WAZIRI MKUU AKUTA MADUDU BWALO LA MILIONI 774, AMSIMAMISHA KAZI MHANDISI "MKURUGENZI MSTAAFU AITWE"
Вставка
- Опубліковано 5 вер 2024
- Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ambana Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo kushindwa kusimamia matumizi ya Fedha ujenzi wa Bwalo shule ya Sekondari ya Wasichana Lugalo ambayo ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa shule hiyo
Ashangazwa kutumika kwa fedha yote ya ujenzi wa Bwalo lakini mpaka sasa halijakamilika.
Bwalo hilo lilipangiwa sh. milioni 774 na wamekwishatumia sh. milioni 341 hadi kufikia hatua ya linta ambayo ni sawa na asilimia 40 ya ujenzi wake.
Aagiza asimamishwe kazi kupisha uchunguzi, yumo pia Mkurugenzi Mstaafu wa Halmashauri aliyestaafu mwezi Aprili mwaka huu, ambapo Mheshimiwa Majaliwa aagiza aitwe na ahojiwe.
Mheshimiwa Majaliwa yupo mkoani Iringa kwa ziara ya kikazi.
Napenda sana Waziri Mkuu anavyofanya kazi, hivi ndo mawaziri wote wanatakiwa kufanya, hii nchi inatakiwa upelekwe hivyo, nipeni miezi 6 tu nisimamie engineers
Jukumu la ujenzi wangepewa JKT hao jamaa wanakula sana pesa za serikali wanaturudisha nyuma
Asante Mh,Waziri,kodi zenyewe tunalipa kimaumivu sana,mpaka vimitaji vimepukutika,halafu wao michenji kibao wanaficha mifukoni mwao.
Asante yako haisaidii tatizo watanzania wenyewe hawamjui adui yao
@@nsajigwamwakalonge5702wewe unemjua usiingilie Uhuru wa Maoni ya watu huo ni Mtazamo wako Wala sio uhalisia uliopo haya mambo sio Kama wewe unavyofikili labda ungekuwa uliwahi hata kusimamia mradi hata wakwako tu ndio ungejua haya mambo lakini huku kupingapinga tu mladi haki unayo na Uhuru wa Maoni
We ujielewi unashukulu kwa kip tangu Waziri anasema kunamabadiliko?na kwanini yanajiludia kilasiku
Majaliwa Nakuamini sana, sina shaka na uzalendo wako ulio tukuka
Kazi nzuri PM
Kazi za serikali ni za ajabu sana,kwanza watumishi wake HAWAJUI kufanya kazi ndani ya Muda na KUOKOA Muda hawajui
😮safi sana wanyooshe hao
Pole sana eng Emmanuel sigachuma, ila mungu yupo tutakuombea. Nimesikitika sana ila mungu yupo.
Pole sana Engineer Sogachuma, kwa ninavyokufahamu hapo umetwishwa mzigo ambao sio wako, ila alikuwa anasema hakuna store ni kama has a worst plan to spoil your character and position
Mungu akupe umri mkubwa pm na hongera sana
Wote hao ni wezi tu wangekuwa wanatenda haki wangewaambia pesa zote waziludishe,.ukishawasimamisha hizo pesa ndo zinludi?
Watanzania wenyewe hawamjui adui yao kazi kusifia tu unadhani yeye siyo mwizi!
Huyu jamaa noma sana 6:11
Muheshimw ttz hil litakuw endlevu,kwa sababu kweny hz sekta kuweka w2 ambao awana uchungu n hil taifa ila wanacho jali n m2mbo yao,bila kuwafunga Hawa au kuwataifisha itakuw saw n bule
Huyu jamaa noma sana
MUNGU Akubariki Sana Mheshimiwa Waziri Mkuu DAMU ya YESU Ikufunike. Simamia Haki
Yesu yupi nchi imejaa uwizi
Damu ya marehemu Nabii Yesu bado haijakauka.ndugu yangu?
Majaliwa sio mkristo hiyo damu ya yesu haimuhusu kijana.
