Hawa ndio Waliodhulumiwa roho zao 1972, nchini Zanzibar

Поділитися
Вставка
  • Опубліковано 28 вер 2024
  • Mnamo mwishoni mwa mwaka wa 1970, Serikali ya Mavamizi ya Zanzibar kama kawaida yake iliwakamata wananchi wengi sana kwa singizio lao hilo hilo la kila siku "kutaka kuipindua Serikali ya Wananchi"!!
    Miongoni mwa waliyokamatwa wakati huo, walikuwemo, Mabwana hawa:
    Salim Ahmed Busaidi
    Abdalla Suleiman Riyami
    Othman Soud
    Azizi Bualy
    Hemed Said
    Mohammed Juma
    Mohammed Hamza
    Musa Ali
    Said Hamoud.
    Wananchi hao baada ya kukamatwa na kuwekwa kizuwizini, walipelekwa mbele ya mkutano wa hadhara uliyoandaliwa makusudi kwa ajili yao katika uwanja wa Maisara, Unguja, kati ya mwaka wa 1971. Serikali ya Mavamizi ya Zanzibar, kwa kutaka kudanganya Ulimwengu na wananchi wa Zanzibar, walileta katika mkutano huo bunduki na silaha nyengine ndogo ndogo kuwa ati wamekamatwa nazo wananchi hao.
    Pia pamoja na hizo silaha, ililetwa bendera na kusemwa kwamba bendera iyo ndiyo
    walitaka wakamatwa hao iwe bendera ya Nchi baada ya kufuzu hayo mapinduzi yao! Hayo hayakutosha, bali Serikali ya Mavamizi, iliwatumilia baadhi ya maofisa wake wa kijeshi wengi wao wakiwamo hao wenye kujiita, "progressives" kuja kusema uwongo wa kuwahilikisha wananchi wenziwao kwa ajili ya
    kutafuta maslahi ya nafsi zao. Maofisa hao waongo, walisema mbele ya umma kuwa ati hao wananchi waliokamatwa walikuwa wakipanga pamoja nao mipango ya kuipindua Serikali ya wananchi.
    Bali wao, yaani hao maofisa waongo, walikuwa wakiripoti kwa wakubwa wao kila khatua zilizokuwa zikifanyika. Mpaka ulipofika wakati, ndipo ilipoarifiwa Idara ya Usalama na kutakiwa wafanye kazi yake. Idara ya
    Usalama iliwakamata wote pamoja na silaha zao ambazo ndizo hizo hapo!! Kilaaliyekuwepo katika mkutano huo na kila aliyesikia hadithi hizo, ila aliyekuwa hana akili timamu au amezidiwa na chuki, aliweza kutambua kuwa yote hayo yalikuwa ni mazingaombwe ya uwongo uliyokuwa umepangwa na baadhi ya wakuu maalumu wa Serikali ya Mavamizi kwa makusudio yao maalumu.
    Baada ya kusemwa uwongo huo, Karume aliwasimamisha baadhi ya hao wadhulumiwa mbele ya umma uliokuwepo hapo na aliwanazii kwa matusi, na aliwakejeli kwa kiasi alichopenda mwenyewe. Baada ya hapo, alitoa hukumu ya kuwaweka gerezani. Kazi zao alizokuwa amezitangaza mbele ya mkutano huo, zilikuwa za "Kuchunga n'gombe" huko Hanyegwa Mchana. Baada ya kuuliwa Karume, April 7, 1972 na kutawalishwa AlHajj Aboud Jumbe, wananchi hao wadhulumiwa, wote walichukuliwa kutoka magerezani na kwenda kuuliwa kwa kupigwa marisasi siku moja. Baada ya kuuliwa, wote walitumbukizwa katika shimo moja.
    Yale yaliyofanyika hivi karibuni huko Ruwanda si ajabu kuwa wameyaiga kwa yaliofanyika Zanzibar. Kuiga maovu ni rahisi! Baadhi ya hao maofisa waliokubali kusema uwongo kuwazulia ndugu zao wakati huo, hivi sasa baada ya kuwa na wao yeshawafika ya kuwafika kwa matokeo ya kuuliwa Mzee Karume, ati ndio wanasema kwa
    sauti za majuto na za kusikitika kuwa, "Yale yote tulioyasema siku ile mbele ya mkutano ule yalikuwa ni maneno ya kupangiwa na wakubwa wetu tuyaseme, kwa hakika yote yalikuwa ni maneno ya uwongo"!!
    Hao ndio "progressives" wetu, wapenda maendeleo. Wametumiliwa kuivamia Serikali ya halali iliyochaguliwa na wananchi kwa uchaguzi wa kidemokrasi wa "One Man One Vote". "Progressives" hao hao ndio waliotumiliwa kwa maslahi ya nafsi zao kwa kusema uwongo uliopelekea kuuliwa kwa
    wananchi wenziwao bila ya kuwa na makosa yoyote. "Progressives" hao hao ndio waliotumiliwa tena, mara hii katika mipango ya kumuuwa Karume!! Si ajabu kuwa hivi sasa "progressives" hao hao wamo mbioni wakitumiliwa, wakijuwa au bila ya kujuwa, katika mipango na njama za kuleta vurugu kupitia huu "Mfumo wa Vyama Vingi" tulioletewa, bali na katika mengineyo. Watu kama hawa khatari kuwanao.
    Daima yafaa kuepukwa. #HistoriaYaZanzibar

