"Mwana FA Alinipigia Simu, Ikabidi Nitorokee Hostel Kuja Dar" | SALAMA NA MAUA SAMA PART 1
Вставка
- Опубліковано 5 вер 2024
- #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
ARCTOTIS
Imagine siku moja usharekodi video yako kama msanii anaye chipukia alafu unaenda kumuonyesha ‘Boss’ kwa mbwembwe zako zote, pale mezani mwake unamkuta anaangalia video ya msanii mwengine na kuisifia sana, huku akikuambia wewe kwamba ile sasa ndo yenyewe, ndo njia sahihi huku akiwa hata bado hajaiangalia video yako. Utajiskiaje? Utaondoka au utabaki? Utanuna au utaskiliza kwa roho safi na kwenda kuhakikisha unayafanyia kazi yote aloambiwa? Kumbuka pia huyo ambaye umeonyeshwa video yake yeye ana support kibao, support ambayo wewe unaitamani hata robo yake na ki ukweli kwa juhudi zako ukipata basi ilikua kutoboa ni LAZIMA.
Hii ni story ya Mauwa Sama ambayo ukimpa sikio au macho na ukamskiliza vizuri basi niamini mimi utakua umefanya jambo la maana sana na nakuahidi utajifunza mengi sana. Mauwa alitokea kupendwa tu na Mwana FA ambaye yeye anamuita ‘God Father’ wake kwa jinsi ambayo alifanya na anaendelea kufanya mengi ambayo yamemueka hapa alipo sana, hapa ambapo mimi na wewe ndo tumepata kumfahamu vizuri na kuwa shabiki yake. Ingawa mimi nakumbuka siku ya kwanza ambayo Mwana FA alinisikilizisha wimbo wa Mauwa ya kwanza ambayo ilibamba huko mkoani Moshi, jinsi Hamis alivyokua anaongea kwa excitement, pale tu niliamini alikua kwenye mikono salama. Baada ya hapo alipovutwa kuja Dar napo pia nlikua na pata kipaumbele cha kuskiliza ngoma zake kabla hazijatoka.
Kufanya kazi kwa nguvu, kujitolea, kujitoa na kuchukua risk ni moja ya mashimo ambayo Mauwa aliweza kuyafunika vizuri, humu anatuhadhithia jinsi ambavyo Mama yake alimsaidia kupata ruhusa ya kuja Dar kwa mara ya kwanza kuonana na Mwana FA ambaye alimuambia aje, ila alipofika sio Mwana FA ambaye alimfuata badala yake alikutana na mtu mmoja mrefu mwenye mabega yanayoanzia mlango huu mpaka mlango ule, anasema alishtuka maana hilo halikua tegemeo lake, yeye alijua akifika basi atakutana na Mwana FA na mambo mengine yaendelee kutokea hapo.
Purukushani, maneno, scandal, kupanda, kushuka na kupanda tena na tena kwa Mauwa Sama ni khadithi ya kusisimua, na yeye si muongeaji saaana ila kwa kiasi flani tuliweza kupata chochote kitu. Story ya familia yake na masomo ambayo wazazi wake walimkazania ayamalize ndo moja ya silaha zake kubwa kwa sasa, anaamini kwa jinsi ambavyo wazazi walimlazimisha kumaliza masomo hiyo ndo kitu ambacho kinamtofautosha yeye na wasanii wengine kwa umbali mkubwa hasa.
Rafiki yangu matumaini uta enjoy na kama ilivyo kawaida yetu pia imani ni kwamba utajifunza kadhaa ambayo yatakusaidia huko mbeleni.
Nikutakia Kheri ya Mwaka Mpya, Rafiki.
Amani,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahs...
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
Audiomack Link bit.ly/YahSton...
UA-cam Link bit.ly/UA-camS...
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
Mungu amlinde mtu wangu mwana fa , ndio maana mungu anambaruki af kwa wema wake.
Mahojiano hujenga mazingira ya aina fulani. Na mazingira hayo yana vigezo vyake: washiriki, kusudi / lengo, mipaka, lugha ikiwa ni pamoja na mengineyo ya mbwembwe za mwili, nk.
Runinga haiitaji mbwembwe nyingi za mwili; la sivyo, mzungumzaji ataonekana kama dude tu. Hakuna kinachochafua mazingira ya mazungumzo kuliko kuchanganya lugha, yaani, mseto wa lugha.
Ushauri: Endapo kweli Tanzania yetu inataka kutoa mchango wake kwa Afrika na nje, yafaa sana lugha hii itumike ipasavyo bila kuichanganya na Kiingereza.
Mwisho, Kiingereza neno *ask* au *asked* si *aks* au *aksed*, kama 'linavyovurundwa' na baadhi ya Wamarekani wengi.
Sawa kabisa, hakika umesema kilicho bora sana!
Nakupenda sana sister salama mashallah ❤❤❤❤🥰🇴🇲🌹
Waow!! what a story!! Nafikiri inabidi uandae movie kabisa
Salama unaheshimika sana kwa ajili umejiheshim kwenye safari yako big up sana. Pamoja na kua ulinizingua sku moja na kofia yangu pale maeneo flani ila nakukubali sana kenge ww. Fanya tu kama nimejilipa kukwita kenge ila sio kwa ubaya ✌
Kenge mwenyewe🤐 tuwachie Salama wet alikulazimusha umsifie mbona umechellewa kulipiza kisasi sio kwa ubaya AMKA 🤛
best interview....yaani Maua anajua kufunguka hana wasiwasi amerelaaaaaaaax....
Mauwa sana msani wangu mpendwa..... Good interview watching from Burundi 🇧🇮
Maisha sio raisi kweli watu wanatoka mbali sana hongera hiyo ni fundisho kwa wasichana wengine.
The best interview
Very talented Maua..
❤Salama jabir akimaliza mauwa tuletee mwasiti tume miss❤
Interview nzuri sana
I agree
Dada salama umenenepa sana dear
best interview ever
Umetisha Sana sister mauwa sama
Mauwa kigugumizi 🤣💕
Maua wewe ni msanii usoshuka , upo unapanda na huna mambo mengi , napenda kazi zako
Iyo intro ndefu sana boring
Duh! Maisha sio rahisi sahisi kwakweli
First 1 to comment...
Salama wambie wasanii/wageni wako waongee kiswahili zaidi.
Ndugu usilazimishe mambo yaende hivo nchi ina lugha mbili anglo na kiswa
Kwani unateseka?
Kwa namna mama alipambana naww ndy mana watt wa kike wakiharibika lawama zote Kwa mama
Uko vzr sana Maua
Ao nawew uritoa kitu mbona hukusimama
Kwani salama ni lzm uvae nguo nyeusi tuu
kwel jamna eb bac salam nae abadilishe nguo
Jamani salama uwe ndugu yangu wahiyari. Ila nipo MISRI nikija TZ nitafika kwako nawewe uje kwangu kwetu
😂😹😹
@@didah4really93 nini mbona umefurahi
salama shikamoo?
Maua leo kawa mtu wa moshi sio wa mazinde tena??
Kwani ni wamazinde huyu
☄️❤️
Kumbe tuna unzaa 🙄😱
Naomba mulete Diamond platnumz
hawezi mleta chuki
Hawezi kuja mpaka DUNIA inaisha
Maua anajua sanaaaa💯
Maua apunguze kingerez kingi wakat wa kuongea kinampoteza na hakimpendez na honestly hakijui vizur. ila ni msanii mzur sana.
Nakubali🤣
I disagree mzee dada anakipiga kingi sana
Mauwa sana msani wangu mpendwa..... Good interview watching from Burundi 🇧🇮