Salama Na ANNA TIBAIJUKA SE6 EP58 | LA PROFESSEUR PART 1 | SendTip MPESA LIPA NO 5578460
Вставка
- Опубліковано 7 вер 2024
- #SalamaNa #SendTip Through MPESA #5578460
Nilipoandikiwa ujumbe mfupi na Edwin Bruno ambaye ni mkwe wa Professor kwamba Mama amekubalia kufanya kipindi na sisi siku hiyo ya Jumapili akishatoka church nilihisi kama naota. Mwenyezi Mungu anajua kwa kiasi gani tumekua tukitaka kufanya maongezi nae kwenye kipindi chetu. U busy wake na pengine mara nyingi kutokuwepo Dar es Salaam napo palikua panaleta ugumu, nyengine ilkua ni tarehe zetu za kufanya production na availability yake zilikua zinapishana sana. So unaweza ukaelewa excitement ambayo nilikua nayo baada ya finally samaki kujaa kwenye ndoana.
Professor Anna Tibaijuka ni LEGEND miongoni ma magwiji kwenye nchi hii kwa kazi yake na usomi wake na uzazi wake na kujibeba kwake. Kazi mbali mbali ambazo amewahi kuzifanya na kuliwakilisha Taifa hili zinajizungumza kwa sauti kubwa. Ila Safari yake mpaka anafikia kwenda kufanya kazi kwenye Taasisi kubwa duniani hakukumdondokea tu miguuni. Usomi wake ambao aliupambania toka akiwa mdogo na kupata ushirikiano kutoka kwa Marehemu Baba yake ndo kila kitu. Enzi ambazo mtoto wa kike alikua anaandaliwa kuwa Mama wa nyumbani, Baba yake aliamini zaidi kwenye kumpeleka mtoto wake shuleni na kwa mujibu wa Mama Tibaijuka Baba yake alikua aliwasisitiza wazee wenzake kufanya hivyo maana dunia ndo ilikua inaelekea huko, kuna ambao walimsikiliza na wengine ambao waliona anapoteza tu pesa na muda.
Mama Tibaijuka na Mimi tuliongelea kuhusu gharama za elimu enzi hizo Mimi nikidhani elimu “ilikua bure” pasi na kujua elimu kipindi hiko ilikua ghali pengine kuliko sasa na ukichukulia shule zenyewe zilikua mbali kweli kweli. Ananiambia pia suala la yeye kutaka kutomuangusha Baba yake ambaye baadhi ya watu walikua wanamcheka kwa kumpeleka Anna shuleni na kuingia gharama zote hizo. Pia ananiambia kuhusu Mama yake kufanya kazi zaidi ili masuala ya nyumbani aweze kuyafanya yeye ili kumsaidia mumewe ambaye pesa yake karibia yote alikua akilipia elimu ya Binti yake.
Mama Anna pia ananisimulia humu jinsi ambavyo aliposwa alipokua kidato cha tano na mchumba ilibidi amsubiri mpaka alipomaliza Chuo Kikuu. Nili enjoy kila sekunde ya maongezi haya ambayo kwa kiasi kikubwa naamini yatakua na faida kwetu sote. Ananihadithia pia jinsi ambavyo alienda Sweden na mumewe ambayo alikua huko kikazi na jinsi ambavyo alipata nafasi ya kusoma Chuo Kikuu BURE na ni nafasi ambayo aliipokea kwa mikono miwili na kuhakikisha hafanyi makosa.
Mama Anna ameshaifanyia Dunia hii mambo tele ya kimaendeleo wakati akifanya kazi zake UN na baada ya hapo alirudi nyumbani na kukifanya kazi Chama cha Mapinduzi kama Mbunge wa Muleba Kusini na Waziri wa Ardhi, nyumba na Maendeleo ya makazi. Hapo kwenye uwaziri sasa… Kulikua na mengi yaliyotokea wakati yeye yuko kwenye cheo hiko na ambayo kwa ki ufupi tu tuliyajadili kwenye meza yetu. Mama Anna yuko na Respect ya hali ya juu kwa Rais wa awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ambaye kwa kiasi kikubwa alimfanya Professor Tibaijuka arudi nyumbani na kulifaidisha Taifa na yale alojifunza wakati anafanya kazi huko kwenye Umoja wa Mataifa.
Yangu matumaini utaokota kadhaa kwenye maongezi yetu haya na kwa kiasi flani yatakusaidia kwenye maisha yako. Tafadhali enjoy pia.
Love,
Salama.
Support us through anchor.fm/yahs...
SUBSRIBE TO OUR CHANNEL bit.ly/YahSton...
Listen our Podcast on
Spotify Link spoti.fi/2Uxr6Cm
ApplePodcast Link apple.co/2Ou1bru
GooglePodcast Link bit.ly/GoogleP...
Audiomack Link bit.ly/YahSton...
UA-cam Link bit.ly/UA-camS...