@@Ali-nl2du uyu sio Muhammad ambae anakaburi,, yesu Hana kabur,, nyie komaeni na nguvu ya subiani, SS tuna nguvu ya damu ya yesu, na inatenda kazi
Kamwombea km waziri mkuu wake,, ajamuombea km kassim majariwa,
Apo sawa mazee
Hii ndiyotunataka wananchi siyoo watu wale tu pesa za walipakodi safii sana mama waache hawa wawatie adabu hawa watu bila ya hivi nchi aiyendi
Safi sana
MAJALIWA MUNGU AKUJAILIE NAKUOMBEA 2030 . Ugombee uraisi
😅
2025 bana
2025🎉🎉
@@LeonardmpembaMsemakweli-q8s una uhakika atatoboa hadi huo mwaka?
Hivi kwa nn tunafanya hivi jmn watumishi daaa yaani kila kona ya nchi hii hakuna sehemu salama, watu wanalipa kodi jmn kwa kujinyima TRA wanawafungia biashara zao Lkni watumishi wa serikali wanachezea pesa hovyo jmn hebu Watanzania tuache jmn haya mambo. Hawa viongozi watakuwa wanafika kila sehemu jmn? Pongezi waziri Mkuu Mi nakuaminia wewe na Mh Makonda mnafanya kazi, halafu hapo hapo unakuta mtu anasema oh watumishi wanadhalilishwa, je wananchi hawadhalilishwi kwa kuliwa pesa zao?
Wameshayatimba hukoo😂😂😂😂
Mnasimamia haki dakika za mwishooo tunaijua hiyo saiv wajifanya mko active😊
Ndomaaan watanzania awapewi kaz nje ya nchi kwa upuuzi kama huuu
Tzd wapigaji wengi yaani hao wote wapigaji na wesha zipiga hizo pesa. Takukuru wafanye kazi zao.
Safi sana mkuu
Watanzania wanyonge mungu anaona IPO siku atatukomboa tuu.
Maguliwa hoyee
Engineer anatwishwa mzigo usio mhusu........Manunuzi na Mkurugenzi
Hapo hamna kitu
Hii nchi inachezewa sana
Bahati nzuri hakuna tumbua tumbua😂😂😂
ila nchi yetu ina vituko sana ,yaani hawa viongozi wa kuteuliwa wanaturudisha nyuma sana ,ni bora mchakato mwingine uwepo wa kupata viongozi wazuri ,ikiwezekana nao wafanyiwe mchujo yaani usaili,awe injinia ,mkurungezi afisa elimu wote waombe kazi na wawajiwe usaili na bodi husika nahisi tunaweza pata viongozi waadilifu...kila mtu ni mpigaji..tu
Huyo Majibu ya muhandishi ni tata haukuna kitu hapo ,ondoka nae
majizi
Du hali ni ngumu sana
Nchini China pamoja na Vietnam watumishi wa umma kama hawa hukumu yao ni kunyongwa.
Hawa watu wangekuwa wanarudisha fedha na wananyongwa
Mmmh Bilioni 3 .....zimekwenda daaah ! Mwisho wa siku ni kwenda kukamua wamachinga walipe kodi .....daaah 😢😢 ! Mbona Hizo wanazoiba hawarudishi wanaishia tu kusimamishwa kazi ? Pesa nyingi zinaliwa ! Kwenye Masoko ,Minada kote kuna makusanyo ila hela inaliwa haifiki serikali kuu ! Mfano kwenye mnada wa ng'ombe na mbuzi kwenye vijiji kwa siku moja kinachokusanywa inaweza kufika hadi 10M kwa siku moja tu ! Ila utakuta Shule ya msingi choo hakuna ,Zahanati haina Dawa,Maji hakuna ..... ! Hii ndio Tanzania 😊
Na kukopa mikopo kumbe hela zinaisshia kwenye mifuko ya watu
Hao bd
Wizi,wizi,kira Ofisi ni Wizi mtupu..Kwanini Hatuwezi kujenga Nchi yetu pasipo dosari.....
