Це відео не доступне.
Перепрошуємо.

Zuchu : "Nilipeleka Nyimbo Kama Tano, Diamond Alizikataa Zote" | SALAMA NA ZUCHU

Поділитися
Вставка
  • Опубліковано 16 жов 2022
  • #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
    Kuna usemi mmoja unaenda kama hivi, kulea mimba si kazi ila kazi ni kulea mtoto, tafsiri yangu naamini mhenga hapo alikua anatuambia kazi pengine inaanza baada ya kupata kazi, tunaelewa jinsi gani ambavyo kupata kazi huwa ni kazi. Tena kazi yoyote, haijalishi kama ni ya upishi au ulinzi au ufundi au hata u daktari, mi nawajua madaktari kadhaa ambao nao pia wanapata shida kupata hizo kazi. Na baada ya kupata shida zote hizo wakati wa kutafuta kazi basi kazi halisi huanza pale unapoipata sasa hiyo kazi yenyewe.
    Kazi ya Zuchu ilianza kabla hajaipata hiyo kazi yenyewe na ilikua kazi haswa kuipata na Mama yake Bi Khadija Kopa ndo alikua kinara kwenye hiyo connection ambayo Binti yake alikua anaitaka ili aweze kuwa msanii wa Diamond, na hayo ndo yalikua maneno yake hasa, toka alivyorudi kutoka Nigeria kwenye mashindano ya kusaka vipaji na alikua hajielewi elewi kwa kiasi flani ni kitu gani alikua anataka kufanya na kama basi kutakua na la kufanya inabidi liwe kutoka WCB na sio sehemu nyengine yoyote na agulia nini kilitokea? WCB aliipata na kilichokua kinatakiwa baada ya hapo ni UVUMILIVU wa HALI YA JUU.
    Kwenye vitabu vyangu vyote Bi Zuhura Othman Soud ndo muandishi wangu BORA wa KIKE kuwahi kutokea katika kizazi chetu hiki cha Bongo Flava, na naweza sema hivyo wakati wowote iwe usiku au mchana, kipaji hicho ndicho kilichonifanya mimi nistaajabu sana na kutaka kuongea nae na kumuuliza yote yale ambayo nilikua nataka kumuuliza, ingawa humo humo nilikua nishajijibu kutoka kwenye historia ya familia atokayo ingawa hiyo haikutakiwa ndo iwe lazima, lazima mtoto wa Khadija Kopa na Othman Soud awe muandishi mzuri maana wazazi wake wamejaa vipaji tena na Baba yake ndo muandishi mkubwa wa nyimbo nyingi za Mama yake zilizowahi kuvuma.
    Kwa umri wake wakati mwengine hujiuliza kajuaje haya maneno yote, anajua maana yake hii? Kasikia wapi hili neno au pengine je huwa anamfikiria Mama yake (ambaye ndo kipenzi chake na ndo amemlea) wakati anaandika hii? Anaona aibu? Je huwa wanaongelea hayo mashairi wanapokua wawili tu? Mazungumzo huendaje?
    Sasa turudi kwenye kazi hiyo ya kuanza kuifanya baada ya kuipata sasa WCB, ukiachana na msoto mrefu alopitia, WCB wenyewe walikua waangalifu sana kwenye mipango ambayo ilikua ikiandaliwa kwaajili yake, yeye ndo msanii wa KWANZA wa KIKE kuwahi kutokea kwenye label kwahiyo ukichana na kipaji pia uwekezaji wa hali ya juu ulitakiwa ufanyike and boy they did that. Toka single yake ya kwanza mpaka wakati naandika hii Zuchu hakuwahi kuwa na kazi chafu, album yake ya kwanza alotoka nayo ya I am Zuchu ilikua na nyimbo 7 ambazo zote zilienda kufanya vizuri, na mpaka leo kila wimbo ambao anaachia ni wa moto, tukisema namba moja nadhani namba zake pia zinasema hivyo za kila sehemu, hakuna chumvi yoyote ndani yake.
    Vipi sasa anaweza ku maintain hii schedule yake ilojaa mambo kuanzia asubuhi mpaka usiku? Kutoka Jumatatu mpaka Jumapili? Je ana muda kwaajili yake? Ana mpenzi? Mipango yake je? Endelevu? Vipi hizi title ambazo tunampa anazichukuliaje? Kuna pressure yoyote? Na kuhusu familia je? Kuna pressure yoyote kwenye baadhi ya mambo na maamuzi? Na kwenye label nako? Watu na furaha na kazi yake?
    Kwa kuanzia msimu wetu wa TANO nadhani introduction ya Ms Zuchu inatufaa sana na yangu matumaini uta enjoy pia.
    Asante kwa support ya toka siku ya kwanza ulipoanza kutupa macho na masikio yako.
    You’re the best, nakukumbusha tu kwamba mengi yajayo yatakufurahisha In Shaa Allah maana kazi ndo kwaanza imeanza.
    Love,
    Salama

