuniafu450 5 років тому +2

      Mariam Fritsi, hapo sasa! Ahsanta!

    • @kokombwana5865
      @kokombwana5865 5 років тому +2

      Nakumbuka nyimbo hizi enzi za utoto,miaka hiyo nikiwa Kivesa Handeni,Tanga

    • @obillaezra6205
      @obillaezra6205 2 роки тому

      Kumbe ulipata bahati ya kumuona hata kuongea naye huyu Gwiji, ambapo kwa Historia aliishi Duniani kipindi kifupi sana 34 na miezi kadhaa, lakini hadi Leo Historia yake bado inazungumzwa” Hongera Mama Najua Kwa sasa ushakula chumvi za kutosha” All the best huko Uswisi

    • @gregorydeus72
      @gregorydeus72 2 роки тому

      Marian Fritsi hongera kwa maelezo mazuri, watching August 2022.

  • @ZilipendwaTanzania
    @ZilipendwaTanzania 4 роки тому +4

    Safari siyo kifo huku tulipotoka wote salama,
    Ilikuwa ndefu Sana na tabu nyingi ndiyo kawaida,
    Sijui wenzetu hapa nyumbani Kuna habari gani mezani,
    Twategemea wote hamjambo mwaendelea vyema na kazi zenu.

  • @Eliaskasanya-hm5yk
    @Eliaskasanya-hm5yk Місяць тому

    Angejengewa sanamu pale Msamvu. Anamchango mkubwa sana kwa nyimbo zake. Pamoja na kubrudisha pia zilifundisha

  • @mzuvendi
    @mzuvendi 7 років тому +18

    Mbaraka alikuwa analicharaza gitaa ilibakie litamke maneno! mungu alimjalia kipaji cha kutunga, kuimba, na kutumia vyombo ambavyo wachache wana sifa hizo..RIP warrior bado tunakuenzi!

  • @julithamuhale7271
    @julithamuhale7271 2 роки тому +4

    Ooh! Mbaraka Mwinshehe! Hakika ulitunga nyimbo nzuri na Sauti yako ya zege hakika hata tunaokusikia hatutakusahau kwa burudani ulizotiachia!

  • @khalifasaid7695
    @khalifasaid7695 2 роки тому +1

    Charles Kasembe na rythm ndani

  • @khalifasaid7695
    @khalifasaid7695 2 роки тому +1

    Aliekung'uta gitaa zito la Bass ni Athuman Babu.huyu mchawi sana kwa Bass na Mbaraka alikuwa nae tokea Mororogoro jazz mpaka Super volcano

  • @kcmedia5693
    @kcmedia5693 2 роки тому +5

    It is quite fascinating that the persons who have commented here in one way or another attended one or several shows of the Maestro. I also happen to be one of them, I am lucky to not only attend his shows but also his band rehearsals. I have witnessed how he builds up his songs. When watching him building up a song you would marvel at the way he directs all the other musicians. He also had keen ear even when on stage, he did want anything to go wrong. The only other person whom I know came close to him in playing the solo guitar in the band was Gerard Nangati. Gerard was mostly playing the solo guitar when Mbaraka was not around. It is even said that there was a tag of war between Mbaraka and Morogoro jazz competing in winning over Gerard Nangati that is when Mbaraka had broken away to form Super Volcano. Eventually Morogoro jazz won and took Gerard unfortunately Morogoro jazz did not survive long . Luckily almost all the musicians who had remained with Morogoro jazz formed Orch Lombelombe and moved to Mombasa. Just listen to sisi ni Vijana wa Orchestra Lombelombe to see how close Gerard style and skills in playing the solo guitar was close to that of Mbaraka Mwishehe.

  • @nathanielmbwambo8981
    @nathanielmbwambo8981 Рік тому +1

    Wimbo mzuri hauchuji

  • @khalifasaid7695
    @khalifasaid7695 Рік тому +1

    Athuman Babu pembeni pale akinyukua Bas.

  • @allyzakaria6902
    @allyzakaria6902 Рік тому +1

    Nyimbo hii kila nikitaka kusafiri huikumbuka !

