KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH: IBADA YA MORNING GLORY: THE SCHOOL OF HEALING 03/ 07/ 2024

Поділитися
Вставка
  • Опубліковано 1 лип 2024
  • KIJITONYAMA LUTHERAN CHURCH: IBADA YA MORNING GLORY: THE SCHOOL OF HEALING 03/ 07/ 2024
    UJUMBE WA LEO: VITA YA KESHO YAKO
    [SEHEMU YA PILI]
    Hagai 2 : 9
    Mathayo 16 : 19
    Kumbu 8 : 3
    Mwanzo 41 : 25 - 49
    1 Wafalme 3 : 11 - 13
    2 Wafalme 5 : 26 - 27
    Hagai 2 : 9
    9 Utukufu wa mwisho wa nyumba hii utakuwa mkuu kuliko utukufu wake wa kwanza, asema Bwana wa majeshi; na katika mahali hapa nitawapa amani, asema Bwana wa majeshi.
    Mathayo 16 : 19
    19 Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni.
    Kumbu 8 : 3
    3 Akakutweza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha Bwana.
    1 Wafalme 3 : 11 - 13
    11 Mungu akamwambia, Kwa kuwa umeomba neno hili, wala hukujitakia maisha ya siku nyingi; wala hukutaka utajiri kwa nafsi yako; wala hukutaka roho za adui zako; bali umejitakia akili za kujua kuhukumu;
    12 basi, tazama, nimefanya kama ulivyosema. Tazama, nimekupa moyo wa hekima na wa akili; hata kabla yako hapakuwa na mtu kama wewe, wala baada yako hatainuka mtu kama wewe.
    13 Na mambo yale usiyoyaomba nimekupa, mali na fahari, hata hapatakuwa na mtu katika wafalme kama wewe, siku zako zote.
    2 Wafalme 5 : 26 - 27
    26 Akamwambia, Je! Moyo wangu haukuenda na wewe, hapo alipogeuka yule mtu katika gari ili akulaki? Je! Huu ndio wakati wa kupokea fedha, na kupokea mavazi, na mashamba ya mizeituni, na mizabibu, na kondoo, na ng'ombe, na watumwa, na wajakazi?
    27 Basi ukoma wa Naamani utakushika wewe, na wazao wako hata milele. Naye akatoka usoni pake mwenye ukoma kama theluji.
    Mwanzo 41 : 25 - 49
    25 Yusufu akamwambia Farao, Ndoto ya Farao ni moja; Mungu amemwonyesha Farao atakayoyafanya hivi karibu.
    26 Wale ng'ombe saba wema ni miaka saba; na yale masuke saba mema ni miaka saba. Ndoto ni moja.
    27 Na wale ng'ombe saba, dhaifu, wabaya, waliopanda baada yao, ni miaka saba; na yale masuke saba matupu yaliyokaushwa na upepo wa mashariki, yatakuwa miaka saba ya njaa.
    28 Ndivyo nilivyomwambia Farao, ya kwamba Mungu amemwonyesha Farao atakayoyafanya hivi karibu.
    29 Tazama, miaka saba ya shibe inakuja, katika nchi yote ya Misri.
    30 Kisha kutakuja miaka saba ya njaa baada yake; na shibe ile yote itasahauliwa katika nchi ya Misri, na njaa itaiharibu nchi.
    31 Wala shibe ile haitajulikana katika nchi kwa sababu ya njaa inayokuja baadaye, maana itakuwa nzito sana.
    32 Na ndoto ya Farao kwa vile ilivyokuja mara mbili, ni kwa sababu neno hilo Mungu amelithibitisha, na Mungu atalitimiza upesi.
    AGENDA ZA MAOMBI
    1. TOBA.
    2. Shukrani kwa Miezi sita 2024.
    3. Omba Neema ya Mungu.
    4. Omba uwepo wa Bwana uende pamoja nawe.
    5. Omba Mungu akuepushe na Majaribu yasiyobeba kitu kwa ajili yako.
    6. Kuombea Akili
    Mhubiri: Mwl. Eng. Googluck Mushi.
    Kwa maombi na ushauri :
    Mch. Kiongozi: Dr. Eliona Kimaro
    Simu: +255 655 516 053, +255 754 516 053
    Mch. Msaidizi: Anna Kuyonga
    Simu: +255 713 553 443
    UA-cam: Kijitonyama Lutheran church
    Barua Pepe: Kijitonyamalutheran@gmail.com

КОМЕНТАРІ • 7