Nahodha || Dodoma Adventist Chorus

Поділитися
Вставка
  • Опубліковано 15 вер 2024
  • NAHODHA
    Siku moja Yesu aliwaambia
    Wanafunzi wake hebu na tuvukeni ng'ambo
    Wakapanda wote ndani ya chombo
    Mara tufani chombo kikaanza kujaa maji
    Wakati huo Yesu amelala
    Wakamwendea kumwamsha
    "Bwana Twaangamia"
    Akasimama, kakemea upepo
    kukawa shwari dhoruba zikakoma
    Kisha akageuka
    (Kisha akageuka)
    Akawauliza
    (Akawauliza)
    Imani yenu i wapi
    (Je imani yenu i wapi nao wakaogopa)
    Ni nani huyu ambaye
    (Je ni nani huyu ambaye)
    Pepo na Bahari vinasikia sauti yake.
    Huyu ni Nahodha mwenye uzoefu mkuu
    Mikononi mwake chombo huwa salama.
    Unawezamwamini maana Chombo hakijawahizama Akiwa ni Nahodha
    Mambo yote huwa salama
    Katikati ya Dhoruba na Shida
    Pepo zivumapo na Bahari ichafukapo
    Unaweza kudhani amelala
    Na hajali kuhusu shida zote upitiazo
    "Je ni kweli huyu ndiye ambaye
    Alisema 'takuwa nami Tena nisiogope
    Nina mashaka na uwezo wake
    Je ni kweli anaweza kuokoa?"
    Usiogope ndugu
    (Usiogope ndugu)
    Na usifadhaike
    (Na usifadhaike)
    Imani yako weka kwake (hajawahi kushindwa)
    Nahodha huyu si mwingine
    Bali Bwana Yesu, amini utafika salama
    Huyu ni Nahodha..
    Huyu ni Nahodha mwenye uzoefu mkuu
    Mikononi mwake chombo huwa salama.
    Unawezamwamini maana Chombo hakijawahizama Akiwa ni Nahodha
    Mambo yote huwa salama
    Mambo huwa ni salama Bwana Yesu akiwa ni Nahodha
    Huyu ni Nahodha mwenye uzoefu mkuu
    (Mikononi mwake)
    Mikononi mwake chombo huwa salama.
    (Usiwe na shaka)
    Unawezamwamini maana chombo hakijawahizama Akiwa ni Nahodha
    (Akiwa ni Nahodha..)
    Mambo yote huwa salama
    (Bwana akiwa chomboni)
    Mambo yote huwa salama
    (Weka tumaini lako kwake)
    Mambo yote huwa salama.
    Luka 8:22-25
    [22]Ikawa siku zile mojawapo alipanda chomboni yeye na wanafunzi wake, akawaambia, Na tuvuke mpaka ng’ambo ya ziwa. Wakatweka matanga.
    [23]Nao walipokuwa wakienda, alilala usingizi. Ikashuka tufani juu ya ziwa, chombo kikaanza kujaa maji, wakawa katika hatari.
    [24]Wakamwendea, wakamwamsha, wakisema, Bwana mkubwa, Bwana mkubwa, tunaangamia. Akaamka, akaukemea upepo na msukosuko wa maji, vikakoma; kukawa shwari.
    [25]Akawaambia, Imani yenu iko wapi? Wakaogopa, wakamaka, wakisema wao kwa wao, Ni nani huyu basi hata anaamuru upepo na maji, navyo vyamtii?
    Artist: Dodoma Adventist Chorus
    Song Title: Nahodha
    Audio Mixing and mastering: Job Music
    Video: RJ Studio (Mr RJ)
    Email: dodomaadventistchorus21@gmail.com
    CONTACTS
    +255 746 698 570
    +255 622 309 142
    You can also find us on:
    audiomack.com/...
    Instagram
    / dodomaadventistchorus
    and all other digital platforms for audio.

КОМЕНТАРІ • 215