Je, Wapwani Tukidai Haki Zetu Mutatupatia?!

Поділитися
Вставка
  • Опубліковано 4 вер 2024

КОМЕНТАРІ • 109

  • @abdallahmasare3116
    @abdallahmasare3116 Місяць тому +6

    Napenda kumsikiliza sana star kwa sababu ya ushahidi wa hakika anaotoa

    • @makhanguwakhutu2408
      @makhanguwakhutu2408 Місяць тому

      @@abdallahmasare3116 Sasa Hawa wenye tuashi nao hapa pwani ya afrika mashariki Hao Kuna machotara Kumanisha mchanganyiko wa bantu na weupe yaweza kuwa India Iran mwarab au weupe wa ulaya na hao wenye unaona wembamba kama Somali oromo tao ni mix ya nilotes na watu weupe ndio matokeo sio watu asili wa afrika tunawaita chotara

  • @ahmedyusuf6501
    @ahmedyusuf6501 Місяць тому +2

    Mashaallah,
    Mwenyezi Mungu akuzidishie ilimu kutuelimisha malimwengu.
    Inshaallah, tuko nyuma yako 🙏🙏🙏🙏

  • @fardoshnassor7847
    @fardoshnassor7847 Місяць тому

    🤲🏾💖

  • @FatwimaZahrau
    @FatwimaZahrau Місяць тому +2

    Jamanini wapwani tusimameni kidete na sisi tupate haki zetu

  • @omarjumaan3061
    @omarjumaan3061 Місяць тому +4

    Kweli kabisa lakini serekali wakaanza kugawanya wapwani kwa kuanzisha black muslims ilikugombanisha wapwani kwa njia ya pesa
    😢

    • @princefeisla3692
      @princefeisla3692 Місяць тому

      Sio serekali ni sisi wenyewe walafi hatuna Imani wabinafsi😢

    • @johnlobuin4212
      @johnlobuin4212 Місяць тому

      Serikali viongozi, taja kiongozi

  • @ashomohammed5963
    @ashomohammed5963 Місяць тому +2

    Kweli kabisaaa.

  • @chriscao9828
    @chriscao9828 Місяць тому

    Nakubaliana na wewe kwa asilimia mia Moja.. sisi watu wa pwani tumedhulumiwa sanaa

  • @user-bu6bp4yl6u
    @user-bu6bp4yl6u Місяць тому +4

    Sadaktha 🌟

  • @abdallakhamis2255
    @abdallakhamis2255 Місяць тому +3

    Watu hupigania Haki zao nyinyi tatizo lenu Wapwani mwangoja kupewa!

    • @stambuliwash.abdillahinass8123
      @stambuliwash.abdillahinass8123  Місяць тому

      Haki ina namna ya kupiganiwa, watu wa kuipigania, na wakati wa kuipigania; haipiganiwi namna yoyote, na watu wowote, ama wakati wowote!

  • @aliyissa9857
    @aliyissa9857 Місяць тому +1

    Bhot Achaye

  • @abdallakhamis2255
    @abdallakhamis2255 Місяць тому +3

    Wapwani wenyewe ndio wameshindwa kupigania Haki zao na ndio sababu wakaitwa Wavivu, Waoga na Wajinga!

    • @shabanmaulana8594
      @shabanmaulana8594 Місяць тому

      Kweli, kabisaaaa manake wazee wakiambiwa majibu yao utasikia waateni atutaki vita wataviata hapa hapa . Mashamba yakaenda , makazi yote ya kaenda mamlaka yote yakatwaliwa tukabakia weupe .

  • @manjoriwakunesa7006
    @manjoriwakunesa7006 Місяць тому +1

    Naomba uchambuzi wa vita vyo majimaji je wapiganaji wakuwa dinigani

  • @johnlobuin4212
    @johnlobuin4212 Місяць тому +1

    Hakuna, hamtapata

  • @makhanguwakhutu2408
    @makhanguwakhutu2408 Місяць тому +2

    Kitu muhim inafaa pia ukumbushwe kwamba hao unaotaja ni watu wakuja afrika kutoka kwao bara la asia huko ndio asili yao haijalish walikuja lini afrika ama Kenya hata wenyewe wana ushahidi kwamba ni wahamiaji kutoka asia na ulaya na ukumbuke kabla ya kuja hawa asians na wazungu afrika kuanzia Nigeria congo hadi huku pwani ilikuwa hamna mipaka na wafrika walisha kwa kuhama hama na idadi yao ilikuwa chache