КОМЕНТАРІ • 171

  • @elizabethmapunda
    @elizabethmapunda Рік тому +17

    Napenda zuchu anavyoongea very charming😍

  • @handwatchmaro4124
    @handwatchmaro4124 Рік тому +11

    Leo nmejikuta nampenda Zuhura😍 zaidi ya Zuchu

  • @zamzamsharif9776
    @zamzamsharif9776 Рік тому +14

    ILike her she’s down to earth. Loove from Ireland 🇮🇪 ❤

  • @hamismkude553
    @hamismkude553 Рік тому +7

    Nawakubali sana zuchu na salama kila mtu ana play party yake vzr yaan salama anajua kuuliza maswali na zuchu anajua kujibu maswali

  • @nurutatu4031
    @nurutatu4031 Рік тому +44

    One of the best interviews ever. Keep it up Salama and Zuchu👏🏽

  • @chancystv3138
    @chancystv3138 Рік тому +144

    Watu wa Zuchu gongeni like hapa 🙌

  • @BigZhumbe
    @BigZhumbe Рік тому +16

    Zuu you are great 🔥🔥🔥🔥🔥🔥🔥 simba jike umebebwa ukabebeka hadi wasafi waliokubeba wanaijoi na mashabiki tuna have fun.

  • @rosemahenge9071
    @rosemahenge9071 Рік тому +36

    Hakuna kitu kizuri kama kuangalia interview ya mtu mchangamfu kama Zuchu 🥰🥰🥰

    • @kantai737
      @kantai737 Рік тому +3

      For real her interviews are always a vibe Na she is really intelligent everytime ukiskia interview zake u can’t help but love her more.

    • @BigZhumbe
      @BigZhumbe Рік тому +4

      Mimi interview hata iwe masaa kumi naimaliza.... Yeye na Simba they are great kwenye interviews

    • @MrTop-wj7no
      @MrTop-wj7no Рік тому +1

      @@BigZhumbe umepatia kabisa

    • @isharsalim454
      @isharsalim454 Рік тому

      🥰🥰

    • @mamananga2849
      @mamananga2849 Рік тому +1

      @@BigZhumbe sanaaa

  • @rehemaothman2475
    @rehemaothman2475 Рік тому +11

    Majibu ya ukomavu nakukubali zuchu🥰🥰🥰🥰😍

  • @hadijasalim7769
    @hadijasalim7769 8 місяців тому +2

    Zuchu hadi umeniliza mamy nakupenda❤❤❤❤

  • @keyla3641
    @keyla3641 Рік тому +15

    Zuchu akili nyingi usibadilike u are a good girl

  • @sarahlondo7597
    @sarahlondo7597 Рік тому +23

    Aaaaw i love the way she is real❤️‍🔥🥰

  • @deborahcharles4916
    @deborahcharles4916 4 місяці тому +3

    I love you zuchu haulingi dada

  • @nyanziratatou5404
    @nyanziratatou5404 4 місяці тому +1

    Ici kibindi nakipenda kwasababu hakina ushabiki kwata kwenye masali maswali yanaoulizwa yanajitosheleza . Kwakweli napenda da Salama.❤

  • @maijamtoso5673
    @maijamtoso5673 Рік тому +17

    Interview Nzuri mno.. inafurahisha na kufunzaa

  • @mohamedrajab358
    @mohamedrajab358 Рік тому +14

    Huyu binti yupo vizuri mno kwenye kichwa chake

  • @mariammbaruk8034
    @mariammbaruk8034 Рік тому +12

    Niliisubir xanaa hii zuchu love u😘😘

  • @diva_20162
    @diva_20162 3 місяці тому +1

    Her voice God waoooh so wonderful 😊😊

  • @estherjackson6038
    @estherjackson6038 Рік тому +4

    Jamani mi naona maneno hapo juu nyuma ya Zuchu,KumaNoko Kula, au sioni vizuri.