Hiki mm ndo kinachoniuma rais anakopa ela Ila wanashindwa kuzisimamia wanakuja kusituka watu wameishamaliza ela alaf unakuta limtu et anaupiga mwingi ovyoo angekua anko magu hao maji Leo wangeita ma mungu ailaze roho ya magufuli mahali pema pepon Amina
Heee pungua tena
Tatzo lipo na rais wetu anasema kulen kidogo msile sn
ASANTE Waziri Mkuu na Pole kwa KAZI ngumu ya kuthibiti ufujaji holela wa hela ya Serikali ambayo ni Kodi ya Watanzania Baadhi ya Watendaji waliopewa dhamana ambao ni wezi wa mali za Umma ni mzigo kwa Taifa.
Kazi ya uchawa tu..Mama Samia Mama Samia kazi ahaaaa!!!!!
@@festohaule9716 wewe ndio mchawi sasa, sijui ni wale chagadema naona.
@@MilloWamilonga-ft8ir Kazi yenu ni uchawa tu..ety Madawati mpaka aje Waziri Mkuu shenzi ..Mkoa unalundo la Viongozi!!!! Kama wewe unapendezwa na tabia za kifasadi wewe ni Zezeta shenzi!!!!!
@@festohaule9716 tuamsifia makengeza mbowe mwenye saccos binafsi.
Lissu na wengine ni vidampa tu.
Halafu katiba mpya shwaini.
Miaka 34 m/kiti ndio yeye tu kwa kisingizio cha utithi kutoka kwa baba mkwe Mtei fankulo
@@MilloWamilonga-ft8ir Mbowe anakusanya Kodi wapi!!! Mazezeta bhana!!!! Kusifia tu Madawati tu kukagua mpaka Waziri Mkuu wa Nchi ety!!!! Uozo mtupu..ni aibu kwanza .vitu vya kufanya Mtendaji wa kati aje Waziri Mkuu ety!!!!
@@festohaule9716 kumbe hujui, kuna ruzuku kibao hutumwa kila chama cha upinzani na saccos ya mbowe inaongoja.
Anashindwa hata kutoa panadol yeye na mikutano tu kuwazuga wenzake.
Usisahau makengeza ni mlambaji mzuri wa asali kutoka ikulu.
Ww chelewa tu.
Dah pesa nyingi imetoka lakini wapi...
Iv hapo cjaelewa jmani/ni bilion mia saba au mialion mia saba
Kasm majaliwa majalia rais wa jamuhuli yamuungano wa tz kila mtanzania atafrai sana tena sana atapita bila kupingwa namtu yeyote tunaamin munguyuo ipo skumoja atakuwa
Safi san na ndio maana nasema serikali ianze kwa kudhibi upotevu wa fedha si kila cku kutuanzishia kodi mpya watu wanaumia mno...Ripoti ya CAG ifanyiwe kazi kila mtu alipe
Serikali ipi sasa!izuie uwizi
Kuleni TU hii nchi IPO siku mungu atatupa raisi kama magufuri.na wazili wake majaliwa.
@@user-qm3hb4sz7y wewe ndio mpumbavu halafu kichwa chako kimejaa mavi ya kuku.
Yaani muuwaji, utawala wa mkono wa chuma, na udikteta irejee?? Fala sana bwamdogo wewe.
Ni wapi hapa
Changamoto kubwa sana
Hii namna ya ununuzi wa Tanzania mnatakiwa mkae muumize kichwa mno mbadili namna la sivyo hii nchi itabaki chini miaka yote sijajuaga mpk nimeingia ktk mfumo huu yaani watu wanajiongezea humo balaa , watu wanapiga mno kwny hii miradi wakirugenzi ndo mamamaaa aisee !! Tafuteni namna aisee laa !! Sivyo tutaumia na nchi itabaki chini miaka yote .