    • @ahmedmohammed937
      @ahmedmohammed937 Місяць тому

      Tupe evidence wacha domo kubwa lako mulikimbia congo mukaja miji yetu

  • @deepskyimages5554
    @deepskyimages5554 Місяць тому

    shida ya wapwani wengi hawapendi kujituma pili pwani kuna kama chuki za ndani kwa ndani dhidi ya sisi wenyewe kwa wenyewe na tatu miongoni mwetu sisi wapwani au kiufupi viongozi wa pwani baadhi yao ni walafi wasiotosheka na wasiopenda wengine wafaidike..! so kwanza maradhi haya yataftiwe tiba kwanza ili kuwepo na umoja thabiti ndipo suluisho inaweza kupatkana.

  • @kalengashoppingcenter1108
    @kalengashoppingcenter1108 Місяць тому

    Wamombsa sawa na Wapemba kwa kujitetea kama wapo Dunia Nyingine we need 1 unit & nicely Africa

  • @user-co9td1iq9o
    @user-co9td1iq9o Місяць тому

    Sasa kama MRC ilitaka pwani ijitenge mukawakataa pwani iwe na serikali yake saii mwalia mwataka haki😂😂😂😂😂

  • @ggmuswahili7074
    @ggmuswahili7074 Місяць тому +2

    Sasa wahindi wakirudi makwao au wakienda ulaya mzee wewe unaumizwa na nini, umesema vizuri tu na ni kweli nakuunga mkono sisi huku tunaishi nao na tumeishi nao vizuri kama ndugu zetu, lakini suali ni...je wao wanaishi na sisi vizuri kwao, mi binafsi nimesoma india miaka minne University, na kwa kweli kule muafrika anaonekana kama takataka, dhulma tunazofanyiwa na la kuhuzunisha zaidi ni, ndugu zetu wahindi weusi wenye asili za kiafrika, kwa mfano mimi binafsi nilipata bahati ya kuenda Gujarat kutembea, ni mkoa flani upo pwani magharibi mwa india, kuna kabila linaitwa siddis, historia yake hawa jamaa wametokea east africa, inavyosemekana Kenya, Tanzania, Uganda, daaah kwa kweli wale watu wanaishi maisha duni sana ukilinganisha na wahindi wengine, serikali imewatekeleza kabisa na kibaya zaidi jamii pia inawanyanyasha, yani wanapitia racism ya hali ya juu. Na ushahidi upo humu humu UA-cam. Ukichukua muda wako zipo content kibao tu media tofauti tofauti na channels tofauti watu wamezuru maeneo hayo na wakaangazia hawa jamaa siddis wanavyoishi. Hapa kwetu ma sha Allah wahindi wapo successful kwasababu wamepewa platform tangia tangu na tangu, tangia zama za mwingereza na hata baada ya mwingereza kuondoka. Tofauti na kule kwa wenzetu. Mtu mweusi hana haki na sioni dalili kua ipo siku watapewa haki yao kama wanavyopata wahindi wengine
    Najua utajiuliza kwanini nimekuja na hii mada, nimeileta hii mada kwasababu unasema wahindi na waarabu ni wakenya zaidi ya baadhi ya makabila fulani, sababu unasema ni kwakua walikuja kwenye ardhi hii inayoitwa kenya kabla ya baadhi ya makabila ya kiafrika, la hasha haupo sahihi mzee wangu kwa hilo. Na hii si kwa wahindi tu, hata kwa waarabu na persians na jamii nyengine zisizokua za kiafrika, sote ni wakenya lakini ukinena wao ni wakenya zaidi ya waafrika, mimi ntakujibu waafrika ni wakenya zaidi ya Asians. Kwanza hizi borders ni borders zimechorwa na mkoloni, na hilo unalifahamu sina shaka, wewe ni mpenzi wa historia bwana. Kwahivyo hizi borders zikichorwa nia na madhuni ilikua ni kutugawanya na kukutuawala. Wenyewe wanasema devide and conquer na naam walifanikiwa kwa hilo na mpaka sasa bado wanaendelea kula matunda. Ilipaswa Afrika iwe ya muafrika kama ilivyo ulaya ni ya mzungu na bara arabia ni ya muarabu, sio kwamba hakuna jamii nyengine kule, tena zipo jamii kwa mfano kama yemen, yapo makabila ya kiafrika ama niseme ya watu weusi,yameingia kitambo kabla hata ya baadhi ya jamii za kiarabu, lakini angalia maisha yao, angalia jamii ya waarabu wekundu au niseme weupe kwa lugha ya hapa kwetu, yani wanachukuliwa kama 2nd class citizens, na si Yemen tu, nimepiga mfano wa Yemen lakini ndo ilivyo karibia kila nchi nje ya bara Afrika, huo ndo uhalisia na hivyo ndo anavyoishi muafrika.
    Kwahiyo hoja yangu mimi ni kua, hizi kauli za kusema huyu ni bora kuliko yule au huyu ni mpwani zaidi ya yule, alafu kibabaya zaidi tunanyosheana vidole wenyewe kwa wenyewe inakua haileti natija, hasa maneno yakitoka kwa mtu anaeheshimiwa na jamii kama wewe, hamna aliye bora kati yetu isipokua kwa matendo yake, mswahili, muhindi, mmijikenda, mwarabu wote ni sawa sawa, hakuna bora wala duni. Shukran