  • @johnontweka1043
    @johnontweka1043 5 років тому +5

    The greatest soloist . Dead took him earlier but his records had & to today they they are so educative. God rest hia soul in his eternal kingdom

  • @hassanbinsalman1437
    @hassanbinsalman1437 6 років тому +12

    I can remember vividly just as if it was yesterday.Those good old days when we were at school.Such talent huwezi kuzipata kwa "muziki" wa kizazi cha sasa.

    • @rahimlipala3000
      @rahimlipala3000 4 роки тому +1

      Ninani alielikung'uta gitaa zito LA bees duuu!!!!

    • @kcmedia5693
      @kcmedia5693 2 роки тому

      @@rahimlipala3000 Ni Charles Ray Kasembe alikuwa mdogo sana (sidhani kama alizidi miaka 16 wakati huo) akitokea TK Lumpopo ya Juma Kilaza nakumbuka tulivyokuwa tukimshangaa akiwa jukwaani

    • @kcmedia5693
      @kcmedia5693 2 роки тому

      @@rahimlipala3000 Samani hapa nilikuwa naelezea aliyepiga rythm guitar

  • @naftalimhemi4163
    @naftalimhemi4163 2 роки тому +1

    Tukitokea Field Mkata Ranch Morogoro tulicheza muziki huu tukijipongeza kwa kurudi salama Mpwapwa Veterinary Institute 1976

  • @slyvesterkameo6847
    @slyvesterkameo6847 6 років тому +12

    Nilibahatika kuhudhuria dansi za Mbaraka Mara 3, 1975, 1976 huko Mpwapwa na 1978 huko Tabora. Nawakumbuka wanamziki Samson Gumbo, Athman Babu, Lazaro na Zully Bonzo, (Hawa baadaye walianzisha Arusha Kurugenzi jazz) ,Zanda na mpiga rhythm mahiri Charles Rey Kasembe..Mbaraka aliweza kupiga gitaa lake kwa kutumia meno take na gitaa likaongea. Hakika alikuwa mchawi wa solo asiyeweza kuelezeka

    • @kakimuniafu450
      @kakimuniafu450 6 років тому +2

      Ndugu Sylvester Kameo, ulibarikiwa sana.

    • @steveswakei9600
      @steveswakei9600 5 років тому +2

      unabahati sana. nlizaliwa 72 na tayari mwaka wa 80 nilikua nimesha mpenda mbaraka nkiwa miaka 8. mie nimekua nikitamani saana nimuone tu hata kwa video moja tu na sijawahi pata kujua ikiwa aliwahi recordi kwenye video.

    • @aliah1732
      @aliah1732 5 років тому +1

      So is me....
      In solo I think on top of Francoo as Fr use to play 2 guitar in many songs ??

    • @peterbayo4677
      @peterbayo4677 4 роки тому +1

      🔥🔥🔥🔥🔥👍👍👍👍 old is gold i was there on earth since 1961 i had 10 when all these zilipendwa are on fire

    • @Ambagaye
      @Ambagaye 3 роки тому +1

      Nikiwa mwanafunzi wa Tabora School, nadhani mwaka 1976 au 1977 alikuja kupiga pale palipokuwa panaitwa Chuo cha Uhazili. Nilikuwa siwezi kulipa kile kiingilio ila nilikuwa najua sana ramani ya ukumbi wa chuo kile, kwa hiyo nikaingilia sehemu ambayo walinzi walikuwa hawajui. Kwa bahati mbaya nikaingia mapema kabla watu hawajaa ujumbini hivyo nikawa target ya walinzi lakini hawakunitoa nje mpaka show ikaisha ndipo mmoja wa walinzi akaniambia "usirudie tena kuingilia madirishani."

  • @khalifasaid7695
    @khalifasaid7695 2 роки тому +1

    Gwiji mpuliza mdomo wa Bata huyo ni Said Makele.ambapo Mbaraka ameingia mdadi na unamsikia anamwita" Gwiji"

  • @Blessedkweli
    @Blessedkweli 6 років тому +8

    Memories are made of this! Thanks Power Nguzo

  • @maregesifidel3810
    @maregesifidel3810 2 роки тому

    Mm ni mshabiki wa nyimbo za mbaraka ingawa nilikuwa mdogo sana wakati anakufa.mungu ampe pumziko la amani mzalendo huyu.Hongerakwa kazi nzuri.