КОМЕНТАРІ • 18

  • @SKY-fk3fz
    @SKY-fk3fz Місяць тому

    So sad

  • @harithmohd6318
    @harithmohd6318 4 місяці тому +2

    Wanzanzibar leo et mnasherekea siku ya mapinduz hamjui kuwa siku hiyo zilipotea roh za watu tena waislam wenzetu ndio walouliwa mujuwe t mukisherekea bc munasherekea damu za watu namutawalip zoho zao sk ya sik

  • @mbarakkhamisali
    @mbarakkhamisali 11 місяців тому +1

    ALLAHU AKBAR

  • @OmarMohamed-zf8dp
    @OmarMohamed-zf8dp 2 роки тому +1

    ulikuwa kwa upanga utakufa kwa upanga ndiomaneno mazito ya qanitukufu

  • @wahdabintabilha3643
    @wahdabintabilha3643 4 роки тому

    Innalillah Wainna Ilaiyh Raji'uun. Kwa hakika Zanzibar tokea 1964 mpaka hii ni kama moto ambao unawaka ndani ya pango. Zanzibar inahitaji kufanyiwa visomo vizito damu za watu zimemwangwa sana.

  • @111dudi
    @111dudi 2 місяці тому +1

    The sultans never did this.

  • @Hussein_Mustafa_Parmar
    @Hussein_Mustafa_Parmar 16 днів тому

    Marxism socialism communism brutal and dictatoship of Nyerere

  • @MohdIkra-d7s
    @MohdIkra-d7s 22 дні тому

    Hemu asimame kiongozi mkuu wa nchiii hiii kisha atueleze kinaga ubaga hichi kilicho tokea hapa haswa kilikua nini na kinamaana gani na tafsiri yake ni nini kimsingi

  • @reubenalfred9707
    @reubenalfred9707 Місяць тому

    Wazanzibar wanachukiana wao kwa wao kuliko hata wanavyotichukia Tanganyika. Wakipta nafasi ya kujitawala basi damu itamwagika sana Zanzbar na inaweza isiwe nchi inayotawalika kwa miaka mingi sana

  • @salyali7807
    @salyali7807 5 місяців тому

    Inna lillah wainna ilayhi 😭😭😭😭

  • @ALIKHAMIS-un4fv
    @ALIKHAMIS-un4fv 2 місяці тому

    Innallilah wainna ilaih rajiun hawa wanaouliwa ni waislamu wenzetu duuh

    • @fahadfaraj6474
      @fahadfaraj6474 2 місяці тому

      Waislam wanakufa syria lebanon na Gaza

  • @printmedia1422
    @printmedia1422 2 роки тому

    Mombasa na maneno yalio tammkwa Siku Sonko alishinda kesi Mombasa, Inna mapishi ya ukatili Kama huo.... Kama Kenya itaendelea na mfumo ya kura za kabila kubwa kutawala
    Katiba ya maskizano iitwao Bomas Draft lazima iwe ndio njia ya kupeleka inchi

  • @azeezabdallaofficial5983
    @azeezabdallaofficial5983 2 роки тому

    Najisi mkubwa Malawi 🇲🇼 huna uzanzubari mchwara

  • @FettyKhamis-k1b
    @FettyKhamis-k1b Рік тому

    Mh watu wanauliwaa

  • @rastafare878
    @rastafare878 2 роки тому

    Allah Akbar

  • @iddijumaali7192
    @iddijumaali7192 3 роки тому

    Hee watu wanauliwa wao wanafurahia

  • @salumali2702
    @salumali2702 4 роки тому

    Dhulma tuuu nchi hiii