  • @AlphayoLugallah
    @AlphayoLugallah Місяць тому +5

    hakuna chama kilichotikisa kutoka Pwani kama IPK ,nilikuwa mdogo nyakati hizo lakini dhoruba zake niliziona

    • @MohamedAbdallahSaid
      @MohamedAbdallahSaid Місяць тому

      Kutoka hapo Serikali ilianza kuwachukulia watu wa Pwani kuwa wanahaki kama Wakenya wengine haswa Waislamu. Mpaka hapo wakati wa harakati za IPK wata Waziri hata Katibu Mkuu muislamu ilikuwa hakuna

    • @MrNoNonsenseYes
      @MrNoNonsenseYes Місяць тому

      Kisha baada ya hizo dhoruba unazozisema matunda yake nini ???

    • @MrNoNonsenseYes
      @MrNoNonsenseYes Місяць тому

      Kisha baada ya hizo dhoruba unazozisema matunda yake nini ???

    • @AlphayoLugallah
      @AlphayoLugallah Місяць тому +2

      @@MrNoNonsenseYes unachokiongea ni sawia na jina lako.mwafrika ila ajidai beberu la kizungu

    • @MohamedAbdallahSaid
      @MohamedAbdallahSaid Місяць тому +1

      @@AlphayoLugallah Watu wengine wanaishi na chuki ilihali kila binaadamu ana haki ya maisha yake.Hata ndani ya familia zao hawana raha juu ya kupenda chuki.Ndio maana ya huyo alieuliza baada dhoruba ya IPK ilitokea nini?

  • @fredmakasinatembeya792
    @fredmakasinatembeya792 Місяць тому

    Wewe Wacha uchochesi.kwenda Oman

    • @hassanalhussein3982
      @hassanalhussein3982 Місяць тому

      Wewe Jaluo Rudi kwenu Sudan. Pwani si Kenya ama bado hujasikia? Karibuni mutajikuta mukiuuana nyinyi Kwa nyinyi mapunda

  • @omadal1
    @omadal1 Місяць тому +2

    My question or concern what is the way forward, infact haya maoni or mwamko unao tuwambia needs solution.

  • @Fm-MornStar2014
    @Fm-MornStar2014 Місяць тому

    Sasa mzee wangu, kila jamii au kanda ikizungumza kana kwamba inaonewa, je tutakuwa WAKENYA lini?
    Nilifikiri tuwe WAKENYA kwanza kabla ya kuwa wa Ukambani, Pwani, Kanda ya ziwa.... Kwanini tusipiganie Kenya badala ya kujigawa makundimakundi.
    Ni maoni yangu tu mzee wangu.
    SHUKURANI KWA MAKALA ZURI.

    • @stambuliwash.abdillahinass8123
      @stambuliwash.abdillahinass8123  Місяць тому

      Kwa hakika, mimi sioni ubaya wa watu/jamii kujitambuwa ki-kabila iwapo hawabagui mtu wa kabila nyengine. Kisha, ukisoma na kuangalia historia yetu utaona kuwa tumeowana na jamii nyingi nyengine na hata kuzaa nao. Sasa, tatizo liko wapi?!