Soundtrack Yeah by @MarcoChali • Marco Chali Feat One T...
Follow:
Twitter: / yahstonetown
Instagram: / yahstonetown
Facebook: / yahstonetown
Channel Administered by Slide Digital
Instagram: slidedigitaltz
Huyu Professor ana madini mengi sana. Kichwa chake ni hazina.
Uongozi sio kuongezeka vyeo..bali kuwasaidia watu kufikia malengo yao🙌🙌🙌🙌
I just loved the positivity and the Haya people perspectives😅😅😅😅
Hongera sana da Salama kwa kutuletea huyu bib Anna❤
Yupo sahihi kwa anayoyaelezaaa hongera akee❤
Wow...
Just wow...
Huyu mama nampenda sana...
Our UN habitat way maker. She paved the way for African/Tanzanian women
She stole money and akasema pesa ya mboga shame on her
She stolen not but she given hela ya mboga.
my role model. good interview.. ...asante sana Salama kwa kubuni kipindi. we love u
Kudos Prof. nimefurahi sana kukusikia ukiongelea kizazi cha wapigania uhuru, vijana wengi siku hizi wanayachukua haya mambo for granted na wanauona utamaduni wetu kama vile ni kero kwao.
Napenda Sana wakristo wanapotumia neno Alhamdulillah katika njia ya kumshukuru Allah ........... The powerful of Islamic
Sisi hatuna unaguzi wa kidini
Alhamdulilah sio uislam. Ni kiarabu. Kama wewe ulivyotumia hapo kiingereza cha mchongo.
It's an Arabic word not Islamic word
Kwa kweli yupo juu huyu mama asante salama
"Leadership is about raising others to achieve their goals".
Such a statement can only be given out by rich - hearted people, under the sun, like the Prof. Anna Tibaijuka herself.
May the Lord grant her healthful and long life.
I love the fact that she identifies herself more as an academic than a politician. Our current professors are struggling to erase their academic history in favour of political titles! "Umenitoa jalalani"
😂😂
Alhamdulillah nimemuelewa na nimejifunza...
I was just thinking how educational system haiendani na ulimwengu wa leo , Natumaini serikali itafanyia hili mabadiliko ili kujikwamua kiuchumi. Well said Mama Tibaijuka 👏
Watching from Nairobi Kenya. We love you mama. Respect Mungu akuongezee miaka na maisha mema.
Ukiangalia nyuma nakujuta Basi hujui ulipo na unapokwenda 🙏🙏
❤❤
We, academicians, are so proud of you Prof. Anna
Bado nimewahi naombeni like zenu ....
One of the best interviews Salama has ever done.
entreprenuership is an organizational skill, well put!! such a good interview.
Nakumbuka shule yangu Jangwani it was 💕 skills za kutosha unatoka umekamilika!
Mahojiani bora kuwahi kutokea. Prof. Anna Tibaijuka amefanya kazi kubwa ya kubadilisha mtazamo wa jamii kuhusu kumsomesha binti wa kike. Mungu akupe maisha marefu Profesa.
Hahahaha! Kwani kuna binti wa kiume ?
Ashakum si matusi!
Interview nzuri sana,yaan zaidi ya darasa Nimefurahia kuanzia mwanzo hadi mwisho.Hongera sana Salama na Prof . Anna Tibaijuka
Bonge moja la intervew,🙌🙌
Mama Anna kichwaa 👏👏👏👏 Asante Salama.
Kabla sijaanza kusikiliza nimeipenda
Hongera sana mama Prof Anna. Safari yako ya maisha ni chachu na msukumo chanya kwa watoto wetu wa kike na kiume pia. Endelea kushare uzoefu na maono yako kwa manufaa ya wengi...
"Kazi iliyombele yetu ni kubwa kuliko kule tunakotoka." 🙌
Very very beautiful interview Mungu ambariki sana Mama Anna Tibaijuka
Prof. Tibajuka ❤ you are the best mama . May God bless you mama
Ni enjoy hilo jibu kuhusu mfumo wa elimu
Hongera sana salama kwa mama yetu, nampenda sana mama tibaijuka, ni role model wangu, namkubali sana
Jamani...hii vision ya babaake ndio iliyofanya tumjue leo huyu muheshimiwa ANNA....🤗🤗 I wish my father could 😭
Mhayaaa
Hongera Mama ana
Salama nafuatilia sana kazi zako tangu enzi za Mkasi ila huwa unaboa sana kitu kimoja, una masuali ya kurukaruka mambo muhimu, mfano huyo mama ni mtu muhimu sana kwa kizazi cha leo na vijavyo, wanapaswa kumfahamu kiundani ili waige mazuri yake lakini sasa wewe unaanza na suali eti kuhusiana na kuingia kwenye siasa, kwa nini usiyatazame maisha yake kwa mpangilio mzuri kuanzia wazazi wake, kuzaliwa, makuzi, kusoma, kazi, siasa mpaka sasa, unarukaruka na kuacha mambo muhimu hii sipendi kabisa.
