UKISIKIA MASIKINI JEURI NDO HII SASA

Поділитися
Вставка
  • Опубліковано 20 жов 2024
  • Mwanamitindo Naomi Campbell, amepigwa marufuku kushiriki kama mdhamini wa mashirika ya kusaidia jamii nchini Uingereza kwa kipindi cha miaka mitano. Hatua hii imechukuliwa kufuatia uchunguzi wa Tume ya Hisani ya Uingereza na ulioonyesha kuwa shirika lake la Fashion for Relief lilihusika na matumizi mabaya ya fedha.
    Uchunguzi huo ulibaini kuwa ni asilimia 8.5 tu ya fedha zilizokusanywa ndizo zilizotumika kusaidia misaada ya kijamii, huku kiasi kikubwa kikielekezwa kwenye malipo yasiyo halali kama hoteli za kifahari, sigara, na usalama wa @Naomi Campbell. Matokeo haya yalisababisha kufungwa rasmi kwa Fashion for Relief Machi 15, 2024, na Naomi Campbell aliondolewa kama mdhamini wa shirika hilo mwaka 2023.
    Aidha, wadhamini wengine wawili wa shirika hilo, Bianka Hellmich na Veronica Chou, wamepigwa marufuku kushiriki katika shughuli za kujitolea miaka minne na mwingine miaka tisa.

КОМЕНТАРІ •