  • @makhanguwakhutu2408
    @makhanguwakhutu2408 Місяць тому +1

    Huwez kudai kwamba mtu mweupe ndio asili ya afrika kuliko siisi wenyewe haijalishi ukija kwa shamba langu ikiwa hujaniona ukadai ni kwako so kitu muhim tuish tu kwa amani na kupendana lakini usiwahi kudai kwamba hawa wafrika ni wageni kwa bara lao hiyo nikukosa kusoma history yako kwa undani mwafrika ndani ya afrika huwez kumuona ni mgeni ndani ya ardh yake eti kwa sababu umekuja miaka alfu

  • @rashidtora1182
    @rashidtora1182 Місяць тому +1

    Watu wafanyeje ,sheikh ?

    • @stambuliwash.abdillahinass8123
      @stambuliwash.abdillahinass8123  Місяць тому +2

      La muhimu sana kufanywa ni watu kueleweshwa kuhusu mambo yaliyotukia hapo kitambo ili waeleweshwe makosa yalitokea wapi, na nani wahusika, mpaka tukafikia hapa tulipo hivi leo. Baada ya hili la kueleweshana kufanyika, jengine la muhimu zaidi ni watu (kizazi kilichohusika na kilichoko) wasameheane na kupanga mikakati na mipango ya kusonga mbele pamoja.

  • @nassirjabry2236
    @nassirjabry2236 Місяць тому +1

    Ikiwa 18%ni wamijibkenda je waona jamii za pwani zimepewa mgao sawa

    • @stambuliwash.abdillahinass8123
      @stambuliwash.abdillahinass8123  Місяць тому +1

      Kwa hakika, hiyo ni dhuluma kubwa sana. Lakini, hata hivyo, ni muhimu watu kuelewa kuwa hata hao Mijikenda walioko hapo kwenye khatamu za kusimamia hiyo Bandari si watu wanaowakilisha maslaha ya watu wa jamii ya Mijikenda bali ni watu wanaojinufaisha wao binafsi (kwa kuwa 'wawakilishi' wa waliowaweka kwenye hizo nafasi za usimamizi)!

    • @mohamedmwatuwano5526
      @mohamedmwatuwano5526 Місяць тому

      Binadam yuashi popote: wakenya wako kila mahali, America, Uingereza, France, nchi za kiarabu n.k. Haya yote ni mambo ya mpito. Tusitiane ghadhabu sizizo na msingi.

  • @ismailsuleiman394
    @ismailsuleiman394 Місяць тому +1

    Stanmbuli mashallah Allah akuzidishie hao wajinga waona leta comment zao bila ushahidi ni mamluki hawajijui asili zao.akili za kijinga sana eti mwafrika lazima awe mweusi.mbona Iko wazi pwani yote kuanzia Sudan mpaka sychelles more than 90% sio weusi kama wanavyo jua wao

    • @michaelthobias9967
      @michaelthobias9967 Місяць тому

      Ukweli mchungu wazungu ,warabu,na wahindi sio wafrica hilo lipo wazi hata Moroco uliona wachezaji wao walisema wao sio wafrica nisahihi mana sio wafrica hapa tz ,Kenya ,Uganda sio wafrica

  • @user-dv9pc4rx7v
    @user-dv9pc4rx7v Місяць тому

    Tafadali Sana andika hii historic kwa vitabu ili isipitwye wewe NI kinze ya information wabara hawawezi kushindana nawe

  • @sankofaman4112
    @sankofaman4112 Місяць тому +1

    Swali langu kuu kila nnapokuskiliza Sheikh Stambuli ni, je wewe ukizungumza juu ya watu wapwani wazungumza kwa niaba ya waislamu, wahindi na waswahili peke yake? Sisi wengine kwetu wapi? Nadhani nlikuskia kipindi flani ukisema kwamba 10 mile strip inafika Sultan Hamud, je sisi waduruma na wataita tulikua wapi kama kwote kulikuwa kwa Waswahili? Au sisi pia tulihusika katika kuwasukuma waswahili? Na je, ukizungumza kuhusu ubaguzi, Waswahili, Wahindi na Wachina waliokuwepo wakati wa utawala wa Sultani na waIngereza hawakuhusika katika kutubagua sisi waPwani weusi? Tatizo hili la ubaguzi naweza kusema nlilianza nyinyi na bado mwaliendeleza nyinyi wenye rangi za kung'aa. You guys were comfortable when you were identified as second class citizens by the masters. In short you were the comfortable as house slaves.

