'SABASITA' AKAMILISHA KABURI LAKE LA MIL.7, ASUBIRI JENEZA LA MIL.3.
Вставка
- Опубліковано 18 жов 2024
- Askari Mstaafu Patrick Kimaro, jina maarufu (Sabasita) ambaye ameandaa kaburi lake lenye thamani ya shilingi Milioni 7, amesema sasa ameshaweka oda ya Jeneza litakalogharimu shilingi Milioni 3, ambalo ameshalipia pesa nusu na kuandaa chumba maalum litakapohifadhiwa.
Sabasita amesema amechagua jeneza lake ambalo anahitaji kuzikwa nalo siku Mungu akiamua kuvuna mavuno yake na wosia uko hatua za mwisho.
Patrick Kimaro maarufu (Sabasita) ambaye alizaliwa Februari 2,1963, aliajiriwa Jeshi la polisi 1987, na amefanya kazi kwa miaka 36, ambapo amepitia vyeo mbalimbali na mpaka anastaafu Februari mwaka huu, alikuwa Supertandent of Police (SP).
#ITVDigital #ITVUpdates #ITVTanzania
Follow @radioonetanzania
Hongera baba, naamini hata kiroho unejiandaa vivyo hivyo. Mungu akujalie kifo chema.
Mimi nakuombea uishi maisha Mema wewe nijasiri kweli kabisa Mungu akubariki Sana babu hiyo ni jambo jema
Baba uko safi kabisa hata watoto wasigejenga kaburi hilo umejiogeza kwa kweli inaonekana kabisa wewe hukuonea mtu yeyote katika kazi yako ya Upolic tufauti na hali ya sasa
pesa za kishetani zinasumbua je umejianda na kiroho
Huyo ni freemason ameambiwa siku za kufa
Malimwengu Dunia na vijimambo kweli
AFE TUJE TUMVUWE VITU VYA THAMANI SUTI SAA NA VIATU TUNAZO HABARI VINAFIKA MILIONI 250 😂😂😂😂😂 KUFA HARAKA TUJE.
Sio rahisi lkn kama unavyo fikiria,,kaburi lipo nyumbani kwake,,,nasio makaburi ya umaa
tukiuza nyumba tunamuuza na yeye