  • @esterpeter7634
    @esterpeter7634 6 років тому +4

    Cool Moods unaambiwa hata Franco alikuwa akimwogopa Mbaraka kwa upigaji wa gitaa la solo huku akiimba kitu ambacho Franco alikuwa hawezi kabisa

  • @nurdinimkasha840
    @nurdinimkasha840 6 років тому +3

    Ama kwa akika mababu zetu wamefaidi sana na sasa nasi twajidai ingawaje wakongwe wa mziki baazi hawapo duniani ira dunia inawakumbuka waishi kwa amani uko wariko

  • @Ambagaye
    @Ambagaye 7 років тому +10

    Katika aliowataja, nilimuona Mbalange mwanzoni mwa miaka ya themanini akiwa karani wa ushuru hapo Morogoro Town Council wakati huo akiwa ameachana kabisa na mambo ya muziki. Power Nguzo! hebu tupe raha sisi wafuasi wako ututafutie mwimbo unaitwa "Tabia Njema ni Silaha" ulitolewa kipindi kimoja na huu. Tafuta ule original sio ule remix ya binti yake Muhtaji Mbaraka

    • @jacksonmulele4033
      @jacksonmulele4033 6 років тому +1

      Mpalanje, alikuwa mbabe kwelikweli, fujo ikitokea ukumbini au getini, lazima atafutwe!

    • @ramadhanimwijage7677
      @ramadhanimwijage7677 3 роки тому

      Mpalange siku hizi limekuwa neno moja la kihuni! Mwenye jina lake akizinduka atashangaa Sana.

    • @Ambagaye
      @Ambagaye 3 роки тому

      @@ramadhanimwijage7677 Hata Kilaza ilikuwa hivyo.

    • @ZilipendwaTanzania
      @ZilipendwaTanzania Рік тому +1

      Huu hapa wimbo wote ua-cam.com/video/m4Kg_rijI7w/v-deo.html

  • @mohammedfarouk8020
    @mohammedfarouk8020 6 років тому +4

    Muniwombeye karibu nitasafiri kurudi uganda

    • @Ambagaye
      @Ambagaye 6 років тому +2

      Safari siyo kifo; utarudi salama!

  • @mussaseif2066
    @mussaseif2066 6 місяців тому +1

    huyu mwamba kaongea

  • @albertokech8168
    @albertokech8168 7 років тому +6

    an excellent composition unlike any other

  • @shulestuff
    @shulestuff 5 років тому +6

    The 1970s !! The golden age of TZ rumba

  • @erichamissi2476
    @erichamissi2476 2 роки тому

    This is the real definition of MUSIC. No doubt about it.... time factor has got no chance to change good thing to bad

  • @salumkyelula443
    @salumkyelula443 Рік тому

    Kweli kabisa safari sio kifo lakini alikuwa anatabiri kifo chake mungu ampe kauri dhabit 😢

  • @alfaniomariandrea2971
    @alfaniomariandrea2971 6 років тому +1

    Kazi nzuri Power Nguzo! Nitafutie wimbo wa Mnzese

  • @AthumaniKimwaga
    @AthumaniKimwaga Рік тому

    Huwezi amini huu wimbo Marijani hakuusikiliza ukiwa ukipigwa hewani umetoka kashakufa

    • @user-ij9jt2wl4d
      @user-ij9jt2wl4d 2 місяці тому

      Sio marijani ni mbaraka mwinshehe halafu hizi nyimbo zimetota 1975 yeye amekufa 1979 kwa hio sio kweli

    • @rudaerisa3721
      @rudaerisa3721 Місяць тому +1

      @@user-ij9jt2wl4d Shida haina ngojangoja ndiyo wimbo aliacha kwa studio.

  • @brownee20007
    @brownee20007 10 місяців тому

    Rythm Charles Kasembe...