    • @stambuliwash.abdillahinass8123
      @stambuliwash.abdillahinass8123  Місяць тому +2

      Kwa hakika, hata wanaozungumza kuhusu haki za watu huku kwetu siku zote huwa hawajumuishi hao watu wa hizo jamii tunazojadili hapa. Na, mimi sioni ni kwa nini kuwa na chuki dhidi ya watu wa jamii hizo ambazo zikitajwa huwa kuna machukivu fulani kutoka kwenu! Kwani hakuna watu wa jamii za kiafrika ambao ni wabaya pia?1 Je, tuchukie kila Muafrika kwa sababu ya waovu wachache miongoni mwao?!

    • @stambuliwash.abdillahinass8123
      @stambuliwash.abdillahinass8123  Місяць тому

      @sankofaman4112 hilo jambo unalotusingizia sisi (watu wenye ranging za kung'ara) kuwa tulikuwa tunaridhika hata tulipokuwa tumewekwa 'daraja ya pili' miongoni mwa watu wa eneo hili si kweli! Na, inasikitisha kuona huelewi yaliyokuwa yakitukia huku kwetu wakati wa utawala wa Wareno, Sultan, Waingereza, na hata hivi sasa tukiwa chini ya mamlaka ya Kenya huru. Tafadhali, hebu angalia makala ya pili ya mjadala huu kwenye ukirasa huu wangu, kisha, tutaongea zaidi. Ahsanta sana kwa maoni yako.

  • @febamohammed2989
    @febamohammed2989 Місяць тому +2

    Be specific mzee ukitaja wapwani unamaanisha kina nani? Maana kwa audit report ya port nimeona 18% mijikenda na ndio highest position au unamaanisha wapwani kina nani?

    • @ericlondonmuwazijimmy1221
      @ericlondonmuwazijimmy1221 Місяць тому

      😂😂😂

    • @stambuliwash.abdillahinass8123
      @stambuliwash.abdillahinass8123  Місяць тому +3

      @@febamohammed2989 Wapwani ambao bandari iko kwao ni Waswahili. Hawa ndugu zetu wengine ambao nao ni Wapwani wanatubaguwa kutokana na itikadi ya uwongo kudai qao ni Wapwani zaidi kuliko sisi Waswahili (jambo ambalo nishalieleza sana na kulitolea ushahidi)!

    • @KhalifaSaid-lg5dh
      @KhalifaSaid-lg5dh Місяць тому +2

      Sisi wadigo ndio wenyew na wenye pwan

    • @ericlondonmuwazijimmy1221
      @ericlondonmuwazijimmy1221 Місяць тому

      @@stambuliwash.abdillahinass8123 so all the time you were talking you were trying to talk of your clansmen 🤔🤔🤔. Rais museveni kasema ideological bankruptcy is bad, nimeamini leo.. you will waste time on useless things.

    • @stambuliwash.abdillahinass8123
      @stambuliwash.abdillahinass8123  Місяць тому +1

      @@ericlondonmuwazijimmy1221 hayo ni maoni yako, na nayaheshimu. Lakini, muhimu sana uelewe 'mambo yana mambo yake!

  • @Nightcamel2203
    @Nightcamel2203 Місяць тому

    There's no spoon feeding my dear. Haki yako ni utoke ukachukue. Hakuna kitu cha kupewa..

    • @stambuliwash.abdillahinass8123
      @stambuliwash.abdillahinass8123  Місяць тому

      It very much depends on the script you are reading! Well, with me, just informing serious thinkers who are aware of what time it is only.

  • @nixonmwanguni3094
    @nixonmwanguni3094 Місяць тому +2

    Kusema kweli kenya mwaidumbukiza kwa shimo.angalieni Somalia ,Congo na nchi nyingi za kiafrika jee mwaitakia kenya hivyo ? Tafakarini.

  • @omaribrahim1087
    @omaribrahim1087 Місяць тому +2

    Pwani sio Mombasa Tu ni kutoka kismayuu Zanzibar pemba mpaka maputo

    • @stambuliwash.abdillahinass8123
      @stambuliwash.abdillahinass8123  Місяць тому +2

      Ni muhimu pia wewe kuelewa kuwa kila sehemu (yaani, Mombasa, Lamu, Malindi, Pemba, Zanzibar nk) ilikuwa ni 'Taifa' (City States) kipekee kabla ya kujumuishwa pamoja!