  • @fortune3502
    @fortune3502 Рік тому +8

    Interview nzuri sanaaa! Daa nimekapenda bureee katoto ka watu jaman

  • @jacintabati6238
    @jacintabati6238 Рік тому +7

    ZUCHU my love🥰😘😍❤❤❤

  • @goodlucksway1456
    @goodlucksway1456 Рік тому +7

    👏👏👏yuko positive sana zuchu kama zuchu

  • @SultanDean
    @SultanDean Рік тому +18

    Salama be asking all the right questions

  • @djibrilheradi8291
    @djibrilheradi8291 Рік тому +4

    Happy for you zuchu,may Allah protect you

  • @elizabethotieno7270
    @elizabethotieno7270 Рік тому +7

    Best interview ever,,,this girl is beautiful and wise

    • @hadiadaoman1981
      @hadiadaoman1981 Рік тому +1

      Exactly even me I love her much more ♥️❤💖🥰

  • @stellah3844
    @stellah3844 Рік тому +12

    Nakupenda Zuchu💓💓💓

  • @dayannahkopellah8396
    @dayannahkopellah8396 Рік тому +18

    She is clever😇

  • @allymakangana6450
    @allymakangana6450 Рік тому +10

    salama ni muwazi sana sio mnafiki

  • @eveodera6676
    @eveodera6676 Рік тому +1

    Salama this is one of the best interviews. I love the way your calm and Zuchu is just awesome.

  • @kantai737
    @kantai737 Рік тому +26

    You just can’t stop loving her❤

  • @violetandisi
    @violetandisi 8 місяців тому

    i just love salama for some strange reason she is so real i mean she asks the correct questions in a polite manner and zuchu love the energy girl and the wisdom

  • @claricejoshua820
    @claricejoshua820 Рік тому +2

    She is very humble nimempenda

  • @sebastianmwakulya8146
    @sebastianmwakulya8146 22 дні тому

    Nimeangalia tena na tena hongereni sana kwa interview

  • @princessiyalicious4185
    @princessiyalicious4185 Рік тому +13

    Yeeee wakwanza mm leo

  • @hopedj275
    @hopedj275 Рік тому +27

    one of the best interview i have ever seen in my life

  • @monicajohn2515
    @monicajohn2515 Рік тому +2

    Yani salama ana bonge la interview saaaana big up salama

  • @africanbeauty6556
    @africanbeauty6556 Рік тому +26

    Proud of you Zuchu!! Keep it up don’t change 🥰

  • @salimdibundile4872
    @salimdibundile4872 Рік тому +6

    Salama you are the best...
    Tunakuomba utuletee kipenzi chetu mbosso khan

  • @keyla3641
    @keyla3641 Рік тому +5

    Hahaha nimeinjoi sana asante salama

  • @lulumalima1739
    @lulumalima1739 9 місяців тому

    Nice much love and prayers from fellow Tanzanian women both you ladies

  • @kellymutabesha1876
    @kellymutabesha1876 Рік тому +20

    Katoto kana akili mingi njomana simba kadata

  • @MrTop-wj7no
    @MrTop-wj7no Рік тому +5

    Interview nzuri Sana Kwa kweli,

  • @loiceamugune6711
    @loiceamugune6711 Рік тому +3

    Salama you are one of the best interviewer

  • @lynawamahoro3465
    @lynawamahoro3465 Рік тому +4

    I like … wise one 👏

  • @jessicahjohnstone7229
    @jessicahjohnstone7229 Рік тому +6

    Best interview

  • @matanohassan9667
    @matanohassan9667 Рік тому +3

    Nakupenda zuchu

  • @jabirsuleiman26
    @jabirsuleiman26 Рік тому +9

    I like it 🎉

  • @vanessaphamarcy2134
    @vanessaphamarcy2134 Рік тому +6

    Nimekupenda buleee unahekima kaza but

  • @zhaujiakashindi6617
    @zhaujiakashindi6617 Рік тому +1

    🥰😘Love you Salama❤️

  • @Jaycollection
    @Jaycollection Рік тому +6

    Interview nzuri sana

  • @shilahshilah6136
    @shilahshilah6136 Рік тому +2

    Mie ni mkenya lakini nampenda zuchu sana,,,,ningepewa nafasi nimuone tu ningeshukuru