Anzisha chako usiwe unarukaruka...Nadhani utatisha sana! Pia asante kwa KUFUATILIA SANA!
Interesting interview
Wahaya ndomana wanafanikiwa sana
Du mama ni noma
❤❤❤!!!!!. Guys!!!!, Frankly speaking!!!, This woman is very very 🧠 🧠 intelligent!!!!!.
Awesome
👌🏽
Mother anaongea vizur 🙌
Hatari sana mama kasoma hadi kasoma tena…NICE one Prof, too bad ckhz tumebaki na ma Prof wa kupost picha za kubenjua makalio tu insta
👏👏👏👊👊
😅😅😅
BOB HAHAHA
Pesa ya mboga imemuharibia
Kusoma kwake kumesaidia nini taifa zaidi ya kujinufaisha yeye mwenyewe
Nimeipenda hii👍
Iwe bojooooo
Waitu oliyo bojo?
Salama! you are the best!
Nice interview
Ability Vs Willingness 🙌🙌
My role model,educated woman Prof Anna Tibaijuka.
Loved this, i laughed the whole part two section
one of the best interview 🙌 👌 Tunajivunia mama Anna Tibaijuka
Bonge ya interview 🙌
If professor you read these comments,, I love you from my heart
Interview kali sana 👏👏
Dah! Akili kubwa...kumuelewa unatakiwa kukaa kwa kutulia sana, atema madini mda wote.
2024 still hii ni best interview
Prof yuko vzr sana,kuna vijana weng sana wanadgree mtaani lakin wamefungua migahawa
one of the best interview hongera sanaa salama
Inasikitisha sana sihasa inavyowageuza wasomi wetu kuwa wabinafsi waliopitiliza na kuweka taaluma zao kando.
Prof upo vizuri sanaa
Such a lovely interview, my lovely sister Salama you are the best. ❤
My rolemodel 😍😍😍
Mama kichwa sana, sema Siasa zilitaka kumuharibia IQ yake lkn mtu ambaye ni msomi kweli na ni icon ya wahaya
Nilisoma story za huyu mama I guess form three or form four
Natamani Salama siku moja nae amhoji Salama!... nimependa sana hii interview
Pia nimejifunza mengi sana. With my headphones on nimejikuta na nod mara nyingi kupiliza. Mama katema madini aisee
mafanikio ni product ya teamwork na mazingira 👏
Interview nzur sana
Life is what you make it!
Miongoni mwa Interviews bora kabisa.
Wakurungwa mmeshawahi
Love you Mama.
Kazi iendelee
Interview nzuri sana
powerfull
The best interview ever❤ #SALAMA NA PROF ANNA TIBAIJUKA
Very nice Interview
Mama kuna Newyork city kule Muleba
I underestimated this mama🙌🙌🙌
Wazazi walikuwa na maono kweli.
Wapili
Huyu mama Yuko vizuri sana .
First
Mjanja mjanja
Huyu Mama Ana Akili sana
Ameongea ki2 ambacho serikali kwa ujumla inatakiwa kuzingatia sana juu ya elimu
Anna
Hii interview nitaitunza kwa ajili ya mwanangu wa kike
uyu mama anajielewa sana.
Mama hauna ha mjakazi angalau........ningekua na wewe ningefaidika sana. Napenda ushauri wako, napenda maamuzi yako.
MHAYA
kohoa upate tonge nan mwingine kaiona iyo
Dada Salama, Boresha kwenye Uulizaji wa Maswali... unauliza maswali laini sana naweza sema hivyo, tunahitaji kujifunza zaidi.
Onesha mfano wa maswali magumu ambayo ulitamani angeuliza.
Khaaaa wewe sio mfuatiliaji salama ana uzoefu sio wa jana ni longtime ago in Bethlehem
@@hellendaniel3809 Salama nimeanza kumfatilia tangu yupo Chanel 5 MKASI, ni long time namfahamu kuliko Unavyodhani... Ebu mfatilie Stanislaus Lambat wa Dar24 ndio utanielewa ni nini namaanisha.
Exactly Ile scandal ya wizi ilimshusha kiasi gan mpaka akasema pesa ya mboga. Nilitaka kufahamu haya mengine Utopolo tu
Hakuna muulizaji Wa maswali magumu hapa bongo kama huyu Salama wengne wte hamna kitu
Nice MAMA
Tunataka interview na zumaridi!
Duu Prof Akili kubwa
👏👏👏❤
Tunaomba utuletee zimbwe junior Mohamed hussein
Namuona ebitoke😆😆ni utani jmn sina mwanasheria
🇹🇿🇹🇿🇹🇿✌️👊
👏👏👏👏👏👍👍👍👍
Not she is a crook just like any politician in Bongo. Her, bishops et al, was given a lot of stolen money. When she got caught, she claimed she gave the money to a private school as a gift.