    • @omaribrahim1087
      @omaribrahim1087 Місяць тому

      @@stambuliwash.abdillahinass8123 ndio

    • @omarjumaan3061
      @omarjumaan3061 Місяць тому +1

      Tafakari huo mwambao wa pwani ulotaja hapa ungekua ni nnchi moja maendeleo yake yangekuaje ???!

    • @omaribrahim1087
      @omaribrahim1087 Місяць тому

      @@omarjumaan3061 tungekuwa na maendeleo zaidi ya tunayoyaona maana wafu wametoka ndani mpaka Congo Malawi na kwengineko kufata maendeleo

    • @makhanguwakhutu2408
      @makhanguwakhutu2408 Місяць тому +1

      Ni kweli lakini ilikuwa kabla ya kuchora mipaka ya Kenya Tanzania Somalia Uganda Sudan na Ethiopia sababu Uganda ilikuwa inakuja Hadi naivasha na Somalia ilikuwa inakuja Hadi garden Hadi isiolo

  • @makhanguwakhutu2408
    @makhanguwakhutu2408 Місяць тому +1

    Bwana istambuli nimekusikiza kuanzia nikiwa mdogo pale mombasa ulikuwa ukihubir sana ukidai mara nyinyi ndio original wa pwani hilo nikukosa kujitambua kila mtu mweupe unaemuona pwani ya afrika yote huyo ni muhamiaji tu sio mwenyeji haijalish amekaa miaka ngapi na mtu yeyote mweusi unaemuona ndani ya afrika huyo siku zote ni mwenyeji haijalish alikuwa sudan congo south Africa hyo yote ni afrika mipaka tumewekewa tu na hao watu weupe ndio waweze ku divide and rule system ndio maana hakuna mtu mweusi hapa kenya pwani anadai ametoka arabuni Asia ama ulaya kwa sababu yeye ni mwenyeji wa afrika so heshimu watu weusi kwa kukubali kuish na watu weupe kwa amani wafrika wetu huteswa asia na ulaya kote hadi sasa na wewe uko hapa kutoa fake history eti tumetoka congo Sudan south Africa hyo ni fake history mumetengezewa na wakoloni munasahau afrika haina mipaka kuanzia pwani ya kenya had pwani ya libya

    • @jumaseifjuma4185
      @jumaseifjuma4185 Місяць тому

      Wewe inaonesha hata geography huijui kwa kudai bara la Afrika ni watu weusi pekee. Hivi zile nchi zote za Afrika ya Kaskazini vp ? Wao siyo Waafrika, ukubali tu siku zote waliofika mwanzo ndo wenyewe waliofika mwisho wageni. Wacha kasumba za uafrika Dunia watu wametembea, wamehama na kuhamia........!

    • @makhanguwakhutu2408
      @makhanguwakhutu2408 Місяць тому

      @@jumaseifjuma4185 hao wenyewe ukiwauliza wanakubali sio wafrika hata mara mingi wameomba wajiunge na ulaya ama Asia lakini imeshindikana kama umewahi kufanya baath Moja Kwa moja kila mtu pale anadai asili yao ni arabuni wengne asili yao ni ulaya hakuna hata mmoja anakubali ni mwafrika hata hapa afrika mashariki watu weupe wote wanakubali Kwa ni arabuni wengne India wengne ulaya na hakuna mtu mweusi ndani ya afrika anadai ametoka inje ya afrika Sasa iweje wewe uwapimge kwamba wao asili yao ni pwani afrika na wenyewe wanakataa na wewe ni muislam qulil haqq Lau kaana murraa la takutumul haqq antum taalamun

    • @makhanguwakhutu2408
      @makhanguwakhutu2408 Місяць тому

      @@jumaseifjuma4185 hao wote wanao ishi coastal region of northern Africa west Africa east Africa jiulize mbona ni weupe nna hawako huku central Africa wako tu mwisho mwisho kilichofanyika miaka mingi walivofika Africa walikuwa na silaha na vita dhidi ya humble man Africa man ndio akatoroka hizo sehem kundi kubwa la Africa wakakimbilia west central south Africa na east Africa Kwa Kutafuta usalama wao