  • @johariasanimatu2732
    @johariasanimatu2732 Рік тому +3

    Zuchu my blood 🥰🥰🥰

  • @gknifeboy9435
    @gknifeboy9435 Рік тому +3

    Gud interview

  • @dilipdab3714
    @dilipdab3714 Рік тому +5

    English.ipo.poa.lakini.salama.yupo.fresh

  • @blandinamyinga9489
    @blandinamyinga9489 Рік тому +7

    Salama with her trick questions eti kwa vile SIMBA aliruka na wanawake wengine ukiwa na mimba 🤣🤣🤣🤣

  • @kimah9461
    @kimah9461 Рік тому +14

    Ikitajwa diamond platnumz zuchu ni mgin🙈🤣👏🤣🤣🤣Is all❤️ beautiful MashaAllah Keep going sis

    • @kantai737
      @kantai737 Рік тому +1

      😂😂😂😂😂

  • @yvespungu3611
    @yvespungu3611 Рік тому +2

    Nice interview

  • @esthermusanga8118
    @esthermusanga8118 Рік тому

    Also me I wish you all the best

  • @rosemarysiame8443
    @rosemarysiame8443 Рік тому +1

    Jamn jaman this was funny jamn if you have crush with someone ooooh my god it's very jamn kafeeling kale duu

  • @ismailebani5262
    @ismailebani5262 Рік тому +3

    Safi Zuchu

  • @TheMullins830
    @TheMullins830 Рік тому +1

    This girl just has some good energy in her. She sounds so sincere when she speaks.

  • @suroorAlafifi-ve8pk
    @suroorAlafifi-ve8pk Рік тому +1

    Will see beautiful woman and I amazing thang 🥰 the best way to be careful about it and nice 🙂

  • @marianusrutagwelera3013
    @marianusrutagwelera3013 4 місяці тому

    Nice sr zuchu😮

  • @nyotakaminkya714
    @nyotakaminkya714 Рік тому

    J'aime tes paroles ina saidia mipango iliko kichwani

  • @abdulraufmohammedsalum6806
    @abdulraufmohammedsalum6806 Рік тому +5

    Salama🙌

  • @aslayhassan2283
    @aslayhassan2283 Рік тому +1

    I like it

  • @remybuyenzi1856
    @remybuyenzi1856 Рік тому +7

    ❤❤❤❤

  • @arnoldmangi2407
    @arnoldmangi2407 Рік тому +3

    Iko poa sana

  • @vincentmushi1247
    @vincentmushi1247 Рік тому +44

    Ukisikia watu wanalalamika kuwa eti Mtu Anaongea kiingeeza wakati wa interview... Ujue hao watu hawajaenda shule...hahahaaaa, Kama unaelewa hauna muda wa kulalamika.. Ndio kiswahili ni lugha yetu na kiingeeza ni lugha pia... Nendeni tuition mkavunje yai jamani

    • @jasmineedamu6089
      @jasmineedamu6089 Рік тому +2

      Achana na sisi😏

    • @fatmazullu4933
      @fatmazullu4933 Рік тому +1

      @@jasmineedamu6089 🤣🤣🤣🤣

    • @minzamariamcasmir189
      @minzamariamcasmir189 Рік тому +2

      Kweli kabisaa….watu wanabidi waelewe she’s an aspiring international artist if not one already so she needs to be accessible to everyone

  • @lareineminah1353
    @lareineminah1353 Рік тому +5

    Mme kawiza kuyitowa
    La simba lisha kuwa waziiii🤣🤣🤣

  • @mohamedjuma1878
    @mohamedjuma1878 Рік тому +5

    Ma Ami Leo mmekutana

  • @oxtinho159
    @oxtinho159 Рік тому +6

    Wa kwanza

  • @mariamandambike5013
    @mariamandambike5013 29 днів тому

    Zuchu🔥🔥

  • @NabakiZanzibar
    @NabakiZanzibar Рік тому +3

    Kuipata hii ni bahati sana,

  • @stephanocyprian2892
    @stephanocyprian2892 Рік тому +2

    Pamojasana zuch

  • @nelialomnyaki
    @nelialomnyaki 2 місяці тому

    Nimependa kingereza cha zuchu

  • @veronyanganda179
    @veronyanganda179 Рік тому +12

    Mafanikio ya zuchu nyuma yake kna watu sahihi wa kwanza mama yake, na mpenzi wake daimondi.

