Sizonje - Mrisho Mpoto ft Banana Zorro (Official Video)

Поділитися
Вставка
  • Опубліковано 5 вер 2024
  • Nyimbo Mpya ya Mwaka 2016, Sizonje.
    [Kibwagizo - Banana Zorro]
    Sizonje hii ndio nyumba yetu
    Milango ipo wanapita madirishani
    Sizonje ndio nyumba yetu
    Milango ipo wanapita madirishani
    Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
    Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
    [Bridge - Banana Zorro]
    Tulikaa barazani, tukasikia kelele
    Kelele toka ndani, mtu anaruka dirishani
    Sizonje, karibu nyumbani kwetu
    Uone maajabu ya nyumba yetu
    [Verse 1 - Mrisho Mpoto]
    Karibu sana Sizonje, hii ndo nyumba yetu,
    Tulipoficha mundu za kupondea wezi,
    Kwani, makaburi yaliofukuliwa lazima yazikwe upya?
    Nyumba hii Sizonje ina vyumba vinne,
    Vitatu havifunguki, kimoja hakina mlango,
    Japo kuwa kina watu ndani, na hawaongei kiswahili,
    Wenyeji wanalala sebleni na walishazoea,
    Sizonje kule tulipotoka panaitwa jikoni,
    Huna haja ya kwenda kule, kumejaa mafundi wa kupika
    Sasa hivi wanakupikia wewe ili ule ulale
    Ukiamka muongee nini hasa ujio na dhima ya safari yako
    Wanashangaa mbona ghafla
    Samahani sana mgeni
    Wapishi wameniomba kwamba
    Nikuulize tena kwa kukuomba kwamba
    Eti unapenda vya mafuta au vya nazi?
    Wanataka kukuonyesha madoido katika mapishi yao Sizonje
    Sizonje chumba hiki naomba usiingie
    Ukimaliza nitakwambia kwanini
    Kuna sauti inajirudia mara kwa mara
    Na hapa mlangoni kulikuwa na picha mbili kubwa
    Moja picha, nyingine mchoro wa picha wa kwanza
    Ninachokumbuka iliwahi kuandikwa
    “USIYEMTAKA KAJA”
    Hatukuwahi kuelewa maana yake
    Labda kwa sababu ya ujio wako unaweza kutusaidia
    [Chorus - Banana Zorro]
    Sizonje hii ndio nyumba yetu
    Milango ipo wanapita madirishani
    Sizonje hii ndio nyumba yetu
    Milango ipo wanapita madirishani
    Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
    Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
    [Verse 2 - Mrisho Mpoto]
    Najua, wimbo mbaya haufai kubembelezea mtoto
    Na kamwe mtoto hawezi kuungua
    Kwa kiazi kilichokuwa kwenye kiganja cha mama yake mzazi
    Njoo huku uone Sizonje
    Si unajua, harufu ya uzazi haiishi mpaka mtoto akue?
    Sawa, Sizonje, huu hapa ni ua
    Lile pale ni shimo la taka
    Na kile pale ni choo
    Kinachotutisha na kutuogopesha zaidi
    Wanaoishi humu ndani hawajawahi kutupa taka
    Wala kwenda chooni
    Kama ukiwa makini
    Kwa nje utasikia sauti za makundi ya watu
    Wengi ni vijana, wana bahasha za khaki mikononi
    “KAMA HAMTUPI TAKA SHIMO HILI MLICHIMBA LA NINI?”
    Lakini pia kwenye sauti zao, Sizonje
    Kuna watoto, wazee na kina mama
    Ukiunganisha sauti zao ndio unapata hizo kelele
    Ninavyosikia, ila sina uhakika
    Waliambiwa kihistoria nyumba hii ni ya kwao
    Na wana haki ya kutupa taka na kutumia choo hiki
    Sasa, njoo nikuonyeshe huku uchochoroni
    Uone maajabu mengine ya nyumba hii
    Sizonje, ukiona tembo anaringa
    Ujue mvua zinakaribia
    [Chorus - Banana Zorro]
    Sizonje hii ndio nyumba yetu
    Milango ipo wanapita madirishani
    Sizonje ndio nyumba yetu
    Milango ipo wanapita madirishani
    Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
    Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
    Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu
    Ingia uyaone, maajabu ya nyumba yetu

КОМЕНТАРІ • 408