  • @Blessedkweli
    @Blessedkweli 6 років тому +2

    Power Nguzo, naomba huu wimbo Tamaa Ya Kuku kama upo nao. Shukran

  • @GEORGEKIBE-j9k
    @GEORGEKIBE-j9k 17 днів тому

    Very good performance

  • @albertokech8168
    @albertokech8168 7 років тому +7

    an excellent composition unlike any other
    as proposed earlier try to get Heshima also called Tabia njema

  • @SindiFRegis
    @SindiFRegis 2 роки тому

    Hi. Asante kwa nyimbo hizi za enzi za kare. Tafadhali nitafutieni wimbo usemao: "Hata ukiwa mlembo wa kupindukia, bila tabia njema watakuchukia..." Nafikiri unaitwa "Tabia njema ni silaha". Asanteni sana.

  • @gerkombo6512
    @gerkombo6512 4 роки тому +1

    Mungu mkubwa tumerudi salama R.I.P

  • @jamestamale6203
    @jamestamale6203 3 роки тому

    Mimi ni mGanda kakin nyimbo za marehemu Mwishehe hazizeiki kamwe. 1979 niki je unga na Minziiro Brigade. Kumbuka Col.Ashimani Wakina

  • @sonialand2646
    @sonialand2646 2 роки тому

    Mie nakumbuka kwetu morogoro tu! Ile morogoro ya zamani

  • @robertsheiza5309
    @robertsheiza5309 5 років тому +2

    Nice composition

  • @sillasngimba5903
    @sillasngimba5903 7 років тому +3

    Lovely song.....

  • @khalifasaid7695
    @khalifasaid7695 2 роки тому

    Kwenye jukwaa mbele unamuona Mbaraka na mpini wake.saidi makelele na mambi idi wakipuliza midomo ya bata. Pembeni athumani Babu anakwaruza bass.Kulwa salum anapuliza pua tembo( saxophone).yani utajiskia tu.

    • @khalifasaid7695
      @khalifasaid7695 2 роки тому

      Bila ya kuwasahau Charles Rey Kasembe kwa Rithm ni mtundu sana.mpalange,issa bendera,kilongola nao ni wachafu sana.

    • @khalifasaid7695
      @khalifasaid7695 2 роки тому

      Sijali, zanda na seniour Bonzo,duh! acha tu.

    • @user-ij9jt2wl4d
      @user-ij9jt2wl4d Рік тому

      Kulwa salum hapo hayupo hapo yupo said athuman makelele na mambo iddi devid senyagwa sekand solo chales kasembe rydhim gitaa waimbaji ni mbaraka mwinshehe mwaruka na stivin hiza suri bonzo

  • @kakimuniafu450
    @kakimuniafu450 5 років тому +1

    Shukran kubwa, ndugu Power Nguzo!

  • @ZilipendwaTanzania
    @ZilipendwaTanzania 4 роки тому +2

    2020

  • @kilisikabasa2848
    @kilisikabasa2848 7 років тому +3

    Pia naomba wimbo wa 'Heshima kijana',wa Mbaraka M.Mwaruka.

  • @abjeffre
    @abjeffre 7 років тому +2

    tis genius.

  • @vaveydkotolomwendwa9958
    @vaveydkotolomwendwa9958 7 років тому +5

    hapo sasa...

  • @sofiambaga9911
    @sofiambaga9911 7 років тому +3

    Naomba wimbo was Regina was Mbaraka Mwinshehe

  • @barackjackson6585
    @barackjackson6585 2 роки тому

    Muongo Bambalawe, kama Safari Sio Kifo, mbona yee kafa SAFARINI i!?🤫😭😢😥

  • @khalifasaid7695
    @khalifasaid7695 2 роки тому

    Aliekung'uta gitaa zito la Bass ni Athuman Babu.huyu mchawi sana kwa Bass na Mbaraka alikuwa nae tokea Mororogoro jazz mpaka Super volcano

  • @nurdinimkasha840
    @nurdinimkasha840 6 років тому +3

    Ama kwa akika mababu zetu wamefaidi sana na sasa nasi twajidai ingawaje wakongwe wa mziki baazi hawapo duniani ira dunia inawakumbuka waishi kwa amani uko wariko

  • @albertokech8168
    @albertokech8168 7 років тому +4

    an excellent composition unlike any other

  • @albertokech8168
    @albertokech8168 7 років тому +5

    an excellent composition unlike any other
    as proposed earlier try to get Heshima also called Tabia njema