    • @makhanguwakhutu2408
      @makhanguwakhutu2408 Місяць тому

      @@jumaseifjuma4185 Sasa wafrika wakaogopa kuish karib ufuani ama pwani za Africa Kwa sababu ya maadui kuwavamia na kuwafanya watumwa hii history nakupea ni miaka mingi sana kabla hata nabii musa aleihi wasalam na ni kitu tu unamutumia tu Akili na common sense Kwamba huko nyuma utumwa mauaji dhidi ya wafrika imefanyika Karne na Karne ndio imechangia wafrika kukimbia na kupoteza hayo maneo ya Northern Africa Kwa zile nichi zinazopakana na pwani ya meditirian sea huko kulikuwa na maadui wakwanza kutoka huko ulaya Kisha wapili arabuni ndio wamechangia huoni Tena mtu mweusi huko isipokuwa Moja moja tu Tena chotara Yani alishachanganya na weupe mfano kama Fulani na hao weupe

    • @makhanguwakhutu2408
      @makhanguwakhutu2408 Місяць тому

      @@jumaseifjuma4185 na ukisikia jina congo haimanishi tu pale penye unaona Kwa Sasa congo maanake asili yake ni kuanzia huko central Africa Hadi huku east Africa na nisawa na kusema habasha ama habsh mwarab alimanisha Africa sio tu hapo adis ababa Ethiopia maana ingne ni kusema Africa na Sudan inamanisha Africa pia Yani bara la watu weusi so sio tu hapo Khartoum congo Sasa Kuna history inafaa uje tukisomeshe ndio utajua kwanini watu walikuwa wengi ndani ya congo forest ni Kwa Ajili yakujicha maadui kutoka ulaya na Asia sio eti asili yao ni congo hyo mkoloni anakupea fake history ili usijielewe afrika yote ni ya mtu mweusi hao weupe ndio matokeo ya uvamizi wakuvamiwa mtu mweusi ndio maana hao weupe wako tu kando Kando ya afrika

  • @MrNoNonsenseYes
    @MrNoNonsenseYes Місяць тому +2

    Huyu mzee uwa kapuku sana Mungu anisameh, wahindi na waarabu kwamba wao ni wakenya zaidi zaidi ya muafrika ???? Nenda Asia kaangalie watu wenye asili ya kiafrika uone wanavyokua mistreated, Si India, si Iran, si Yemen etc, Mtu mwenye asili ya Kiafrika hakijui kitu kinachoitwa true peace of mind katika maeneo hayo. Nishakusikia haipungui mara kumi ukizungumzia udugu wako au wenu na wa Asia lakini kama haitoshi, at the same ukizungumzia kutokua na udugu kwako/kwenu na jamii nyengine za pwani kama vile mijikenda, are you an agent umetumwa ????
    Personally nilichokigundua mimi ni kua unapata tabu sana, unasumbuliwa na inferiority complex, inahuzunisha sana especially ukizingatia umri wako. Alafu haki ya wapwani wapi hao unayo izungumzia na wewe na wenzio mushacreate division among coasterians,

    • @AlphayoLugallah
      @AlphayoLugallah Місяць тому +1

      @@MrNoNonsenseYes matamshi yako yanaonyesha ukomavu wako wa akili. Mungu akusamehe kwa kosa lipi?!

    • @AlphayoLugallah
      @AlphayoLugallah Місяць тому +1

      @@MrNoNonsenseYes kuchanganya kiswahili na kizungu haimaanishi hu msomi sanaa.twajua hu mzungu kutokana na jina

    • @stambuliwash.abdillahinass8123
      @stambuliwash.abdillahinass8123  Місяць тому +3

      @MrNoNonsenseYes, pengine hujui kuwa kuna Waarabu na Wahindi ambao walikuwako kwenye ufuo wetu kwa karne nyingi kabla ya baadhi ya Waafrika wenzetu kuja kuishi kwenye Mwambao huu wetu! Hata hivyo, kuna baadhi ya watu wa jamii hizo ambao wamezaa na wenyeji wa huku (Waswahili) na kuishi kwa muda mrefu sana. Tafadhali, elewa hilo.

    • @AlphayoLugallah
      @AlphayoLugallah Місяць тому

      @@stambuliwash.abdillahinass8123 huyu hata usinge mjibu.hana ustaarabu wala hayumo kwa kutaka kujuwa ila umetumia busara na hekima kumjibu

    • @AlphayoLugallah
      @AlphayoLugallah Місяць тому

      @@stambuliwash.abdillahinass8123 huyu hata usinge mjibu.hana ustaarabu wala hayumo kwa kutaka kujuwa. ila umetumia busara na hekima kumjibu