Hapa ni mkoa gani jaman
Tunaomba.ukumu yake if anyike haraka Kam ilivokuwa kwa yule jamaa aliechoma picha ya mama..Ili haki itendeke
Hivi mtu hats amekwapua tu bilioni 3, kusimamishwa kazi inamuathiri nini. Mi nilitarajia akamatwe na kushitakiwa.
Jamani watu mtakuja kuleta misiba isiyo ya lazima, hembu tazama sasa unaambiwa huna kazi ukiwa unatafakali hapohapo unaambiwa unakwenda mahakamani mtu hajafa tu hapo 😂😂😂😂
ata shule ya mama samia uku namtumbo niwiz mtupu akunamaendeleo yoyote
Sisi watu weusi tuna matatizo gani kwa nini hatuwaonei watu huruma tunao waongoza
Hawa watu wasiojali wananchi kwann wasifungwe maisha/wasinyongwe ili wengine wajifunze? Always hayahaya mambo mwisho wake hatuuoni ni kufukuzwa kazi tuu then wat? Kesho Lazima arudie mtu mwingine coz watu hawaogopi kufukuzwa ikiwa walichoiba kinaweza wasaidia kuendesha maisha. Huu ni ushenzi
Rais Samia anajitahd kutafuta fedha lakini wateule wake wanamwangusha😢
Yaaaan hawa watumishi wengine ni kama makondooo
❤
Saf wazri yani viongozi mgesimamiana kwa namnahiyo Tanzania tungekua mbari sana yani nchi imekua ni yawtu wachache tu na familiazao huku balabala maji vituo vya polisi sekta mbalimbali kumejaa matatizo na wazr mkuu ndy msimamiz mkuu tunaomba tusaidie na huku mlimba nako balabala baado hatuoni chochote kinachofanyika no janjajanja tu
Kukopa fedha sio shida,shida ni usimamizi wa fedha
Ifike mda tuanze kupigana risasi hadharani kwa wale wanaokula pesa za serikali
Serikali msipokuwa wakali...iii
Hizi ndio sababu tuna chukiaa kulipaa kodi ona ujinga wanao fanya milion 774 ni pesa inge weza fanya mambo makubwa sana ila wanaa tafuna
Wanasimamisha watu hewa, hakuna hata anaesimamishwa hapo
Waziri mkuu shida yenu hamja wahi waonyesha watu mfano. Unaiba mnachukua pension yake kama haitoshi mali zake na jela juu. Lakini kila siku eti takukuru. Halafu what. Tumewachoka sasa
Tunaombeni kazi jamani mbona mnatoa fedha nyingi hivyo?ndio maana wanajipigia tu. Nilishawaambia tupeni kazi sisi wakandarasi/mafundi local mbona hamuelewi?
They are not needed in development project plan
Baba Maja kamua baba
Kilolo we acha tu Kuna miradi ya maji pasua kichwa sana.mradi wa bilioni 1.5,hakuna mabirika ya kunyweshea mifugo.mabomba feki.
Ifike mahali wanaopewa dhamana ya miradi ya maendeleo kwa watanzania,ukomeshwe udhalimu na ubadhirifu wa fedha umma.
Bila kubadilisha mfumo mtaburuzwa sana
Wana lengo la kumhujumu Rais.
Kiteve huwezi sema hapo uwiiiii
Hv mradi kama huu mpka waziri mkuu ufike ndio uonekane wawakilishi wa rais walikuwa wapi kipindi chote hebu waanze kwa wateuliwa wa rais wa mkoa huo
Majizi yanafilisi nchi hii kama watakavyo
Hawa wasimamizi hawana kitabu chamanunuzi na matumizi, wameenda mikono mitupu,kweli hapo lazima hesabu zipoteane
Wezi hao wanajaza vitambi tuuu
there are times nashindwa kujizuia.... kuonesha vile nisivyokuwa muumini wa the so called *utawala bora* yaani hapo unahitaji kuwasikiliza viongozi waliolaza bilioni tatu hapo????
