MATESO YA FAMILIA - PASTOR SUNBELLA KYANDO
Вставка
- Опубліковано 22 жов 2024
- Isaya 40:24
Naam, hawakupandwa; hawakutiwa katika ardhi kama mbegu; naam, shina lao halikutia mizizi katika ardhi; tena awapuzia tu, wakanyauka, upepo wa kisulisuli wawaondoa kama mabua makavu.
Mwandishi hakatai kuwa kuna watu wamepandwa lakini hawana mizizi,yaani hawakuingizwa chini ya ardhi ili wapate mizizi.Kwa mfano wa mti usio na mizizi kuangushwa kwake inakuwa ni rahisi sana.
Biblia inaendelea kusema kuwa, "Shina lao halikutia mizizi..."
Hii ni lugha ya kiroho,yaani ni kweli mti ni mkubwa na umesitawi lakini hauna umaana(useless),maana hata kwa upepo tu huu mti utaanguka.Yaani watu hawa hata wawe wanaonekana wamefanikiwa kwa kiasi gani katika ulimwengu wa mwili lakini adui akiwaangalia katika ulimwengu wa roho anawaona ni sawa na bua,akitaka kuwaondoa muda wowote kwenye hizo nafasi walizopo. Shetani akiwa na uhalali wa kukushikilia anaweza akakuacha ukaanza jambo,iwe kazi,biashara,ndoa n.k kwa sababu anaujua wakati ambao atautuma upepo na kukutoa kwenye hiyo nafasi.
Anachokifanya adui, anatafuta kukupiga sehemu ambayo akikupiga hiyo sehemu mpaka uweze kusimama tena, inakugharimu sana na itakuwa imekuingiza kwenye aibu sana.
Ndio maana ni muhimu sana kabla mitego haijateguka tuhakikishe tumeitegua.
#PastorSunbella#Mateso#Familia
Amen mtumishi barikiwa sana
YESU AHSANTE
Amen
Amen amen amen asante yesu kwakunipa mtumishi wako huu ujumbeee. Ili tufunguke
Amen amen amen Daddy
Nnashida Sana ya kumuona huyu mchungaji the day I will put my feet in Tanzania there will be no rest till is done..
Koo zetu hivo Sana Kuna siku nilimuliza maswala hayo alishindwa kunijibu akasema nimefikilia nini.kikweli ninafwatilia wachungaji ninapata neno Kila siku Asante kwa wachungaji kwa kutuelimisha asanteni Sana niwachache wanaharibia sifa zenu.
Bwana yesu asifiwe Jamani Munisaidie namba ya pasta Sanbella niko Burundi naitaji kuongea naye
Mwenye sikio na asikie maneno yenye utukufu juu ya utukufu.
Mtumishi nahitaji kuongea na wew Niko kagera nimetafuta namba kanisani kwako nimekosa
No za simu tunaomba
Amen