SIKILIZA SHAIRI ZURI ZA KUHUSU HARUSI YA NDUGU WAWILI WATOTO WA SHARIFU HUSSEIN BADAWY huko Mamburui

Поділитися
Вставка
  • Опубліковано 27 гру 2023
  • Mwanzo naanza isimu ∆∆∆ Ya Mola wangu Jaliya.
    Kiswalia na Hashimu ∆∆∆ Kipenzi tumwa Nabiya.
    Na Ali zake Kiramu ∆∆∆ Na swahaba nao piya.
    Nyuso leo zimeng'ara ∆∆∆ Kwa hili jambo la shani.
    Nami kwenye msafara ∆∆∆ Sina budi kuwa ndani.
    Kwetu ndio siku bora ∆∆∆ Ilomridhi Manani.
    Ni bwana abubakari ∆∆∆ Na nduguye muhidini.
    Wameianza safari ∆∆∆ Ya kuingia ndoani.
    Naomba iwe ya kheri ∆∆∆ Kwa baraka za amini.
    Pongezi wenye harusi ∆∆∆ Mambo yenu yamefana.
    Kwa nguvu zake Qudusi ∆∆∆ Wana wamependezana.
    Mola atawanafisi ∆∆∆ Kwa mahaba kushibana.
    Ni kwako Abu alama ∆∆∆ Mja ulo na hisani.
    Kwa kweli ulisimama ∆∆∆ Nae Sayidi Huseni.
    Kwa wema na kwa huruma ∆∆∆ Mukajenga utu ndani.
    Kazi tumeshuhudiya ∆∆∆ Uliyoifanya ndani.
    Bidii na yako niya ∆∆∆ 'Metowa tunda mtini.
    Leo chombo chaoleya ∆∆∆ Kimakini baharini.
    Safari waloiunda ∆∆∆ Mola aijaze kheri.
    Na chombo walichopanda ∆∆∆ Kisiingie dosari.
    Kweli moyo ukipenda ∆∆∆ Roho haina khiari.
    Ya Ilahi ya Rabana ∆∆∆ Ulo juu arshini.
    Waruzukiye na wana ∆∆∆ Tena wakupenda dini.
    Wasikiapo adhana ∆∆∆ Waende msikitini.
    Hapa nitasema basi ∆∆∆ Mbele sitoendeleya.
    Famili ya idarusi ∆∆∆ Na Huseni badawiya.
    Yawashukuru unasi ∆∆∆ Nyote mulohudhuriya.
  • Розваги

КОМЕНТАРІ • 3