Swala sio kumsimamisha tu pia wakipatikana na hatia fedha za umma zirudishwe
YAANI TUTAFIKA MBINGUNI TUKIWA HOI SANA🥹
Tumbua
Mpe muda msikilize ili wajieleze vzr
Kiongozi kama wazir mkuu anapotembelea mradi anakua na taarifa zote kabla hajafka kwaio anajua hujuma zipi zinaendelea.
Walipe izo pesa kama kwa kutaifishwa mali ili siku nyingine wajifunze we unakulaje pesa zote izo na uoga huna Mxieeeeeew watu tunatoa makodi kila kukicha af nyie mzile tu bila aibu
mkuu tunakuombea san wamesha jisahau hao
Ushauliwangu kwa wazili mkuu wewesepanavioziwote wamkoa kwanimkuuwa mkoa anafanya kaziga mkuu wawila anafanyanini wotehao wanateni pasenti timua wakalime lakini hawawatu mnawafuga ndio sababu ya uozo wote huo
😡😡😡😡😡 wote wapigaji hata huyo Waziri mwenyewe , Mungu atawakata hata kama nikutoka kwa familia zenu. Eti amesimamiahwa kazi , yaani wameshazoea Iba utakavyo mwishoni huna adhabu yoyote zaidi ya kusimamishwa kazi uka enjoy pesa uliyoiba, yaani wanatuona wajinga 😢😢😢 endeleeni tu kushibisha matumbo yenu .
Leo naomba kuuliza wenzangu, hivi hawa wafanyakazi wakishafukuzwa kazi kuna hatua zinachukuliwa au ndo kashafukuzwa halafu basi??? 🥲
Wachache sana wanaochukuliwa hatuaa 😢, wengine wanapiga pesa wanasbiri kfukuzwaa tu
@@mwanaidimussa hapo hapajabadilisha chochote
Pamoja ni hiyo hela kupigwa bado pia na serikali ijitafakar yaani unatenga mil 774 zote kwa ajiri ya bwalo kweli??? Kwanini lisijengwe la kawaida halafu pesa zingine zitumike kununua vifaa vinginw vya shule au ata zipelekwe maeneo mengin kabisa penye uhaba
Hahahaha. 774M ni nyingi kwako tu hamna pesa hapo
Brother hatujengi ilimradi tuu Hilo jengo mbaka vitukuu vyako watatumiaa
Mlipomtoa Jafo tulijua hili litarudi!
Mama SAMIA SULUHU HASSAN uache kukopa.
Dhibiti Majizi yanayoiba pesa za serkali.
Majitu haya hayana na huruma na sisi watanzania Masikini mmnaotubana kulipa Kodi hafu yenyewe yanaiba pakubwa.
Unakopa nyingi yanatumia kidogo hafu yanaiba nyingi..
Haina haja ya kuendeleza kukopa mama yetu. Kama vipi myanyonge tuu
Dawa ni kugoma kulipa kodi
Engineer wanamuonea injinia anasimamia ujenzi na sio fedha hapo shida ni mkurugenz wamekuta tuu baba wa watu hajui kujielezea
Wakati wa kuidhinisha malipo injinia Kuna Saini yake, hata hivyo ndo maana unafanyika uchunguzi ili kama hakuhusika atarudishwa kazini
Huyu Engineer ni classmate wangu chuoni, siamini kama tuhuma hizo zinamhusu, kama wametumia 44% ya fedha tu tafairi yake hawajapokea fedha zote ila Hela zomekuja chache na team ya ujenzi ikaamua kuanzisha miradi yote Kwa pamoja pasi na kujali hii ni pesa ya bwalo au darasa
Wafukuzeni kazi wajinga wajinga woteeeeeeeeeeee Jamani wenzenu tumechoka kuona na kusikia wizi kila kukicha🥹🥹🥹🥹🥹
Chapa kazi nchi hii wahuni wengi kwa mambo ya kijinga bila kuona mbele huyu alipaswa kufungwa bila kusikilizwa