  • @maulidmalik5364
    @maulidmalik5364 Рік тому +2

    Jaman sjaona msosi leo

  • @esthermbike3300
    @esthermbike3300 Рік тому +7

    Wema sasa

  • @mwanatz5980
    @mwanatz5980 Рік тому +10

    😍😍😍

  • @fatmasaid3536
    @fatmasaid3536 Рік тому +8

    Kwajili ya kiki, she's been trained ili atakapo ulizwa kama anam date simba ajifanye shy ili ionekane kuna something kwa mtazamo wangu hamna lolote ila kiki tu.

  • @KSJ6569
    @KSJ6569 Рік тому +3

    Iyi nimarudiyo sio mpya

  • @esthermusanga8118
    @esthermusanga8118 Рік тому +1

    👋👋👋👍

  • @AfricaYangu
    @AfricaYangu Рік тому +5

    All went well until u ask her about Diamond that's when she started behaving like a little girl

  • @donraykiko4243
    @donraykiko4243 Рік тому +2

    Kwaiyo kiswahili mpemba kinampiga chenga au ndo tunakomoana tu

  • @mosah2851
    @mosah2851 Рік тому +2

    Zuchu anasauti huyu mtoto!!

  • @vincentmushi1247
    @vincentmushi1247 Рік тому +15

    Interview nzuri... Na hongereni wote... Zuchu Aka chuchu... Hapo kwenye ku date na simba... Hahahaaaa.
    Ni Swali gumu sana... Biggest mistake... Zuchu ni mtulivu lkn simba wetu bado ni kicheche.

  • @husseynomar9523
    @husseynomar9523 Рік тому

    Salama tafadhali tuleteeni SHEIKH MUHIDDIN MAALIM SIASA NA SABRA MACHANO WATU ZANZIBAR

  • @AllyForyour
    @AllyForyour 6 місяців тому

    Lafudhi ya zuchu❤❤❤

  • @ZuwenaZuwena-oe9kk
    @ZuwenaZuwena-oe9kk 3 місяці тому

    Jamani.mmeonavia2.vyadadae2.zuhura😂😂😂😂

  • @judithjulius5993
    @judithjulius5993 Рік тому +2

    Kato kadogo lakini kanaongea point tupu

  • @kidungweshaaban9317
    @kidungweshaaban9317 Рік тому +2

    hujampa hat juice why!?our zuchu!!

  • @damariszuckschwert9489
    @damariszuckschwert9489 Рік тому +4

    Hawa mababa wengi ni nyoko kabisa.

  • @mvponlinetv
    @mvponlinetv Рік тому +2

    Ivi nyinyi wa sanii wa tanzania ndio hamuwezi kuongea bila yakuongea English au inakuwa nihashuo tu

  • @lissaseif4744
    @lissaseif4744 Рік тому

    Weeeeee mbn umeliwa sasa

  • @yusternyirenda7231
    @yusternyirenda7231 7 місяців тому

    Dalili zote zinaonyesha zuchu analala na diamond tena kwa asilimia elfu niko paleeeeeee! mapenzi! huwa hayajifichi ipo siku watashindwa kuendelea kuficha 😂😂😂

  • @ashahamisi5884
    @ashahamisi5884 Рік тому +1

    Leo sema no no lakini ipo siku utasema yes . Huwezi kuzuia mahusiano kamwe kua siry ficha social media tu.

  • @Dotto-hp3qf
    @Dotto-hp3qf 7 місяців тому +1

    Ni nyimbo alikuwa anaipenda..na aliiagwa nayo. Ni nyimbo ya kumbukumbu kwako

  • @anitakamene4656
    @anitakamene4656 Рік тому +2

    Nice

  • @dayannahkopellah8396
    @dayannahkopellah8396 Рік тому +5

    🤣🤣🤣